mambo yatanyooka chadema ikishika dora 2015,
Best hawa jamaa wamelala siku nyingi full usingizi
basi hilo shirika lifungwe tu...
tatizo watoto watasoma shule gani? si unajua jinsi hizi Mamlaka aka AUTHORITIES zinavyojua jukulipa vzr, watoto watahama FEDHA kwenda Kayumba................. zoezi gumu hilo
Watu wamekua hawaangali ubora bali wanadhamini fedha na kutaharisha afya za watu. TFDA na wauzaji wa vyakula hivi wanatakiwa kuwa makini na bidhaa wanazoziuza na kutoweka stock kwa wingi na pia waangalie muda wa vyakula hivi maana ni hatari.Watu wengi wanaamini kuwa katika Supermarkets kunauzwa vyakula vyenye ubora. Hata hivyo wanakosea sana.
Katika baadhi ya maduka hayo makubwa kuna vyakula vibovu na vingine vinahatarisha maisha ya walaji.
Majuzi mimi mwenyewe nilinunua unga unaoitwa Bora wa Lishe katika supermarket moja iliyoko Vertenary katika kituo cha Mafuta cha Oilcom na nilipofika nyumbani niligundua kuwa unga huo una wadudu weusi.
Niliwapa unga huo unaozalishwa na kampuni ya Fortune Foods Products ili wachukue hatua. Niliambiwa kuwa kampuni hiyo haina kibali kwavile ilikosa sifa. Lakini imeruhusiwa kinyemela iuze bidhaa zake. Swali hapa ni kwamba hivi tuna sheria inayoruhusu mtu asiye na vibali vya TFDA au TBS kuuza bidhaa zake kwenye Supermarkets?
Kama jibu ni hapana, hao wanaoitwa wakaguzi wa idara hizo mbili za kulinda maisha ya mlaji, wanafanyia ukaguzi wao wapi?
we nawe kila kitu ni chadema, hata ukiachwa na mkeo /mmeo utasubiri chadema ishike dola ndo ikurudishie....
..afu DORA si ni jina la msichana au ulitaka kumaanisha DORA ipi au yupi ambaye atashikwa na chadema??
Kumbe Supermarket yenyewe iko Temeke. Kama ni Temeke basi hiyo sio supermarket bali ni genge maana Temeke hakuwezi kuwa na Supermarket.
[Majuzi mimi mwenyewe nilinunua unga unaoitwa Bora wa Lishe katika supermarket moja iliyoko Vertenary katika kituo cha Mafuta cha Oilcom]