Swali Chokonozi: Hivi ni kweli Mwanza ni Maskini kuliko hata Dodoma na Katavi?

Babu wa Kambo

JF-Expert Member
May 2, 2016
559
808
Hivi majuzi wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti Bungeni Waziri wa Fedha alitaja Mikoa mitano inayoongoza kwa Umaskini, ambayo wananchi wake ni Maskini kiasi wanashindwa hata mlo wa siku. Aliitaja Mikoa hiyo na akatoa na asilimia kuwa ni; Kigoma (48.9), Geita (43.7), Kagera (39.3), Singida (38.2), na Mwanza (35.3)

Swali langu la msingi hapa ni njia gani ya kitakwimu iliyotumika kufanya research hii mpaka kutupa majibu kama haya? Je ni kweli Mwanza ni maskini kiasi cha kuwa chini ya mstari wa Dodoma na Katavi? Utafiti huu umefanyika maeneo gani ya Mikoa hii?

Mara kwa mara tunaona taarifa zikiripotiwa wananchi wa Dodoma wanakufa njaa na wengine kujinusuru kwa kula Mizizi na udongo, au hii Dodoma tunayoisikia ni ya Sudan Kusini?! Au la takwimu hizi ni za mwaka gani?

Msaada wa ufafanuzi tafadhali, ni njia gani za kitafiti zilizotupa takwimu hizi?
(Nimechukua Dodoma na Katavi kama mfano tu)
 
Hivi majuzi wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti Bungeni Waziri wa Fedha alitaja Mikoa mitano inayoongoza kwa Umaskini, ambayo wananchi wake ni Maskini kiasi wanashindwa hata mlo wa siku. Aliitaja Mikoa hiyo na akatoa na asilimia kuwa ni; Kigoma (48.9), Geita (43.7), Kagera (39.3), Singida (38.2), na Mwanza (35.3)

Swali langu la msingi hapa ni njia gani ya kitakwimu iliyotumika kufanya research hii mpaka kutupa majibu kama haya? Je ni kweli Mwanza ni maskini kiasi cha kuwa chini ya mstari wa Dodoma na Katavi? Utafiti huu umefanyika maeneo gani ya Mikoa hii?

Mara kwa mara tunaona taarifa zikiripotiwa wananchi wa Dodoma wanakufa njaa na wengine kujinusuru kwa kula Mizizi na udongo, au hii Dodoma tuyoisikia ni ya Sudan Kusini?! Au la takwimu hizi ni za mwaka gani?

Msaada wa ufafanuzi tafadhali, ni njia gani za kitafiti zilizotupa takwimu hizi?
(Nimechukua Dodoma na Katavi kama mfano tu)
Kwanza naomba ku declare interest, mimi ni chapa ng'ombe!.

Hili ni swali la msingi sana!. Mwanza ndio mkoa unaoongoza kwa utajiri Tanzania ila pia ni mmoja ya mikoa yenye watu wengi sana Tanzania!. Wasukuma ndilo kabila kuu Tanzania linaloongoza kwa idadi ya watu, ambao wamesambaa katika mikoo 5 ya Mwanza, Shinyanga, Shimiyu, Katavi, na Geita.

Miongoni wa wakazi wa Mwanza, pia ndani yake kuna makabila masikini wa kutupwa kama Wanzinza, Wakerewe, Wakara, Wanyamtunzu, hivyo kitakwimu kutoka na wingi wa idadi ya masikini wote wa Mwanza ni wengi kuliko masikini wote wa Singida na Dodoma put together!. Tofauti ya masikini wa Mwanza ni baadhi tuu, lakini Singida na Dodoma wote ni masikini!.

Pasco
 
Kwanza naomba ku declare interest, mimi ni chapa ng'ombe!.

Hili ni swali la msingi sana!. Mwanza ndio mkoa unaoongoza kwa utajiri Tanzania ila pia ni mmoja ya mikoa yenye watu wengi sana Tanzania!. Wasukuma ndilo kabila kuu Tanzania linaloongoza kwa idadi ya watu, ambao wamesambaa katika mikoo 5 ya Mwanza, Shinyanga, Shimiyu, Katavi, na Geita.

Miongoni wa wakazi wa Mwanza, pia ndani yake kuna makabila masikini wa kutupwa kama Wanzinza, Wakerewe, Wakara, Wanyamtunzu, hivyo kitakwimu kutoka na wingi wa idadi ya masikini wote wa Mwanza ni wengi kuliko masikini wote wa Singida na Dodoma put together!. Tofauti ya masikini wa Mwanza ni baadhi tuu, lakini Singida na Dodoma wote ni masikini!.

Pasco
Kuna shaka kubwa sana juu ya utafiti wa huyu waziri wetu, binafsi naijua vizuri mikoa ya Lindi na Dodoma na Singida kwa kuisoma na kuishi pia hii mikoa ni maskini hakuna pa kulinganisha huwezi chukua mkoa wa mwanza ukalinganisha na mikoa hiyo hapo tajwa wakarudie utafiti tena..!
 
Hivi majuzi wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti Bungeni Waziri wa Fedha alitaja Mikoa mitano inayoongoza kwa Umaskini, ambayo wananchi wake ni Maskini kiasi wanashindwa hata mlo wa siku. Aliitaja Mikoa hiyo na akatoa na asilimia kuwa ni; Kigoma (48.9), Geita (43.7), Kagera (39.3), Singida (38.2), na Mwanza (35.3)

Swali langu la msingi hapa ni njia gani ya kitakwimu iliyotumika kufanya research hii mpaka kutupa majibu kama haya? Je ni kweli Mwanza ni maskini kiasi cha kuwa chini ya mstari wa Dodoma na Katavi? Utafiti huu umefanyika maeneo gani ya Mikoa hii?

Mara kwa mara tunaona taarifa zikiripotiwa wananchi wa Dodoma wanakufa njaa na wengine kujinusuru kwa kula Mizizi na udongo, au hii Dodoma tuyoisikia ni ya Sudan Kusini?! Au la takwimu hizi ni za mwaka gani?

Msaada wa ufafanuzi tafadhali, ni njia gani za kitafiti zilizotupa takwimu hizi?
(Nimechukua Dodoma na Katavi kama mfano tu)

Mbona jibu lake ni jepesi.Hujiulizi Tanzania tuna kila kitu na bado ni masikini kulinganisha na nchi zisizo na raslimali kama zetu!
 
huo utafiti umefanywa na serikali nashangaa watu wanabisha kitu gani tena
 
Kwanza naomba ku declare interest, mimi ni chapa ng'ombe!.

Hili ni swali la msingi sana!. Mwanza ndio mkoa unaoongoza kwa utajiri Tanzania ila pia ni mmoja ya mikoa yenye watu wengi sana Tanzania!. Wasukuma ndilo kabila kuu Tanzania linaloongoza kwa idadi ya watu, ambao wamesambaa katika mikoo 5 ya Mwanza, Shinyanga, Shimiyu, Katavi, na Geita.

Miongoni wa wakazi wa Mwanza, pia ndani yake kuna makabila masikini wa kutupwa kama Wanzinza, Wakerewe, Wakara, Wanyamtunzu, hivyo kitakwimu kutoka na wingi wa idadi ya masikini wote wa Mwanza ni wengi kuliko masikini wote wa Singida na Dodoma put together!. Tofauti ya masikini wa Mwanza ni baadhi tuu, lakini Singida na Dodoma wote ni masikini!.

Pasco
STATISTICS huwa haina utaratibu huo, eti kwa sababu shule "A" yenye Wanafunzi 450 wamefeli 50 na shule "B" yenye Wanafunzi 45 wamefeli 40 basi shule "A" ndo imefelisha zaidi sababu idadi inaonekana ni kubwa kuliko B, yaani 50 kwa 40. Hii hesabu haipo duniani.
 
Hivi majuzi wakati akiwasilisha Hotuba ya Bajeti Bungeni Waziri wa Fedha alitaja Mikoa mitano inayoongoza kwa Umaskini, ambayo wananchi wake ni Maskini kiasi wanashindwa hata mlo wa siku. Aliitaja Mikoa hiyo na akatoa na asilimia kuwa ni; Kigoma (48.9), Geita (43.7), Kagera (39.3), Singida (38.2), na Mwanza (35.3)

Swali langu la msingi hapa ni njia gani ya kitakwimu iliyotumika kufanya research hii mpaka kutupa majibu kama haya? Je ni kweli Mwanza ni maskini kiasi cha kuwa chini ya mstari wa Dodoma na Katavi? Utafiti huu umefanyika maeneo gani ya Mikoa hii?

Mara kwa mara tunaona taarifa zikiripotiwa wananchi wa Dodoma wanakufa njaa na wengine kujinusuru kwa kula Mizizi na udongo, au hii Dodoma tuyoisikia ni ya Sudan Kusini?! Au la takwimu hizi ni za mwaka gani?

Msaada wa ufafanuzi tafadhali, ni njia gani za kitafiti zilizotupa takwimu hizi?
(Nimechukua Dodoma na Katavi kama mfano tu)
Na mimi hilo swali nimejiuliza.
Yaani hata Lindi imechanja mbele kuliko Mwanza?
 
Kwanza naomba ku declare interest, mimi ni chapa ng'ombe!.

Hili ni swali la msingi sana!. Mwanza ndio mkoa unaoongoza kwa utajiri Tanzania ila pia ni mmoja ya mikoa yenye watu wengi sana Tanzania!. Wasukuma ndilo kabila kuu Tanzania linaloongoza kwa idadi ya watu, ambao wamesambaa katika mikoo 5 ya Mwanza, Shinyanga, Shimiyu, Katavi, na Geita.

Miongoni wa wakazi wa Mwanza, pia ndani yake kuna makabila masikini wa kutupwa kama Wanzinza, Wakerewe, Wakara, Wanyamtunzu, hivyo kitakwimu kutoka na wingi wa idadi ya masikini wote wa Mwanza ni wengi kuliko masikini wote wa Singida na Dodoma put together!. Tofauti ya masikini wa Mwanza ni baadhi tuu, lakini Singida na Dodoma wote ni masikini!.

Pasco
Pasco punguza uongo katika hili. Bahati nzuri ni kwamba naijua Mwanza ndani na nje. Nakukatalia kabisa unaposema Wakerewe, Wanzinza, Wakara na Wanyantuzu ni masikini kwa kiwango unachotaka watu waamini.
Ukitaka kuwapata Wasukuma matajiri basi wengi wao utawapata kwenye jamii ya Wanyantuzu. Karibu jamii yote ya Wakerewe na Wakara ni wavuvi. Kipato cha wavuvi kinazidi kwa mbali kipato cha wakazi wengi wa Dar ambao maisha yao kiuhalisia ni ya shida ingawa wapo mjini.
Tatizo hapa ni vigezo vinavyotumika kupata takwimu za Umasikini.
Ukweli ni kwamba wale wanaoonekana masikini wana mali nyingi tu. Chukulia mfano wa Tanzania kuwa kwenye kundi la nchi masikini, je kuna uhalisia? Leo hii TRA ikiamua kukusanya kodi kutoka kwa wafugaji wa kisukuma pekee utashangaa kuona mabilioni ya shilingi yanayoweza kupatikana toka kwa hao wanaoitwa masikini. Nina shaka kubwa na mfumo uliotumika kupata takwimu hizi.
 
Hizo takwimu inawezekana in za kweli. Mchangiaji aliyede
Clarke interest kwamba ni msukuma aache dharau za kisukuma kwa kuyadharau makabila ya wenziye wazinza na wakerewe. Kama wasukuma ndo wengi hao minority wataathiri vipi hilo la mkoa kiasi kikubwa? Hayo makabila yapo sehemu ndogo tu ya Sengerema na Ukerewe na wala siyo maskini kiasi cha kuzidiwa na wasukuma. Hebu jenga hoja zenye mashiko acha majigambo ya kisukuma
 
Kuna shaka kubwa sana juu ya utafiti wa huyu waziri wetu, binafsi naijua vizuri mikoa ya Lindi na Dodoma na Singida kwa kuisoma na kuishi pia hii mikoa ni maskini hakuna pa kulinganisha huwezi chukua mkoa wa mwanza ukalinganisha na mikoa hiyo hapo tajwa wakarudie utafiti tena..!
Kuna msemo usemao, numbers don't lie!.

Mfano kwenye matokeo ya kidato cha nne, siku zote shule za seminari ndizo zinazoongoza. Utakuta darasa lina wanafunzi 10 na wote wakapata DIV 1, hiyo shule inakuwa imepasisha asilimia 100% kwa 100%. Shule nyingine yenye wanafunzi 100, wanafunzi 70 wakapata Div 1, na wanafunzi 30 wakafeli, matokeo ya shule hiyo kwa asilimia itakuwa ni 70% kwa 100!.

Angalia Mwanza
upload_2016-6-10_11-0-21.png

upload_2016-6-10_10-52-10.png


Linganisha na Dodoma
upload_2016-6-10_10-58-45.png

upload_2016-6-10_10-53-50.png
 
Hizo takwimu inawezekana in za kweli. Mchangiaji aliyede
Clarke interest kwamba ni msukuma aache dharau za kisukuma kwa kuyadharau makabila ya wenziye wazinza na wakerewe. Kama wasukuma ndo wengi hao minority wataathiri vipi hilo la mkoa kiasi kikubwa? Hayo makabila yapo sehemu ndogo tu ya Sengerema na Ukerewe na wala siyo maskini kiasi cha kuzidiwa na wasukuma. Hebu jenga hoja zenye mashiko acha majigambo ya kisukuma
Wazinza na wakerewe wanamalizana kwa uchawi, vinginevyo wangekuwa wameendelea..
..mkerewe akisoma harudi kwao,anaogopa chatu,bazinza twimanye
 
Kuna shaka kubwa sana juu ya utafiti wa huyu waziri wetu, binafsi naijua vizuri mikoa ya Lindi na Dodoma na Singida kwa kuisoma na kuishi pia hii mikoa ni maskini hakuna pa kulinganisha huwezi chukua mkoa wa mwanza ukalinganisha na mikoa hiyo hapo tajwa wakarudie utafiti tena..!
Idadi kubwa ya Watanzania ipo Vijijini ambako shughuli yao kubwa ni kilimo! Hivi huko Mwanza ambako nako mamilioni wanaishi Vijijini wanalima nini hasa?!

Tuchukulie Lindi ulikotolea mfano: wanalima ufuta, wanalima korosho na ukanda wa pwani wanalima nazi! Barabara c kikwazo tena na pesa ya hivi vitu moja kwa moja inaingia mfukoni mwa mwananchi!

Siku hizi mtu anatoka Dar es salaam saa 12 asubuhi na saa 7 mchana yupo Lindi na hivyo kurahisisha biashara! Household size ya Mwanza ni karibu mara 2 ya household size ya Lindi! Kwavile Lindi na Mtwara walipewa upendeleo maalumu wa gharama za kuunga umeme; unakuta vijiji vingi vina umeme!

Sasa nyie endeleeni tu kukariri kwa Kusini maskini huku mkibishana na takwimu! Mtoto wa sister angalau baada ya kumaliza chuo kikuu tu alirudi Bush lakini mzunguko wa biz wa pale kijijini tu unamwezesha kuuza mayai ya kuku wa kisasa trey 6 @8,000 kwa cku kitu ambacho kwa zamani isingewezekana hata trey moja!
 
Back
Top Bottom