Taabani majinuni sina hamu!.

Taabani majinuni sina hamu!.

KENZY

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2015
Posts
35,752
Reaction score
86,393
Samaleko...

Nilikutana na binti fulani wenyewe wanasema English figure!, kitoto cheupe rangi ya mtume, kilichonipendeza zaidi ni muonekano wa sura yake!, anamacho fulani hivi akikuangalia unaweza ukahisi anakutaka ama ameshakukubalia!.. basi hicho ndicho kimenifanya niwe taabani majinuni nisiekuwa na hamu!.

Shida ilianzia hapa, siku ya kwanza nilikutana nae eneo lake la kazi nikamsemesha!, ajabu akawa amenikazia macho sana nikamwambia shida yangu akanihudumia japo alikosea order ila siku mind!.
siku nyengine ikawa hivyohivyo kila nikikutananae basi hata kama hatutasemeshana lkn lazima macho yangu na yake yakutane na kwa namna alivyokuwa ananiangalia nikaanza kushituka kuna nini kinaendelea..?!

Shababi bin malavidavi nikajua mtoto ameshanielewa!, nikaona huyu nikiimbisha tu hachomoi tena nikaona sitaki habari zakuomba namba naenda kumface ana kwa ana!.
kama wasemavyo waswahili "usiku wa deni haukawii kukucha!". siku ikawadia nikamuita mtoto nikaanza kuimbisha mubashara, mtoto akawa anaendelea kuniangalia lilelile jicho lake lakunivuruga basi hapo mimi ndo najua kadata na kaelewa mistari, basi jasusi la mahaba nikawa nashuka tu madude!, japo muda mwengine alikuwa akionyesha kama kutokunielewa hivi lkn nikawa natambaa na biti kama Ngwair kwenye wimbo wake wa "She got a gwan".

Nilimwaga sera zangu pale, huku nikijiachia na swaga zangu zakinyamwezi lakini hatima yake alinikataa, yani hakuomba hata anifikirie ni aliichapa palepale!. ule unyamwezi niliokuwa nimeuvaa ukavulika!, yale maneno yakijasusi mahaba yakatokomea pasipo fahamika!.. kwanini..? kwasababu mimi nilienda nikiwa natambua huyu hapindui maana dalili alikuwa ameshanionyesha.
niliondoka lile eneo nikiwa kama mtu alienyimwa kitambulisho cha NIDA!.

Ikapita wiki nikaja kurudi anapofanya kazi sasa hapo ndipo nilipokuja kuelewa kuwa ile angalia yake ilikuwa na maana gani!, kumbe yule mtoto anatatizo la usikivu yani kusikia anasikia lakini usikivu wake si mkubwa!, hivyo mara nyingi anakuwa anaangalia mtu mdomoni anavyoongea ili aweze kuelewa unaongea nini kwa maneno ambayo hatayasikia!..

Mimi baada yakugundua hilo kusema kweli nimejikuta najilaumu sana kwa kushindwa kumuelewa toka awali, hivyo nikaamua kutanguliza hamu zangu kumbe dada wa watu wala hana shida na huba langu!, hapa nipo taabani majinuni sasahivi nahesabika kama jitu la hovyo mbele zake!.
 
Samaleko...

Nilikutana na binti fulani wenyewe wanasema English figure!, kitoto cheupe rangi ya mtume, kilichonipendeza zaidi ni muonekano wa sura yake!, anamacho fulani hivi akikuangalia unaweza ukahisi anakutaka ama ameshakukubalia!.. basi hicho ndicho kimenifanya niwe taabani majinuni nisiekuwa na hamu!.

Shida ilianzia hapa, siku ya kwanza nilikutana nae eneo lake la kazi nikamsemesha!, ajabu akawa amenikazia macho sana nikamwambia shida yangu akanihudumia japo alikosea order ila siku mind!.
siku nyengine ikawa hivyohivyo kila nikikutananae basi hata kama hatutasemeshana lkn lazima macho yangu na yake yakutane na kwa namna alivyokuwa ananiangalia nikaanza kushituka kuna nini kinaendelea..?!

Shababi bin malavidavi nikajua mtoto ameshanielewa!, nikaona huyu nikiimbisha tu hachomoi tena nikaona sitaki habari zakuomba namba naenda kumface ana kwa ana!.
kama wasemavyo waswahili "usiku wa deni haukawii kukucha!". siku ikawadia nikamuita mtoto nikaanza kuimbisha mubashara, mtoto akawa anaendelea kuniangalia lilelile jicho lake lakunivuruga basi hapo mimi ndo najua kadata na kaelewa mistari, basi jasusi la mahaba nikawa nashuka tu madude!, japo muda mwengine alikuwa akionyesha kama kutokunielewa hivi lkn nikawa natambaa na biti kama Ngwair kwenye wimbo wake wa "She got a gwan".

Nilimwaga sera zangu pale, huku nikijiachia na swaga zangu zakinyamwezi lakini hatima yake alinikataa, yani hakuomba hata anifikirie ni aliichapa palepale!. ule unyamwezi niliokuwa nimeuvaa ukavulika!, yale maneno yakijasusi mahaba yakatokomea pasipo fahamika!.. kwanini..? kwasababu mimi nilienda nikiwa natambua huyu hapindui maana dalili alikuwa ameshanionyesha.
niliondoka lile eneo nikiwa kama mtu alienyimwa kitambulisho cha NIDA!.

Ikapita wiki nikaja kurudi anapofanya kazi sasa hapo ndipo nilipokuja kuelewa kuwa ile angalia yake ilikuwa na maana gani!, kumbe yule mtoto anatatizo la usikivu yani kusikia anasikia lakini usikivu wake si mkubwa!, hivyo mara nyingi anakuwa anaangalia mtu mdomoni anavyoongea ili aweze kuelewa unaongea nini kwa maneno ambayo hatayasikia!..

Mimi baada yakugundua hilo kusema kweli nimejikuta najilaumu sana kwa kushindwa kumuelewa toka awali, hivyo nikaamua kutanguliza hamu zangu kumbe dada wa watu wala hana shida na huba langu!, hapa nipo taabani majinuni sasahivi nahesabika kama jitu la hovyo mbele zake!.
Dah,

Story hii kabla sijafika robo kuisoma nilihisi itaishia hivyo hivyo tu!
 
walekum salam rahmatullah wAbarakatuh sheikh
Kitten Supplies.jpeg
 
Kwanini uhesabike hivyo? Kumueleza mtu hisia zako hakukufanyi kuwa mtu wa hovyo, ila kumlazimisha akubali tongozo ndio uhovyo unapoanzia.
wewe hujui uhovyo unaanzia wapi nimeamua kuminya sijaandika yote..😅
 
Back
Top Bottom