Dr Slaa, kulikuwa na kasumba iliyozoeleka huko nyuma kuwa jimbo likichukuliwa na upinzani, huwa kuna visasi vinavyofanywa na serikali ya chama tawala vya kutotekelezwa kwa mipango ya maendeleo katika jimbo hilo kwa makusudi ili kuwakomoa wananchi wale. Kwa mfano kuna tetesi kuwa mgao wa umeme Arusha mjini ni mkali kuliko sehemu zingine na watu wanahisi ni kwa sababu ya kuchagua chadema. Je chadema wamejiandaaje kupambana na tatizo hili la serikali ya chama tawala ambalo kwa kiasi kikubwa hutumiwa ili kuzoofisha upinzani?
Sisi wengine tunajua ni wajibu wa serikali kupeleka maendeleo sehemu zote za nchi pasipo upendeleo wa aina yoyote kwa kuwa wanalipa kodi, lakini inapokuja kwenye majimbo ya wapinzani huwa kuna tatizo la serikali kuwasusia wananchi wale.
Pia kwa uelewa wangu, jimbo linaloongozwa na mbunge wa upinzani linatakiwa lifanye vizuri kimaendeleo kwa sababu kutakuwa na matumizi mazuri ya fedha za maendeleo kwa kuwa kuna usimamizi mzuri.
Sisi wengine tunajua ni wajibu wa serikali kupeleka maendeleo sehemu zote za nchi pasipo upendeleo wa aina yoyote kwa kuwa wanalipa kodi, lakini inapokuja kwenye majimbo ya wapinzani huwa kuna tatizo la serikali kuwasusia wananchi wale.
Pia kwa uelewa wangu, jimbo linaloongozwa na mbunge wa upinzani linatakiwa lifanye vizuri kimaendeleo kwa sababu kutakuwa na matumizi mazuri ya fedha za maendeleo kwa kuwa kuna usimamizi mzuri.