Taarifa kwa umma kuhusu madai ya TRA kupandisha ushuru wa magari toka nje ya nchi

TRA Tanzania

Member
Jul 16, 2022
77
222
Kufuatia taarifa iliyoko katika mtandao wa Kijamii ikidai TRA imepandisha ushuru wa magari tunapenda kukanusha na kufafanua kama ifuatavyo;

1. Viwango vya kodi vinapitishwa na bunge na sio TRA.

2.Kodi hukokotolewa kwa kuzingatia thamani ya gari kwenye soko la dunia, gharama ya usafirishaji na bima. Ikiwa gari limenunuliwa kwa fedha za kigeni kiwango cha kubadilisha fedha cha siku husika kitatumika na sio ya wakati wa kuagiza gari hilo hivyo huenda ikatofuatiana na kiwango cha kikokotoo wakati wa kuagiza.

3. Umri wa gari unaweza kusababisha kodi ikaongezeka kutokana na uchakavu, kwa magari yaliyotengenezwa zaidi ya miaka 8 lakini haifiki miaka 10 kodi ya uchakavu ni 15% na gari lenye umri kuanzia miaka kumi na kuendelea tangu limetengenezwa kodi ya uchakavu ni 30%.

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi bure kwa simu namba 0800110016 au 0800 750075 au 0800 780078 siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia saa 2 kamili asubuhi mpaka saa 1 kamili jioni au tuma barua pepe kwenda huduma@tra.go.tz.

Pamoja tunajenga taifa letu

Imetolewa na: Idara ya Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano
 
Kufuatia taarifa iliyoko katika mtandao wa Kijamii ikidai TRA imepandisha ushuru wa magari tunapenda kukanusha na kufafanua kama ifuatavyo;

1. Viwango vya kodi vinapitishwa na bunge na sio TRA.

2.Kodi hukokotolewa kwa kuzingatia thamani ya gari kwenye soko la dunia, gharama ya usafirishaji na bima. Ikiwa gari limenunuliwa kwa fedha za kigeni kiwango cha kubadilisha fedha cha siku husika kitatumika na sio ya wakati wa kuagiza gari hilo hivyo huenda ikatofuatiana na kiwango cha kikokotoo wakati wa kuagiza.

3. Umri wa gari unaweza kusababisha kodi ikaongezeka kutokana na uchakavu, kwa magari yaliyotengenezwa zaidi ya miaka 8 lakini haifiki miaka 10 kodi ya uchakavu ni 15% na gari lenye umri kuanzia miaka kumi na kuendelea tangu limetengenezwa kodi ya uchakavu ni 30%.

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi bure kwa simu namba 0800110016 au 0800 750075 au 0800 780078 siku ya Jumatatu mpaka Ijumaa kuanzia saa 2 kamili asubuhi mpaka saa 1 kamili jioni au tuma barua pepe kwenda huduma@tra.go.tz.

Pamoja tunajenga taifa letu

Imetolewa na: Idara ya Elimu kwa Mlipakodi na Mawasiliano

Good
 
Hii sheria ya kuwekea magari yenye umri mkubwa sio sahihi kabisa inamaana mtu akiwekewa kodi kubwa na akalipa je garii itapungua umri? Tusidanganyane watanzania kununua gari yenye umri mdogo uchumi kwa wengi hauturuhusu tutapambania magari ya 2005-2009 huko
 
Ni sahihi

Dunia inapokabiliwa na uhaba wa Dola, nyakati kama hizi ni sahihi na busara kudhibiti matumizi ya forex.


wakati wa Mwl Nyerere tulipitia kipindi kama hiki na ikatulazimu tupate kibali cha Governor mwenyewe kupata dola
 
Nje ya mada kidogo; kwa nini mnatoza kodi kubwa hata zaidi ya gharama ya kununulia na kusafirishia gari husika toka Japan kwa mfano hali hamjashiriki japo kwenye utengenezaji wa indicator ya gari lenyewe? Nani wa kulaumiwa katika uporaji huu na kumnyima raia wa kawaida haki ya kumiliki chombo hiki muhimu kwa familia na mtu mmoja mmoja?
 
Maana yake kwa wale waliokuwa wanasapoti kwamba Bandari apewe Mwarabu

Kwasababu walidhani kuna watu pale Bandarini wanafanya upigaji unaosababisha raia watozwe pesa nyingi wanapoagiza bidhaa zao.

Kupitia tangazo lenu maana yake watu washajionea kumbe upigaji unaamzia Dodoma unakuja kutekelezwa Bandarini.
 
Huyu mnayemuuliza maswali ya msingi ni karani katumwa apandishe taarifa ktk kurasa rasmi ya TRA JF na sio muhusika. Ukitaka kupata taarifa vizuri hakikisha unakutana na watendaji wakuu watakupa options zote walizonazo.
 
Nje ya mada kidogo; kwa nini mnatoza kodi kubwa hata zaidi ya gharama ya kununulia na kusafirishia gari husika toka Japan kwa mfano hali hamjashiriki japo kwenye utengenezaji wa indicator ya gari lenyewe? Nani wa kulaumiwa katika uporaji huu na kumnyima raia wa kawaida haki ya kumiliki chombo hiki muhimu kwa familia na mtu mmoja mmoja?
Gharama za kuingiza magari Tanzania ziko fair kabisa sidhani itakuwa busara kupunguza zaidi ya hapa zilipo. Hata rate ya kuingiza magari ni nzuri sana na hii inamaanisha kuwa kodi zinalipika. Gharama zikupunguzwa zitafanya nchi igeuke jalala la magari chakafu na pia msongamano wa magari. Cha muhimu ni kuwa fedha zinatopatikana zitumike kwenye maendeleo ya nchi na siyo jinsi zinavyotapanywa sasa hivi kwa viongozi kuishi maisha ya anasa.
 
Back
Top Bottom