Swali la kizushi: Bunge limeshavunjwa?

Kiwi

JF-Expert Member
Sep 30, 2009
1,054
990
Wanajamvi heshima kwenu,

Wakati tunaendelea na kampeni za uchaguzi na wakati wengine tukiwa tunajipanga kuelekea Jangwani kesho kushuhudia ufunguzi rasmi wa kampeni za UKAWA, naomba kujuzwa kama Bunge lilishavunjwa? Hili swali niliwahi kuliuliza lakini nilimuudhi sana mwanajamvi mmoja akanitolea lugha isiyopendeza.

Kwa kumbukumbu zangu JK alipaswa kulivunja Bunge Dodoma kabla ya kikao cha kuwajadili wagombea urais kwa tiketi ya CCM. Lakini kulitokea sintofahamu na akaahidi (kama sikosei) kulivunja Bunge 20.8.2015. Tangu kipindi hicho mpaka sasa yametokea mabadiliko mengi kiasi cha mimi binafsi kushindwa kufuatilia na kuweka kumbukumbu sahihi.

Kama Bunge halijavunjwa, litavunjwa lini wakati kila mtu sasa hivi yuko kwenye kampeni? Baadhi ya wabunge wamesharudi kwenye majimbo yao kuomba ridhaa ya miaka mingine mitano, watakatiza kampeni ili warudi kwa shughuli hiyo? Je itakuwaje kwa wabunge wapya (na wa zamani watakaorudi tena) ambao watachaguliwa Oktoba 25? Wanajamvi naomba kupewa elimu kuhusu hili.
 
Hii nchi tulikuwa tunaongozwa mlad tuu mimi pia bashangaa baadhi ya mawaziri wanapanda jukwaan kuuomba ubunge sasa sijui utaratibu gan unatumika wanatumia uwaziri kuomba ubunge! Machafuko nayaona wazi waziii
 
Du! Muwe mnajitahidi kujua mambo, mbona Bunge lilishavunjwa kwa tangazo la serikali katika gazeti la serikali.
 
  • Thanks
Reactions: gsu
Du! Muwe mnajitahidi kujua mambo, mbona Bunge lilishavunjwa kwa tangazo la serikali katika gazeti la serikali.

Hivi kila mtu anaweza kuliona na kulisoma hilo gazeti la serikali? Katiba ya Nchi inaruhusu Bunge kuvunjwa kwa tamko la kwenye gazeti la serikali? Unaweza kutufahamisha malofa kama mimi hilo ni gazeti namba ngapi ili nijaribu kulitafuta? Natanguliza shukrani!
 
Wanajamvi heshima kwenu,

Wakati tunaendelea na kampeni za uchaguzi na wakati wengine tukiwa tunajipanga kuelekea Jangwani kesho kushuhudia ufunguzi rasmi wa kampeni za UKAWA, naomba kujuzwa kama Bunge lilishavunjwa? Hili swali niliwahi kuliuliza lakini nilimuudhi sana mwanajamvi mmoja akanitolea lugha isiyopendeza.

Kwa kumbukumbu zangu JK alipaswa kulivunja Bunge Dodoma kabla ya kikao cha kuwajadili wagombea urais kwa tiketi ya CCM. Lakini kulitokea sintofahamu na akaahidi (kama sikosei) kulivunja Bunge 20.8.2015. Tangu kipindi hicho mpaka sasa yametokea mabadiliko mengi kiasi cha mimi binafsi kushindwa kufuatilia na kuweka kumbukumbu sahihi.

Kama Bunge halijavunjwa, litavunjwa lini wakati kila mtu sasa hivi yuko kwenye kampeni? Baadhi ya wabunge wamesharudi kwenye majimbo yao kuomba ridhaa ya miaka mingine mitano, watakatiza kampeni ili warudi kwa shughuli hiyo? Je itakuwaje kwa wabunge wapya (na wa zamani watakaorudi tena) ambao watachaguliwa Oktoba 25? Wanajamvi naomba kupewa elimu kuhusu hili.

Eti mpaka leo hujui kama bunge lipo au limevunjwa hewa kabisa,inaonekana hujui chochote katika taifa hili.
 
Pinda anasubiri livunjwe ahamie ukawa,maana ataona aibu akihutubia mbele ya magufuli na makamba ambao wana maadili kuliko yeye,
 
Back
Top Bottom