Sumatra yaipiga ban Champion Bus

Sumatra yaipiga ban Champion Bus

Rugaijamu

JF-Expert Member
Joined
Jul 10, 2010
Posts
2,942
Reaction score
1,300
Hii ni kufuatia ajali ya basi la kampuni hiyo mkoani Dodoma.Zuio hilo linaanza kesho,litadumu kwa muda usiojulikana kupisha uchunguzi-sumatra.SOURCE TBC TAIFA-habari.
 
Hood mbona hawafungwi? !#*
 
Hood mbona hawafungwi? !#*

wanazi hawa, au nishinikizo kwa kuwa mkuu alikuwa huko?
ndio maana serikali inajidhalilisha kila siku, uwezi kufundia kampuni nzima kwa ajari iliyosabanishwa na bus moja,
kwani hayo mabusi ni auto pilot kusema kuna failure kwenye system?
hii hadhabu ni kali sana, wangedili na dereva na bosi wake sio mabasi yote na sisi wasafiri wanatuweka kundi gani
 
Pumbafu zao Sumatra na traffic police wote! Leo basi la Mohamed(sina uhakika kama ni Classic au Trans) limeua watu wanne likitokea Arusha na lenyewe walifungie au? Sasa hv nipo kwenye basi la Mghamba kuelekea kahama kasi yaje inatisha! Dereva wala hajari bamps mbaya zaidi nipo siti ya mwisho kabisa! Jamaa hajaigopi hata Sekenke mwendo ulelue! maaskari wakitusimamisha wanaongea na konda hata ndani hawaingii mambo yanakwisha! Ipo hvi zaidh ya asilimia 78 ya ajari za mabasi ni uzembe wa madereva.Sasa unafungia kampuni moja nyingine inaua utafungia ngapi? Lazima washughulike na madereva.
 
we ndofu ..huna namba za polisi ukaripoti juu ya huo mwendo kasi?

ila nchii hii hakuna haki kabisa...........kila siku sumr inaua lakini mbona hawajaadhibiwa
 
Pumbafu zao Sumatra na traffic police wote! Leo basi la Mohamed(sina uhakika kama ni Classic au Trans) limeua watu wanne likitokea Arusha na lenyewe walifungie au? Sasa hv nipo kwenye basi la Mghamba kuelekea kahama kasi yaje inatisha! Dereva wala hajari bamps mbaya zaidi nipo siti ya mwisho kabisa! Jamaa hajaigopi hata Sekenke mwendo ulelue! maaskari wakitusimamisha wanaongea na konda hata ndani hawaingii mambo yanakwisha! Ipo hvi zaidh ya asilimia 78 ya ajari za mabasi ni uzembe wa madereva.Sasa unafungia kampuni moja nyingine inaua utafungia ngapi? Lazima washughulike na madereva.


mkuu hiyo kauli yako ifute ama sivyo na wewe ni dhaifu na legelege, kwani huyo dereva mnamuogopa hapo ndani ya basi?
yaani hata misaada tunayoweza kujipatia wenyewe tunataka MWANASHERIA MKUU atusemee
na huyo polisi traffic anakula rushwa mbele yenu mnaangalia maana yake ni nini? mna matatizo gani kichwa mpaka mnadharauliwa hivyo?
mbona wenzenu madereva tunawakomalia na wanatuliza hiyo mizuka yao

WATANZANIA TUBADILIKE MENTALITY ZETU NA SERIKALI inafuata tu maana hawata kuwa na pakushika kwa kiasi kikubwa mambo mengi yanakwenda mlama huku tukiangalia
 
Hivi na sie tunaishi duniani ama ndo tuko angani kisiwa kinachoelea hewani?

Hii sheria imeanza leo ama iliwekwa kusubiri Champion ikipata ajari?hata kwa vigezo vya idadi za ajari kwa kampuni,ni mara ngapi tumesikia Championi ikipata ajari ukilinganisha na makampuni mengine?...rekodi nyingine kwenye Uongozi mchovu uliowekwa chini ya matapeli na vibaka wanaojiita system (dola)
 
Pumbafu zao Sumatra na traffic police wote! Leo basi la Mohamed(sina uhakika kama ni Classic au Trans) limeua watu wanne likitokea Arusha na lenyewe walifungie au? Sasa hv nipo kwenye basi la Mghamba kuelekea kahama kasi yaje inatisha! Dereva wala hajari bamps mbaya zaidi nipo siti ya mwisho kabisa! Jamaa hajaigopi hata Sekenke mwendo ulelue! maaskari wakitusimamisha wanaongea na konda hata ndani hawaingii mambo yanakwisha! Ipo hvi zaidh ya asilimia 78 ya ajari za mabasi ni uzembe wa madereva.Sasa unafungia kampuni moja nyingine inaua utafungia ngapi? Lazima washughulike na madereva.

Mohamed Trans walishawahi kufungiwa MIEZI 3 njia ya Dar arusha,Lakini cha kushangaza haikupita hata mwezi tukasikia Ajali nyingine huko huko,sasa sijuhi waliwafungulia kimyakimya!
 
Mmiliki atasajili kampuni mpya kwa mabasi yaleyale na kuyaweka barabarani yakiwa ktk rangi na jina jipya. Si ajabu tayari yapo gereji yanavuliwa gamba mabasi yote. Tena kwa maelekezo ya vyombo vya dola. Wanajuana hao!
 
we ndofu ..huna namba za polisi ukaripoti juu ya huo mwendo kasi?

ila nchii hii hakuna haki kabisa...........kila siku sumr inaua lakini mbona hawajaadhibiwa

Ndugu yangu' nchi hii unamtegemea police? Ipo hv bado polisi wanatusimamisha na wanamalizana na Konda chini.Tumesimamishwa zaidi ya mara tatu!
 
mkuu hiyo kauli yako ifute ama sivyo na wewe ni dhaifu na legelege, kwani huyo dereva mnamuogopa hapo ndani ya basi?
yaani hata misaada tunayoweza kujipatia wenyewe tunataka MWANASHERIA MKUU atusemee
na huyo polisi traffic anakula rushwa mbele yenu mnaangalia maana yake ni nini? mna matatizo gani kichwa mpaka mnadharauliwa hivyo?
mbona wenzenu madereva tunawakomalia na wanatuliza hiyo mizuka yao

WATANZANIA TUBADILIKE MENTALITY ZETU NA SERIKALI inafuata tu maana hawata kuwa na pakushika kwa kiasi kikubwa mambo mengi yanakwenda mlama huku tukiangalia

Mkuu nimejaribu kufuata ushauri wako kesi imekuwa ya kwangu! Watu wamenigeukia wananiuliza "unataka tufike Kahama kesho?" upande wangu nipo mimi na jamaa wengine watatu tu! Hakika kazi ipo hapa Tanzania! Roho inaniuma sana mkuu, hawa ndo watanzania wa leo miaka 50 baada ya uhuru!
 
Ni kosa kubwa la kitaaluma kuifungua kampuni ya basi ambayo mabasi yake yanapata ajali. Mabasi hayajiendeshi yenyewe. Kuna mtu anayaendesha wakati yanapata ajali. Mtu huyu ni Dereva. Kwa hiyo, SUMATRA inapaswa iwafungie leseni madereva wote wanaosababisha ajali na si kampuni ya mabasi. Kama kampuni moja imeonekana ina rekodi nyingi za kupata ajali basi inachoweza kufanya ni kusitisha au kuzifungua leseni za madereva wake wote kwa sababu tukiendelea na huu utaratibu, SUMATRA itajikuta inafungua kampani zote za mabasi coz katika biashara ya aina hii ni vigumu madereva wa wakaendesha magari zaid ya 30 ya kampuni moja tena mwaka mzima bila kupata ajali au kusababisha ajali.

Labda tu ikionekana kuna matatizo kwa upande wa gari la kampuni. Mfano linaendeshwa na matairi vipara, long run services na magari yaliyochoka. Hapa SUMATRA inachoweza kufanya ni kulifutia vibali gari husika.
 
We unashangaa ya kutofungiwa hood!Vipi SUMRY zilizokuwa zinafululiza kutuchinja?

mi mwenyewe nilikuwa nataka niulize kuhusu Sumry....kila mwezi lazima tusikie ajali ya hili bus.....mbona halifungiwi?....
 
mkuu hiyo kauli yako ifute ama sivyo na wewe ni dhaifu na legelege, kwani huyo dereva mnamuogopa hapo ndani ya basi?<br />
yaani hata misaada tunayoweza kujipatia wenyewe tunataka MWANASHERIA MKUU atusemee<br />
na huyo polisi traffic anakula rushwa mbele yenu mnaangalia maana yake ni nini? mna matatizo gani kichwa mpaka mnadharauliwa hivyo?<br />
mbona wenzenu madereva tunawakomalia na wanatuliza hiyo mizuka yao<br />
<br />
WATANZANIA TUBADILIKE MENTALITY ZETU NA SERIKALI inafuata tu maana hawata kuwa na pakushika kwa kiasi kikubwa mambo mengi yanakwenda mlama huku tukiangalia
<br />
<br />
Nakubaliana na wewe kwa hilo. Watanzania tumekuwa watu kulalamika tu bila kuchukua hatua. Ni yaleyale ya kuichagua CCM baadaye kulalamika kama kawa.
 
mi mwenyewe nilikuwa nataka niulize kuhusu Sumry....kila mwezi lazima tusikie ajali ya hili bus.....mbona halifungiwi?....

Kiwanda cha ajali za barabarani, lakini wanapeta tuu.

No one thinks straight i tell you, watu ni bure kabisa.

Hiyo ya sumatra kufungia champion itapunguza ajali?
 
Kiwanda cha ajali za barabarani, lakini wanapeta tuu.<br />
<br />
No one thinks straight i tell you, watu ni bure kabisa.<br />
<br />
Hiyo ya sumatra kufungia champion itapunguza ajali?
<br />
<br />
waaapi!upuuzi mtupu.Si walishawahi kuwafungia Mohamed trans na ajali ndo zikazidi.
 
Kwa maamuzi haya ya SUMATRA ni dhairi kuwa tumeshindwa kugundua kiini cha hizi ajali za kila uchao.Miaka ya 90 walikuja na speed governor,wakazuia magari ya abiria kusafiri usiku,kufungia kampuni.Sasa tochi kubaini waendao kasi lakini wapi ngoma iko palepale.Hizi ajali sasa tuzitangaze kuwa ni janga la taifa sasa!
 
mi mwenyewe nilikuwa nataka niulize kuhusu Sumry....kila mwezi lazima tusikie ajali ya hili bus.....mbona halifungiwi?....

Masebu hawezi kujifungia mwenyewe. hawa washenzi wana visa sumry
 
Back
Top Bottom