Abdallah M. Nassor
JF-Expert Member
- Mar 20, 2008
- 600
- 620
Habarini wakuu!
Niende moja kwa moja juu ya utapeli unaofanywa na wakata tiketi wa boti za Azam. Mnamo siku ya Alhamis majira ya saa saba mchana nilifika bandarini nikiwa ni msafiri kwenda Zanzibar. Bajeti ya nauli niliyokuwa nayo ni 25,000 kwenda na kurudu nauli hio hio.
Sasa kufika pale nikaambiwa bei ni 35,000/- nikasema nataka ya 25, mkatishaji akasema labda ukate ya kesho asubuhi. Basi kwa shingo upande nikaongeza 10,000/- nikapewa hio ya elf 35.
Kinachoniuma zaidi ni pale jamaa yangu niliyekuwa nasafiri nae alifika bado robo saa tuanze kuingia melini alikata tiketi ya 25,000/-. Kabla hajafika nilimwambia awahi asijekuta na hizo za 35 zimeisha akaambulia za 50.
Hilo nikalimezea tu nikasema bas labda sio bahati yangu. Kilichoniuma zaidi na zaidi ni huko Zenji, nilifika saa moja kasoro asubuhi kukata tiketi na hapo pia naambiwa hakuna za elfu 25 kwenye boti ya saa tatu zipo za 35, 50 na 60 tu. Kwa shingo upande tena nikakata hio 35.
Jamaa yangu kama kawaida yake kachelewa chelewa badae anakuja bandarini ananipigia simu namwambia nipo humu VIP Lounge, anasema kwani sikupata za 25? Mbona yeye kakata sasa hivi kwa 25!
Kwa kweli nimeumia sana kwani bajeti yangu imeharibiwa na hawa wakata tiketi, hivyo naomba sana SUMATRA komesheni hii hali, yaani wanalazimisha kuuza za bei ya juu kwanza halafu ndio wauze economy. Na wanadanganya kwa kusema zimeisha. Sumatra tusaidieni kwa hili tafadhali.
Nawasilisha wakuu!
Niende moja kwa moja juu ya utapeli unaofanywa na wakata tiketi wa boti za Azam. Mnamo siku ya Alhamis majira ya saa saba mchana nilifika bandarini nikiwa ni msafiri kwenda Zanzibar. Bajeti ya nauli niliyokuwa nayo ni 25,000 kwenda na kurudu nauli hio hio.
Sasa kufika pale nikaambiwa bei ni 35,000/- nikasema nataka ya 25, mkatishaji akasema labda ukate ya kesho asubuhi. Basi kwa shingo upande nikaongeza 10,000/- nikapewa hio ya elf 35.
Kinachoniuma zaidi ni pale jamaa yangu niliyekuwa nasafiri nae alifika bado robo saa tuanze kuingia melini alikata tiketi ya 25,000/-. Kabla hajafika nilimwambia awahi asijekuta na hizo za 35 zimeisha akaambulia za 50.
Hilo nikalimezea tu nikasema bas labda sio bahati yangu. Kilichoniuma zaidi na zaidi ni huko Zenji, nilifika saa moja kasoro asubuhi kukata tiketi na hapo pia naambiwa hakuna za elfu 25 kwenye boti ya saa tatu zipo za 35, 50 na 60 tu. Kwa shingo upande tena nikakata hio 35.
Jamaa yangu kama kawaida yake kachelewa chelewa badae anakuja bandarini ananipigia simu namwambia nipo humu VIP Lounge, anasema kwani sikupata za 25? Mbona yeye kakata sasa hivi kwa 25!
Kwa kweli nimeumia sana kwani bajeti yangu imeharibiwa na hawa wakata tiketi, hivyo naomba sana SUMATRA komesheni hii hali, yaani wanalazimisha kuuza za bei ya juu kwanza halafu ndio wauze economy. Na wanadanganya kwa kusema zimeisha. Sumatra tusaidieni kwa hili tafadhali.
Nawasilisha wakuu!