geraldkowero1
JF-Expert Member
- Jul 5, 2014
- 1,838
- 644
kama ndo wanasheria tulionao mnaandika hivi, I'm sure tuna safari ndefu ya kufika nchi ya ahadi!!!
Nadhani hawa ni kati ya wanasheria wasioelimika wanaotegemewa na chama kikubwa kuwasaidia kuwatetea humu jf ila hahati mbaya sana kwao huwa hawana hata muda wa kusikiliza taarifa za habari za vyombo mbali mbali. Kwa wengi tuliosikiliza taarifa ya habari saa mbili usiku jana tarehe 14 tuliwaona na kuwasikiliza wananchi pale nje ya hospitali ya wilaya ya Geita na wanaoaminika kumleta pale nd.Mawazo wakisema wazi walivamiwa na kundi la green guards. Hawa green guards walijiandaa na silaha za mapanga,mashoka na nondo na kuwazidi nguvu. Kwa kutumia akili kidogo tu utaona mlengwa haswa pale alikuwa ni marehemu Mawazo. Walijitahidi kupambana huku wakiwa hawana silaha na hawakupata msaada wowote wa polisi na wala pale hospitali hatukuliona gari la polisi. Hili suala lipo kisiasa zaidi ya kulihusisha na visasi hata kama haukuwepo uhusiano mwema na Zitto siku za nyuma.Polisi wasingeweza kutumia silaha za jadi kumuua Mawazo na wala hawana mafunzo hayo. Wana uwezo wa kumweka rumande wakati wowote. Wanaweza kumfungulia makesi mengi watakavyo na hata kumshona risasi katika mazingira tata. Zitto hamiliki green guards na hata polisi hawana mamlaka na hivyo vikundi na wala katika mauaji ya Mwangosi polisi hawakutumia silaha za jadi bali risasi. Kutueleza mafanikio ya ccm Geita na kuwa marehemu hakuwa tishio kwao hayo ni kadri ya maono yako wanaojua alikuwa tishio kiasi gani ni waliokuwa nae kwenye kampeni. Kamanda Mawazo awe na visasi lakini watekelezaji wa adhabu wawe green guards sijui katika uanasheria wako ambao hufundishwa pia misindi ya awali ya uchunguzi/upelelezi hautii shaka au ni yale majigambo mliyo nayo ya kujipachika udaktari na uprofesa bila kujua mnavunja sheria? Tumempoteza Mawazo wala sitegemei haki yoyote kutendeka ila ninachoamini ni kuwa damu ya Mawazo inayolia ardhini itapata majibu kwa wabaya wake kuumbuka vibaya na usishangae hata wapangaji wa mauaji hayo kutajwa hadharani. R.I.P. KAMANDA ALPHONCE MAWAZO.