Supu ya boga karibuni

Miss Natafuta

JF-Expert Member
Sep 16, 2015
25,557
45,827
Maza katoka kijijini kaja kunitembelea kaja na maboga ya kutosha namuonea huruma sijui alibebaje anyway am her little daughter hata kama nimezeeka vipi so hapa nimeona nipike soup ya boga.

Kula maboga sio umaskini boga ni chakula kizuri sana kwa wagonjwa ,watoto pia mahoteli makubwa wanatumia kama appetizer so nawashauri hasa watu wa dar nyie ambao chakula chenu ni mzunguko wa wali, ugali, tambi, pilau mjitahidi kuongeza na vyakula kama maboga kwenye meza zenu.

Mapishi ya soup ya boga mahitaji vipande vya boga vilivochemshwa inategemea na mpo wangapi tuseme kama nataka bakuli nne nitachukua nusu boga maziwa robo lita ukipata ile cream ya juu ya maziwa ni safi sana butter kijiko kimoja
vitunguu vile vya majani kama vinne hivi chumvi, pilipili manga.

Mapishi;

Chukua boga blend au pondaponda hadi lisagike kabisa unasweza ukasaga na tui na nazi au maji tu ukipenda weka sufuria jikoni weka mafuta kidogo sana na butter kijiko kimoja weka vitunguu vya majani baada ya kukatakata vidogodogo au hata vitunguu maji ukipenda ila vya majani ndo vizuri zaidi according to me, acha kitunguu kiive kidogo kisiungue kabisa.

Mwaga lile boga uliloliblend kwenye huo mchanganyiko wa vitunguu
koroga kwa nguvu weka chumvi, weka pilipili manga, koroga sana weka maziwa koroga sana ili yasikatike baada ya hapo acha kidogo ila koroga tu kwa muda
hapo supu yako itakuwa tayari.

Karibuni hapa nakunywa supu ya boga

2433016.jpg


Kesho nitawapikia vegetable soup
 
Iko vizuri...natamani kuionja, mchanganyiko wa maziwa na nazi ndani yake bila Shaka, kuna maajabu mno! Nimeipenda hiyo supu, sijui niite uji ila bila Shaka ni tamu mnooooo
 
Iko vizuri...natamani kuionja, mchanganyiko wa maziwa na nazi ndani yake bila Shaka, kuna maajabu mno! Nimeipenda hiyo supu, sijui niite uji ila bila Shaka ni tamu mnooooo
tamu sana mkuu karibu sana
 
Miss Natafuta,

Ungeongeza na faida cha chakula hicho ingesaidia sana hasa kwa makundi mbali mbali wazee, watoto me au ke
nishaongeza mkuu
Kwa muda mrefu maboga yamekuwa yanajulikana kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kutumika kama dawa, vilevile chakula hicho kina protini yenye nguvu ambayo inaweza kupambana na magonjwa mbalimbali yanayotokana na kuvu au fungus.
Maboga yamekuwa yakitumika sana katika tiba za kiasili katika kutibu magonjwa tofauti kama vile kisukari, shinikizo la damu, kiasi kikubwa cha mafuta mwilini pamoja na saratani katika nchi kama vile China, Korea, India, Yugoslavia, Argentina, Mexico, Barazil na kwingineko.
Kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa kwenye jarida la Kilimo na Kemia ya Vyakula, imeonyeshwa kuwa protini inayotokana na boga iitwayo Pr-2, inapambana vilivyo na ugonjwa unaosababishwa kuvu au fungus wa sehemu za uke (Vaginal yeast infection). Vilevile michubuko inavyotokana na mkojo au nepi (diaper rashes) pamoja na matatizo mengine ya kiafya. Protini hiyo ya Pr-2 iliyoko kwenye maboga halikadhalika inazuia aina 10 za fungus au kuvu ikiwemo aina hatari ya fungus wajulikanao kama Candida Albicans. Fungus hao ni maarufu kwa kusababisha matatizo kwa watu wenye ugonjwa wa kisukari na kupelekea kupata fungus midomoni, katika ngozi, chini ya kucha pamoja na katika mfumo mzima wa mwili.
Waaalamu wana matumaini kuwa, protini hiyo inayopatikana kwenye maboga inaweza kupelekea mafanikio ya kutengezezwa tiba asilia ya kupambana na magonjwa ya kuvu au fungus.
… Haya shime kama ulikuwa unadharau kula maboga, nafikiri inakubidi ufikirie tena!
 
Kuna thread fulani iliuliza chakula gani hatupendi alafu mimi nikajibu pale vyakula vyote nakula . .
Nilisahau sipendi maboga jamani,nilishaonja yana ladha fulani hivi inaboaaa
 
Kuna thread fulani iliuliza chakula gani hatupendi alafu mimi nikajibu pale vyakula vyote nakula . .
Nilisahau sipendi maboga jamani,nilishaonja yana ladha fulani hivi inaboaaa
Pole sana, nilienda Rufiji halafu nikapigika, basi asubuhi ni chai na mapande ya maboga, mchana na usiku ni wali na maboga
Nalog off
 
Napenda sana boga, ila la kuchemsha tu...
Ila sasa huwa stimu zinakata likiwa na maji maji, nashindwa kujua nakosea kulichemsha naweka maji mengi au sijui kuchagua boga zuri lenye Unga?
 
We Miss Natafuta umeolewa?

Boga ni zuri sana. Basi tu wengi hawajui kuliandaa liondokane na ile ladha yake bland. Hiyo supu uliyoandaa safi sana hata kwa waliofunga kufungulia nayo.

Faida ingine ya boga ni kusaidia ubongo kuchakata taarifa na kuvuta kumbukumbu za harakaharaka. Sio unaulizwa jina la mwalimu wako mkuu msingi unasema hadi baadae.
 
We Miss Natafuta umeolewa?

Boga ni zuri sana. Basi tu wengi hawajui kuliandaa liondokane na ile ladha yake bland. Hiyo supu uliyoandaa safi sana hata kwa waliofunga kufungulia nayo.

Faida ingine ya boga ni kusaidia ubongo kuchakata taarifa na kuvuta kumbukumbu za harakaharaka. Sio unaulizwa jina la mwalimu wako mkuu msingi unasema hadi baadae.
mambo ya kuolewa yanatoka wapi tena mkuu? kwani kupika lazima uwe umeolewa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom