Sumaye amgwaya Lowassa!

n00b

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2008
Posts
1,013
Reaction score
2,684
Wakuu,

Nipo kwenye ukumbi tayari na nitawajuza kila kinachoendelea ikiwa ni pamoja na picha. Mods mtanisadia kuziweka sawa kwakuwa nitakuwa naandika kadiri matukio yanavyojiri.

Ni hapa Courtyard Hotel - Dar



 

Attachments

  • sumaye-leo.jpg
    35.9 KB · Views: 6,041
  • sumaye-leo1.jpg
    45.3 KB · Views: 7,948
Muda wowote kuanzia sasa ataanza kuongea, kishawasili
 
Tuko pamoja mkuu, tupe anasemaje mheshiwa. Nategemea atoe maamuzi mazito kwamba anajitoa CCM ila hasije CDM
 
Ameanzia kanisani Azania Front, ndio maana kachelewa kuanza.
 
Sumaye:

Sijawahi kukutana na Chadema wala yeyote wa upinzani.... Lakini upinzani si uadui, ni Watznania... Kama ningekutana nao, ningesema tu kwamba mbona na wengine wanakutana nao na wanagombea Urais...

Kuna uvumi mzito kuwa kama nitaingia Chadema nitashughulikiwa.

Dawa si kushughulikia wanaokihama chama bali sababu ya wanachokihama... Kukosa NEC hakuninyimi usingizi wala hakunizuii kugombea Urais kama nitataka...

Mwalimu alisema Chama si mama yake
 
Sumaye: Tusiandame watu bali tuandame maovu
 
Sumaye:
Mambo ya Hanang, yalitokea nchi nzima... Na yalitokea kwa staili tofauti

Tatizo ni kubwa sana, maana nchi nzima mattumizi makubwa ya fedha... Tatizo ni kubwa na limeota mizizi

Nimewahi kuzungumzia mara kadhaa...

Nilisema nikiwa Same "Rushwa ni tatizo Barani na Tanzania pia... Kwetu sisi huwezi kushinda bila kutoa fedha"

Nilisema haya 2010:

"Kiongozi anayetoa rushwa anapata wapi kama si mwizi na mla rushwa... Hawezi kuwatendea haki maana wananchi ni kama bidhaa na hatawatumikia bali atatfuta za kihonga baadae"
 

Aseme ni nani anatoa Rushwa. Kama ni mkweli ataje watu kwa majina na si kusema kuna watu bila kutaja majina. Kama anajeuri. CCM wote wameoza
 
Sumaye:

Baadhi ya taarifa katika magazeti na taarifa za habari.... Kuna gazeti limeandika "Sumaye kupasua jipu Dar es Salaam...." Sina jipu wala jipu wala bomu la kupasua.

Kuna lililonishangaza kwamba 'Sumaye amtangazia jipu Lowassa, ikiwa ataingia Lowassa basi atamkabili kwa namna yoyote....'

Hakuna aliyezungumza na mimi kwamba nitapambana na Lowassa, siamini kama kuna source ya karibu na mimi. Basi sikifahamu na kama chanzo kipo sikifahamu, sijaongea na mtu na wala nisingeweza kuyasema, sina uhasama na Lowassa, na niliamua kugombea sitogombea kwa sababu ya mtu, bali kwa sababu ya maslahi ya nchi na si ya mtu.
 
Sumaye: Tusiandame watu bali tuandame maovu

ma body guard wake wa TISS wapo naye hapo mkutanoni? maana ukiwa PM mstaafu si unalindwa kila kona na hao UWT, nahisi haohao ndio wanam-feed habari JK na EL kama vipi angekataa ulinzi!
 
Hadi hapo naona hamna jipya kabla hata hajamaliza,. Hawa ccm wanatuchezea akili
 
Sumaye:
Nilisema kiongozi anatumia rushwa hatajali umma bali atatafuta fedha kunnua tena... CCM lazima tupige vita rushwa... Nilisema haya Julai 7 mwaka jana...

Nasema haya isionekane nasema haya baada ya kushindwa Hanang
 
Katika uchaguzi wa demokrasia, mtu huchaguliwa kwa uwezo na kwa ajili yao kuwatumikia, katika demokrasia ya rushwa, fedha huwachagulia watu mwakilishi kwa ajili ya waliotoa fedha, kama nimetoa fedha kwa ajili yako, na wapiga kura wanakua wapiga mihuri.

Sasa imetoka mtu kuhonga achaguliwe, na sasa mtu anatoa rushwa kununua watu ili apate kujenga mtandao wake na sasa ni rushwa ya kimtandao ambayo ni hatari sana...
 
Nimeshastuka hakuna jipya hapa. Yale yale ya EL kusema sikukutana na JK barabarani. Aseme ameita mkutano kusema nini hasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…