Uchaguzi 2020 Taarifa ya kujitoa kwa mgombea Ubunge jimbo la Ulyankulu kupitia CHADEMA

Mocumentary

JF-Expert Member
Jul 31, 2017
769
1,959
Tafadhali rejea mada tajwa hapo juu.kumbukumbu namba ya tarehe 29/08/2020 kutoka kwa ndugu Lazaro Stephano Maige ambaye tarehe 25/08/2020 aliteuliwa kuwa mgombea nafasi ya Ubunge kwa Jimbo la Ulyankulu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akinijulisha kwamba amejitoa kugombea nafasi hiyo.

Kufuatia kujitoa kwa Mgombea Ubunge wa jimbo la Ulyankulu ndugu Lazaro Stephano Maige kutokea Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kumwacha mgombea nafasi ya Ubunge Jimbo la Ulyankulu Bi. Rehema Juma Migilla kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa mgombea pekee.

Kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura 343 inafafanua kuwa, endapo mgombea aliyeteuliwa ni mmoja atahesabika kuwa amechaguliwa na upigaji kura hautafanyika katika jimbo hilo kwa uchaguzi wa mbunge.

Kwa barua hii, kutokana na maelezo yaliyopo hapo juu, ninakutaarifu kuwa, umepita bila kupingwa, hivyo mara baada ya Uchaguzi kukamilika utapatiwa hati ya kuchaguliwa.

IMG_20200904_200327.jpg
 
Huyo ni mgombea na hela zake jumlisha hela za chama, mtihani mkubwa kwa wawakilishi wa chama siku ya upigaji kura, anaishi nyumba ya kupanga, kaenda kwenye uchaguzi kwa sababu tu haingii kazini siku hiyo, watoto wapo shule, mwenye nyumba anadai chake, jumlisha mengineyo
 
Halafu kuna mjinga fulani kisa amekaa Ulaya Uchochoroni, eti anafanya kampeni kuwa Rais wa Tanzania. My foot!!
Kumuita Mtu mjinga kisa tu humpendi ni kiwango kikubwa sana cha immaturity

Mmeshamnunua huyo, let's wait and see! Huna haja ya kumtusi mtu, hata ukitumia lugha ya kawaida unaweza kuelezea tu jambo lako hata ni la kipuuzi likaeleweka kwa upuuzi huo!
 
Huyo kashafika bei, shida ya upinzani ni wabinafsi, hawawezi kuacha kununuliwa

Hata Lissu alipoambiwa watampa kikazi kidogodogo, hizo ni dalili za kumnunua ajitoe
Kweli. Hata Lissu anajitangaza ili "anunuliwe" ikiwezekana na mabeberu.
 
Mambo yanazidi kua matam, kwahio kuna wanachama wa cdm ambao watapigia kura ccm! uchaguzi mtam sana huu, wale warembo wa mbowe wa praise and worship wanasemaje juu ya hili, nlisema kuna watu 6 watahamia ccm kwa taarifa zangu za ndan bado wanne nnaowajua
 
Upinzani nchi hii, unanunulika kirahisi sana. Hadi sasa naamini kabisa, mpinzani wa roho na mwili(kwa viongozi wa juu) ni Lissu TU.
Aise hata mbowe sio mupinzani tena? Bali ni lisu pekee.
 
Back
Top Bottom