Sumry imeua nane papo hapo

Sumry imeua nane papo hapo

1.jpg


Basi la kampuni ya Sumry limetumbukia mtoni na kuua watu tisa na kujeruhi wengine hamsini na tatu.


Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Sitalike wilaya ya Mlele mkoani Katavi



Tukio hilo la kusikitisha lilitokea saa sita usiku kuamkia Julai 5, 2013 basi hilo lilipokuwa likitokea mjini Sumbawanga kuelekea Mpanda mkoani Katavi likiwa na abiri waliokuwa wametoka Mbeya.
2.jpg

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Katavi Emanuely Nnley alisema jana kuwa ajali hiyo ilihusisha basi aina ya Nissan Diesel lenye namba T909 AZT mali ya kampuni ya Sumry lililokuwa likiendeshwa na dereva aliyetajwa kwa jina na Stephano Chimane maarufu kwa jina la Ntungu



Alisema basi hilo lilipofika katika daraja hilo lenye kona kali na mteremko, dereva wake alishindwa kulimudu na kulenga daraja hali iliyosababisha tairi za nyuma kupanda juu ya ukingo na kutumbukia mtoni ambapo dereva wa basi hilo aliweza kutoka na kukimbilia kusikojulikana ...


Mkuu wa mkoa wa Katavi Dr Rajabu Rutengwe alitoa rambi rambi kwa wafiwa wote na kuwapa pole wahanga wa ajali hiyo mbaya kutokea tangu mkoa huo uanze.


BASI LA SUMMRY LAUA WATU 9 NA KUJERUHI 53 - GUMZO LA JIJI
 
acha kutetea upuuzi mkuu,hivi saa 8 ya usiku mnaenda wapi na basi?kwanini msipaki hata kabla ya saa 5 kama mnaona hampo ktk mazingra ya kuimaliza mbuga mapema?UKIAMUMUA KU-TAKE RISK,KUBALIANA NA MATOKEO YAKE YANAYOWEZA KUJITOKEZA,(kwamfano,ukitembea na mwanafunzi,kubaliana na kifungo cha 30yrs ukikamatwa)HAKUNA KUMSINGIZIA MUNGU KWA LOLOTE HAPO

Nimetetea upuuzi gani!!!!!!
mama yangu mdogo kafariki katika hiyo ajali halafu unaniambia natetea upuuzi!!!!!!
wametoka Mbeya wanaelekea mpanda moja kwa moja!!!!!!!!
siku ya jana tumetoka kumpumzisha katika nyumba ya milele

Machungu ambayo ajali hii imenisababishia
ni kubwa sana na kidonda ni kibichi!!!!!!
kwahiyo tuheshimiane sana
 
Nimetetea upuuzi gani!!!!!!
mama yangu mdogo kafariki katika hiyo ajali halafu unaniambia natetea upuuzi!!!!!!
wametoka Mbeya wanaelekea mpanda moja kwa moja!!!!!!!!
siku ya jana tumetoka kumpumzisha katika nyumba ya milele

Machungu ambayo ajali hii imenisababishia
ni kubwa sana na kidonda ni kibichi!!!!!!
kwahiyo tuheshimiane sana

Pole sana mkuu.
Hata hivyo bado haihalalishi uzembe wao wa kutembea muda ambao hauruhusiwi kisheria.KUTEMBEA USIKU NI RISK SANA,SIO KWA GARI TU,HATA KWA MIGUU.HIVI INGETOKEA MAJAMBAZI WAMEWATEKA THEN WAKAUA WATU KUMI SI MNGEWASEMA SANA KWA UJINGA WAO WA KUTEMBEA USIKU.?ACHA KUTETEA UPUUZI.
 
Pole sana mkuu.
Hata hivyo bado haihalalishi uzembe wao wa kutembea muda ambao hauruhusiwi kisheria.KUTEMBEA USIKU NI RISK SANA,SIO KWA GARI TU,HATA KWA MIGUU.HIVI INGETOKEA MAJAMBAZI WAMEWATEKA THEN WAKAUA WATU KUMI SI MNGEWASEMA SANA KWA UJINGA WAO WA KUTEMBEA USIKU.?ACHA KUTETEA UPUUZI.

kuwa na staha kwa kujua muda na aina ya maneno ambayo unatakiwa kumwambia mlengwa ukizingatia yupo kwenye matatizo,
ficha UPUUZI wako
 
Ubaya wa madereva ndo huu,baada ya ajari WANAKIMBIA,wakati akiwa anaendesha abiria wakisema dereva punguza spidi,anakua mbishi na kudai usimfundishe kuendesha
""VV"l
 
kuwa na staha kwa kujua
muda na aina ya maneno ambayo unatakiwa kumwambia mlengwa ukizingatia
yupo kwenye matatizo,
ficha UPUUZI wako

inamaana unataka hadi msiba uishe ndio tuseme kuwa wamekufa kwa uzembe?HAYA BASI WAMEKUFA KISHUJAA.
 
Back
Top Bottom