kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
SIO siri kuwa hivi sasa, taaluma ya ualimu imepoteza hadhi katika jamii. Ile fahari ya kujiita ama kuitwa mwalimu kama ilivyokuwa zamani, sasa imepotea.
Vijana wengi wanaukimbia ualimu kwa kile wanachodai kuwa haulipi kimaisha.Hata wazazi nyumbani, wanashtadi kuwaeleza watoto wao uzuri wa fani kama udaktari, uhasibu na nyinginezo, huku wakiusema vibaya ualimu.
Ilivyo sasa, ualimu unaonekana kuwa taaluma kimbilio la watu waliopoteza matumaini ya kufanikiwa katika taaluma nyingine au wale wanaofeli katika mitihani. Hata fikra za wanajamii zimejengwa katika kuamini hili.
Haya yananikumbusha kauli ya Ofisa Mchechemuaji wa sera katika asasi ya mtandao wa elimu Tanzania(TenMet), Florence Katabazi aliyewahi kusema kuwa katika hali hii si ajabu kuona kati ya walimu 10,000 ni 400 tu wenye sifa na haiba ya ualimu.
Lakini kwa nini tumefika hapa? Wafuatiliaji wa masuala ya elimu wanaweza kuorodhesha lundo la sababu ikiwemo maslahi madogo wanayopata walimu.
Taarifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco) ya mwaka 2009 inasema mwaka 1975, Tanzania ilikuwa ikiongoza kwa kuwalipa mishahara mizuri walimu wake kuliko nchi kadhaa za Afrika Mashariki na Kusini ikifuatiwa na Burundi.
Mwaka 2004, hali ikabadilika, mishahara ya walimu Tanzania ni midogo zaidi ikilinganishwa na mishahara ya walimu katika nchi kama Kenya, Msumbiji, Malawi na Rwanda.
Kama haitoshi, walimu Tanzania wanalia kwa kufanya kazi katika mazingira duni, hawana vifaa stahiki huku mwajiri wao akishindwa kuwaendeleza kitaaluma. Haya yote yanachangia kupungua kwa hamasa ya watu kujiunga na taaluma ya ualimu, hivyo kukuza tatizo la uhaba wa walimu shuleni.
Utafiti kuhusu walimu wanafunzi uliofanywa na Towse na wenzake mwaka 2007, unaonyesha asilimia 10 ya walimu wa kiume na asilimia 15 ya walimu wa kike walisema ualimu ndio uliokuwa chaguo lao la kwanza huku asilimia 37 wakisema waliamua kuwa walimu baada ya kupata alama za chini katika matokeo ya mitihani yao.
Hivi ndivyo hali ya ualimu ilivyo nchini. Kumbe kuna watu walioingia katika kazi hii adhimu bila ya ridhaa ya nafsi zao. Kwa sura hii, si ajabu kuona ama kusikia madudu yanayofanywa na walimu wetu ambao kumbe moyoni hawautaki ualimu!
Hata hivyo, tufanye nini kuleta nafuu katika taaluma hii? Kwanza serikali iimarishe Mkakati wa Maendeleo na Menejimentti ya ualimu(TDMS)ambao pamoja na mambo mengine unalenga kuondoa changamoto zinazowakabili walimu.
Mdau wa Elimu Mbaraka Madenge, mkazi wa Mbezi Samaki jijini Dar es Salaam, anasema walimu pia wanatakiwa wapewe mafunzo kulingana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia Walimu wanatakiwa kupewa kipaumbele kwa kuwekewa kompyuta shuleni ili waweze kujifunza vitu vingi vya dunia ya leo.
Kwa upande wake, ripoti ya Unesco inashauri kuwa kuwepo kwa motisha maalumu kwa walimu wanaopangiwa kazi katika maeneo ya pembezoni.
Mapendekezo mengine ni kupandishwa madaraja haraka, kupandishwa mishahara, kupewa posho ya usafiri na nyumba, kupewa nyumba, likizo maalumu ya masomo au fursa ya kupata mafunzo.
Jambo jingine linaloweza kurejesha hadhi ya walimu ni pamoja na kupewa fursa ya kujiendeleza kitaaluma kama ilivyoelezwa katika ripoti. Hili litasaidia kupunguza utoro hasa baada ya walimu kunyimwa nafasi ya kusoma.
Aidha, semina na mafunzo mbalimbali yaandaliwe ili kuwawezesha walimu kujua haki zao za msingi na kuzipigania pale inapotakiwa.
Inatia moyo kusikia serikali imeridhia uanzishwaji wa Bodi ya Kitaaluma ya Walimu ambayo pamoja na mambo mengine itasimamia maadili ya ualimu.
Nashauri chombo hiki kisiishie tu katika kudhibiti walimu, lakini kiwe chombo kitakachobadili taaluma ya ualimu kwa jumla na kutetea maslahi ya walimu ili ualimu nao ugeuke kuwa taaluma yenye hadhi katika jamii kama zilivyo taaluma nyingine.
Furaha Maugo ni mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi 0765434357
Vijana wengi wanaukimbia ualimu kwa kile wanachodai kuwa haulipi kimaisha.Hata wazazi nyumbani, wanashtadi kuwaeleza watoto wao uzuri wa fani kama udaktari, uhasibu na nyinginezo, huku wakiusema vibaya ualimu.
Ilivyo sasa, ualimu unaonekana kuwa taaluma kimbilio la watu waliopoteza matumaini ya kufanikiwa katika taaluma nyingine au wale wanaofeli katika mitihani. Hata fikra za wanajamii zimejengwa katika kuamini hili.
Haya yananikumbusha kauli ya Ofisa Mchechemuaji wa sera katika asasi ya mtandao wa elimu Tanzania(TenMet), Florence Katabazi aliyewahi kusema kuwa katika hali hii si ajabu kuona kati ya walimu 10,000 ni 400 tu wenye sifa na haiba ya ualimu.
Lakini kwa nini tumefika hapa? Wafuatiliaji wa masuala ya elimu wanaweza kuorodhesha lundo la sababu ikiwemo maslahi madogo wanayopata walimu.
Taarifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Elimu, Sayansi na Utamaduni (Unesco) ya mwaka 2009 inasema mwaka 1975, Tanzania ilikuwa ikiongoza kwa kuwalipa mishahara mizuri walimu wake kuliko nchi kadhaa za Afrika Mashariki na Kusini ikifuatiwa na Burundi.
Mwaka 2004, hali ikabadilika, mishahara ya walimu Tanzania ni midogo zaidi ikilinganishwa na mishahara ya walimu katika nchi kama Kenya, Msumbiji, Malawi na Rwanda.
Kama haitoshi, walimu Tanzania wanalia kwa kufanya kazi katika mazingira duni, hawana vifaa stahiki huku mwajiri wao akishindwa kuwaendeleza kitaaluma. Haya yote yanachangia kupungua kwa hamasa ya watu kujiunga na taaluma ya ualimu, hivyo kukuza tatizo la uhaba wa walimu shuleni.
Utafiti kuhusu walimu wanafunzi uliofanywa na Towse na wenzake mwaka 2007, unaonyesha asilimia 10 ya walimu wa kiume na asilimia 15 ya walimu wa kike walisema ualimu ndio uliokuwa chaguo lao la kwanza huku asilimia 37 wakisema waliamua kuwa walimu baada ya kupata alama za chini katika matokeo ya mitihani yao.
Hivi ndivyo hali ya ualimu ilivyo nchini. Kumbe kuna watu walioingia katika kazi hii adhimu bila ya ridhaa ya nafsi zao. Kwa sura hii, si ajabu kuona ama kusikia madudu yanayofanywa na walimu wetu ambao kumbe moyoni hawautaki ualimu!
Hata hivyo, tufanye nini kuleta nafuu katika taaluma hii? Kwanza serikali iimarishe Mkakati wa Maendeleo na Menejimentti ya ualimu(TDMS)ambao pamoja na mambo mengine unalenga kuondoa changamoto zinazowakabili walimu.
Mdau wa Elimu Mbaraka Madenge, mkazi wa Mbezi Samaki jijini Dar es Salaam, anasema walimu pia wanatakiwa wapewe mafunzo kulingana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia Walimu wanatakiwa kupewa kipaumbele kwa kuwekewa kompyuta shuleni ili waweze kujifunza vitu vingi vya dunia ya leo.
Kwa upande wake, ripoti ya Unesco inashauri kuwa kuwepo kwa motisha maalumu kwa walimu wanaopangiwa kazi katika maeneo ya pembezoni.
Mapendekezo mengine ni kupandishwa madaraja haraka, kupandishwa mishahara, kupewa posho ya usafiri na nyumba, kupewa nyumba, likizo maalumu ya masomo au fursa ya kupata mafunzo.
Jambo jingine linaloweza kurejesha hadhi ya walimu ni pamoja na kupewa fursa ya kujiendeleza kitaaluma kama ilivyoelezwa katika ripoti. Hili litasaidia kupunguza utoro hasa baada ya walimu kunyimwa nafasi ya kusoma.
Aidha, semina na mafunzo mbalimbali yaandaliwe ili kuwawezesha walimu kujua haki zao za msingi na kuzipigania pale inapotakiwa.
Inatia moyo kusikia serikali imeridhia uanzishwaji wa Bodi ya Kitaaluma ya Walimu ambayo pamoja na mambo mengine itasimamia maadili ya ualimu.
Nashauri chombo hiki kisiishie tu katika kudhibiti walimu, lakini kiwe chombo kitakachobadili taaluma ya ualimu kwa jumla na kutetea maslahi ya walimu ili ualimu nao ugeuke kuwa taaluma yenye hadhi katika jamii kama zilivyo taaluma nyingine.
Furaha Maugo ni mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi 0765434357