mabereng'ombe
Member
- Nov 22, 2013
- 70
- 18
Watu wengi wanaamini kuwa katika Supermarkets kunauzwa vyakula vyenye ubora. Hata hivyo wanakosea sana.
Katika baadhi ya maduka hayo makubwa kuna vyakula vibovu na vingine vinahatarisha maisha ya walaji.
Majuzi mimi mwenyewe nilinunua unga unaoitwa Bora wa Lishe katika supermarket moja iliyoko Vertenary katika kituo cha Mafuta cha Oilcom na nilipofika nyumbani niligundua kuwa unga huo una wadudu weusi.
Niliwapa unga huo unaozalishwa na kampuni ya Fortune Foods Products ili wachukue hatua. Niliambiwa kuwa kampuni hiyo haina kibali kwavile ilikosa sifa. Lakini imeruhusiwa kinyemela iuze bidhaa zake. Swali hapa ni kwamba hivi tuna sheria inayoruhusu mtu asiye na vibali vya TFDA au TBS kuuza bidhaa zake kwenye Supermarkets?
Kama jibu ni hapana, hao wanaoitwa wakaguzi wa idara hizo mbili za kulinda maisha ya mlaji, wanafanyia ukaguzi wao wapi?
Katika baadhi ya maduka hayo makubwa kuna vyakula vibovu na vingine vinahatarisha maisha ya walaji.
Majuzi mimi mwenyewe nilinunua unga unaoitwa Bora wa Lishe katika supermarket moja iliyoko Vertenary katika kituo cha Mafuta cha Oilcom na nilipofika nyumbani niligundua kuwa unga huo una wadudu weusi.
Niliwapa unga huo unaozalishwa na kampuni ya Fortune Foods Products ili wachukue hatua. Niliambiwa kuwa kampuni hiyo haina kibali kwavile ilikosa sifa. Lakini imeruhusiwa kinyemela iuze bidhaa zake. Swali hapa ni kwamba hivi tuna sheria inayoruhusu mtu asiye na vibali vya TFDA au TBS kuuza bidhaa zake kwenye Supermarkets?
Kama jibu ni hapana, hao wanaoitwa wakaguzi wa idara hizo mbili za kulinda maisha ya mlaji, wanafanyia ukaguzi wao wapi?