Taa ya Solar Wakawaka

Kitia

JF-Expert Member
Dec 2, 2006
418
74
Wakawaka light.jpg

Kuna hii ya Solar ambayo nimeifanyia utafiti kwa muda wa mwaka mmoja na nimethibitisha kuwa hii taa ni madhubuti na inakidhi sifa ambazo watengenezaji wake wamezipa.

Wakawaka.jpg

Hii taa ni taa ndogo, mbadala wa kibatari. Ukichaji siku moja unaweza kutumia kwa siku 5 ndipo inafifia na kuzima kabisa. Kwa maeneo yetu ya Tanzania yenye mwanga wa jua mkali ni dhahiri kwamba utakuwa na taa ya uhakikamuda wote.

Watchman with wakawaka.jpg

Taa yenyewe inatumia mwanga wa jua kuchaji betri tatu za AA za kuchaji, ambazo uhai wake ni miaka mitatu ndipo utabidi uzibadilishe uziweke mpya.

Batteries.jpg

Kwa hesabu za haraka haraka taa hii inaleta unafuu wa gharama ukilinganisha na bei ya mafuta ya taa utakayonunua kwa miaka mitatu. Kama nilivyosema taa hizi ni mbadala wa kibatari, na hata pale umeme unapokatika, kuwa nayo kwenye gari au hata ukisafiri.

Taa hizo na bei yake moja ni Tshs. 30,000. Nipo katika matayarisho ya kufungua sehemu ya mauzo Dar es salaam kwa hiyo atakayetaka habari zaidi anitumie PM na pia soma habari zaidi hapa:
 
Picha hii hapa inaonyesha hali halisi kati ya mtumiaji wa taa ya Solar ya Wakawaka na mtumiaji wa kibatari:

Wakawaka comparison.png
 
[video=youtube_share;pGH-RJ71-Hs]http://youtu.be/pGH-RJ71-Hs[/video]
 
Tofauti ya taa hizi na taa nyingne za solar ni ninini hadi iuzwe bei hiyo? Maana taa nyingine za solar bei yake ni kati ya Tshs 15,000 - 20,000
 
Tofauti ya taa hizi na taa nyingne za solar ni ninini hadi iuzwe bei hiyo? Maana taa nyingine za solar bei yake ni kati ya Tshs 15,000 - 20,000

Tofauti ya kwanza ni ubora wake. kama ulinisoma vizuri nimeandika kwamba hii taa inawaka kwa SIKU 5 ndio inazimika. Nimeifanyia majaribia mimi mwenyewe nikalinganisha na zingine zinazowaka kwa MASAA MATATU au MANNE tu. Kuwaka kwa muda mrefu wa taa hii ni ubunifu mpya ulio na haki miliki kutoka Holland, ubunifu ambao humo kwenye taa kuna chip maalum. Mimi binafsi natumia taa hiyo.
 
Kiongozi, mimi wa mkoani nitazipataje nipo Kigoma!

Kwa sasa hivi tupo katika harakati za kufungua sehemu ya mauzo kwa Dar es salaam kwanza. Baadae tutafungua sehemu za mauzo kwenye miji mingine. Asante kwa kuuliza.
 
Kwa yule ambaye anahitaji hizi taa na anaishi Dar es salaam anitumie PM.
 
Tofauti ya kwanza ni ubora wake. kama ulinisoma vizuri nimeandika kwamba hii taa inawaka kwa SIKU 5 ndio inazimika. Nimeifanyia majaribia mimi mwenyewe nikalinganisha na zingine zinazowaka kwa MASAA MATATU au MANNE tu. Kuwaka kwa muda mrefu wa taa hii ni ubunifu mpya ulio na haki miliki kutoka Holland, ubunifu ambao humo kwenye taa kuna chip maalum. Mimi binafsi natumia taa hiyo.

Mimi nahitaji npo arusha npe maelekezo 0784815017
 
Back
Top Bottom