Sugu aunguruma Bungeni, atetea kazi za wasanii

MANGI MASTA

Senior Member
Jul 14, 2011
175
56
Waziri kivuli wa kambi rasmi ya upinzani mh.Sugu analihutubia bunge..ila jamaaa kweli ni mtetezi wa wasanii kwani analia sana kuhusu wizi wa kazi za wasanii.

HOTUBA YAKE HII HAPA:
HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI MHE.JOSEPH MBILINYI, (MB) WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO, KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2011/2012

UTANGULIZI

Mheshimiwa Naibu Spika,
namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia uhai, afya njema na kunipa fursa ya kipekee ya kufanya maajabu yenye manufaa kwa taifa langu; kwa baraka zake, niliweza kung'ara kwenye sanaa na kuwa nyota wa muziki wa Bongofleva; kwa uwezo wake, leo nimekuwa Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini; na kwa mapenzi yake, mimi Msanii wa Bongofleva sasa nimekuwa Waziri Kivuli wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ya kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu kuwasilisha maoni na mapendekezo ya Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni, na Michezo, kwa mwaka wa fedha 2011/2012, kwa mujibu wa Kanuni za Bunge Kifungu cha 99 (7) toleo la 2007.

Mheshimiwa Naibu Spika
, natambua na kuthamini imani na heshima kubwa niliyopewa na wananchi wa Jimbo la Mbeya Mjini, katika uchaguzi mkuu uliopita. Licha ya kuletewa mabomu ya machozi, virungu na bado hakuna yeyote kati yetu aliyeogopa. Uwongo haukuweza kufunika ukweli na hata rushwa haikuweza kurubuni akili. Wananchi kwa umoja wao walijitoa mhanga kulinda kura zetu bila woga, na hatimaye dunia nzima inajua na imekubali kuwa mimi ndiye SUGU na CHADEMA si chama legelege, bali ni chama makini na kinachoaminika mbele ya jamii.

Mheshimiwa Spika, namshukuru na kumpongeza kwa moyo wa dhati kabisa Katibu Mkuu wa chama changu, Dk. Willibrod Peter Slaa, na makamanda wote wa CHADEMA nchi nzima kwa kazi kubwa tuliyoifanya katika uchaguzi mkuu uliopita, na kwa harakati nzito tunazoendelea kuzifanya za kuielimisha jamii juu ya haki zao za msingi. Watapiga kelele sana, lakini hatutarudi nyuma, tunasonga mbele mpaka kieleweke.

Mheshimiwa Spika,
kwa heshima na taadhima namshukuru Kiongozi Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani na Mwenyekiti wa CHADEMA, Mhe. Freeman Aikael Mbowe (Mbunge) kwa kuniamini na kuniteua kuwa Waziri Kivuli wa wizara hii nyeti; Naibu Kiongozi Mhe. Kabwe Zuberi Zitto (Mbunge) na Mnadhimu Mkuu wa Kambi rasmi ya Upinzani, Mhe. Tundu Lissu, kwa ushirikiano wao mkubwa wanaonipa katika kutekeleza majukumu yangu ya kibunge.

Mheshimiwa Spika,nachukua fursa hii pia kuwashukuru kwa dhati wadau wote wa Sekta ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, kwa kutuamini na kuthamini kazi kubwa ya uwakilishi inayofanywa na Kambi rasmi ya Upinzani bungeni, hata kuamua kutupa ushirikiano mkubwa katika maandalizi ya hotuba hii.

Naomba niwatambue baadhi ya wadau hao kwa shukrani kama ifuatavyo: ·Baraza la Habari Tanzania (MCT) ·Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) ·Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na, ·Rulu Arts Promotion SEKTA YA HABARI Weledi na Maadili ya Uandishi wa Habari.

Mheshimiwa Spika, vyombo vya habari ni taasisi muhimu sana katika ujenzi wa taifa lenye kufuata misingi ya demokrasia na utawala bora. Vyombo vya habari vina dhima kubwa ya kutoa habari na taarifa kwa umma wa Watanzania kuhusu mambo yanayohusu maisha yao na vilevile kutoa elimu na burudani. Vyombo vya habari ni kiungo muhimu cha kuunganisha jumuiya mbalimbali, kujenga utaifa, umoja na kuhimiza maendeleo.

Mheshimiwa Spika, Vyombo vya habari kwa ujumla wake ni taasisi yenye nguvu. Ina uwezo mkubwa wa kujenga na vilevile kubomoa ikiwa vitatumiwa na kujiendesha vibaya au kuingiliwa uhuru wake. Hivyo basi, wakati vyombo vya habari vina wajibu wa kufanya kazi kwa kuzingatia umakini, weledi na maadili ya uandishi wa habari, Serikali nayo ina wajibu mkubwa wa kuhakikisha uhuru na haki za kutafuta na kupata habari vinalindwa.

Mheshimiwa Spika, ni ukweli usiotiliwa shaka kuwa baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikikiuka kabisa maadili ya uandishi wa habari. Kinachosikitisha zaidi ni pale ambapo baadhi ya waandishi wa habari na baadhi ya vyombo vya habari na ambavyo vimepewa dhamana kubwa na jamii wanapokubali kutumiwa na baadhi ya watu wenye nguvu ama za kisiasa au za kifedha ili kuendeleza ajenda zao binafsi. Hili ni jambo lisilopendeza hata kidogo na halina mustakabali mzuri kwa amani na maendeleo ya nchi yetu.

Mheshimiwa Spika
, kinachosikitisha zaidi, vyombo vya habari vya Serikali na hapa nalizungumzia gazeti la serikali Daily News kuongoza katika ukiukwaji wa maadili ambapo katika kipindi cha mchakato wa uchaguzi mkuu uliyopita gazeti hili lilichapisha tahariri ya uchochezi iliyosema, "Kamwe Dk. Slaa hatakuwa rais wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania." Maoni haya ya Mhariri yalilenga kuleta uchochezi na kujenga hoja kwamba hata kama Watanzania watamchagua Dk. Slaa kuwa rais wao, lakini kamwe hatakabidhiwa jukumu la uongozi, jambo ambalo ni la hatari kwa usalama wa taifa.

Mheshimiwa Spika
, jambo la hatari zaidi hapa ni kwamba walioendesha vitendo hivi vya uchochezi ni wahariri wa gazeti la serikali ambalo lilitakiwa kuwa mfano wa kuigwa kwa vyombo vingine vya habari nchini.

Mheshimiwa Spika, Kambi ya upinzani inaitaka serikali ilieleze Bunge hili tukufu imemchukulia hatua gani Kaimu Mhariri Mtendaji wa gazeti hilo ambaye aliidhinisha kuchapishwa kwa tahariri hiyo? Je, Idara ya Habari na Maelezo iliwahi kuandika barua kwa mhariri huyu kumuonya kama ambavyo imekuwa ikifanya hivyo kwa magazeti mengine; hata kabla ya habari haijaandikwa, tayari barua inakuwa imeandaliwa na kinachosubiriwa ni gazeti kuchapishwa na barua hiyo kufika kwa wahusika?

Kama serikali haijamchukulia hatua, waziri anaweza vipi kuwa na mamlaka ya kuadhibu vyombo vingine vinavyodaiwa kukiuka maadili ya uandishi wa habari wakati yenyewe imeshindwa kuwajibisha wahariri wa gazeti lake? Mheshimiwa Spika, kuna tabia imezuka ya viongozi wa Serikali kuvitisha vyombo ya habari pale vinapotoa udhaifu wa watendaji Serikalini, kama ilivyotokea hapa Bungeni wakati Mhe. Waziri Ofisi ya Rais mahusiano alipotoa vitisho kwa gazeti la Mwananchi. Kambi ya Upinzani inalaani kitendo hicho na kuitaka Serikali iache mara moja.

Mheshimiwa Spika, hili ni jambo ambalo wote tunatakiwa tulikemee kwa nguvu zetu zote na kila inapowezekana tuwaumbue na tuwataje wale wote wanaoshiriki katika matendo haya ambayo hayana nia njema sio tu kwa tasnia yenyewe ya habari kwa kuipa jina baya na kuipaka matope, bali pia kwa nchi yetu kwani tuna mifano dhahiri hapa Afrika na kwingineko duniani juu ya athari ambazo zimewahi kutokea vyombo vya habari vilipotumika vibaya. Na sote tunakumbuka yaliyofanywa na vyombo vya habari vya serikali kule Rwanda na maafa yaliyotokea. Sheria ya Haki ya Kupata Habari.

Mheshimiwa Spika,
haki ya kupata habari ni haki ya msingi ya binadamu na inalindwa na Ibara ya 18 ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni haki ambayo inamhusu kila Mtanzania bila ya kujali wadhifa au daraja lake kwenye jamii, umri au jinsia. Mwaka 2006, na nataka niamini kwa nia njema kabisa, Serikali ilianzisha mchakato wa kutunga sheria ya Uhuru wa Habari kwa kutoa rasimu ya muswada wa sheria hiyo.

Mheshimiwa Spika,
hata hivyo rasimu ya muswada huo ilikataliwa na wadau kwa sababu haikukidhi haja wala viwango vya sheria kama hiyo vinavyotakikana. Mwaka 2007, Serikali iliitikia wito wa wadau wa habari na haki za binadamu wa kutaka kuwepo na sheria mbili tofauti na kutenganisha rasimu yake ya Muswada wa Sheria ya Uhuru wa Habari na kutengeneza rasimu mbili, moja ya sheria ya Haki ya Kupata Habari na nyingine ya sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari.

Mheshimiwa Spika, hoja ya kutenganisha muswada huo ilikuwa na bado, ni muhimu sana, kwa sababu sheria ya haki ya kupata habari ni mtambuka na inahusu haki ya kikatiba ya Watanzania wote. Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ni ya kisekta na inahusiana zaidi na kutoa mwelekeo wa jinsi vyombo vya habari vitakavyofanya kazi nchini.

Mheshimiwa Spika,
mchakato huo ulipata muitiko mzuri kutoka kwa wadau mbalimbali wa habari na wanaharakati wa haki za binadamu ambao kwa umoja wao walitembea nchi nzima kukusanya mawazo na mapendekezo ya wananchi kuhusu Sheria ya Haki ya Kupata Habari. Walipeleka mapendekezo yao kwa Serikali ili yaweze kujumuishwa katika mchakato wa utungaji wa sheria.

Mheshimiwa Spika,
Kambi rasmi ya Upinzani inasisitiza kuwa Sheria hii ni muhimu sana, kwani itaimarisha utawala wa wazi na uwajibikaji. Utawala ulioshamiri katika mila za usiri ndio ulioifikisha Tanzania yetu mahali pabaya. Ndio chanzo cha mikataba mibovu na kushindwa kwa uwajibikaji kwa sababu tu watendaji wabovu wanaweza kujificha katika kinga ya usiri.

Mheshimiwa Spika,
Serikali imekuwa ikitoa ahadi mwaka hadi mwaka kuhusu mchakato wa utungaji wa sheria hii muhimu. Lakini hadi leo hatujaona muswada wa sheria hiyo ukiacha ule ambao wadau wamependekeza. Kambi rasmi ya Upinzani tunaitaka Serikali kuuleta bungeni muswada wa sheria hiyo ndani ya mwaka huu, ili tuujadili na kupitisha sheria hiyo bila ya kukawia zaidi.

Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani tunaitahadharisha serikali kuwa isijaribu kuchakachua hata kidogo maoni hayo ya wadau, kwa sababu tumejiridhisha kuwa yana msingi na dhamira ya dhati ya kuboresha tasnia nzima ya habari na uhuru wake. Pendekezo la wadau limo katika Kiambatanisho Na. 1 cha hotuba hii. Tunachukua fursa hii kuwataarifu mapema wadau wote wa habari kwamba tutakuwa pamoja nao wakati wote wa harakati za kushinikiza muswada huo uletwe bungeni ndani ya mwaka huu. Tunataka sheria hiyo ipatikane mapema iwezekavyo ikiwa imebeba maoni yote ya wadau.

Mheshimiwa Spika, pamoja na umuhimu wa kupata sheria mpya ya vyombo vya habari, ni muhimu pia kuwapo kwa sheria inayokidhi mahitaji na inayokubalika kwa jamii yote ya wananchi. Sheria ya habari katu, si mali ya waandishi wa habari na wamiliki wa vyombo vya habari pekee yao. Ni sheria ya Watanzania wote. Hii ni kwa sababu, haki ya kupata na kutoa habari, ni haki ya asili.

Mheshimiwa Spika,
wakati wananchi wanasubiri sheria mpya ya habari, Kambi ya Upinzani inaitaka serikali kuleta bungeni muswada wa kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 kwa kuwa sheria hiyo ni kinyume na Katiba. Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari.

Mheshimiwa Spika, katika sera ya Habari na Utangazaji iliyotolewa na Serikali na kupitishwa na Bunge lako tukufu mwaka 2003, kipengere cha 2.2.2 kinaelekeza kwamba; "Sheria mbovu za habari ambazo zimekuwa zikikosolewa na kulalamikiwa kwa kuwa haziendani na misingi ya kidemokrasia zitadurusiwa, kurekebishwa au kufutwa." Hivyo basi, Serikali iliahidi kuwa itatunga sheria mpya zinazoendana na wakati na kukidhi mahitaji ya kidemokrasia ya wananchi.

Mheshimiwa Spika,
tunasisitiza kuwa mapendekezo ya wadau yanakidhi kwa kiwango kikubwa ahadi hiyo ya Serikali na wadau walizipitia sheria 27 zinazogusa habari na kupendekeza sheria 17 miongoni mwa hizo ama zidurusiwe, zirekebishwe au kufutwa. Kambi rasmi ya Upinzani inaitaka serikali isiendelee kusuasua katika jambo hili na ilete muswada bungeni wa Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari ndani ya mwaka huu wa fedha.

Mheshimiwa Spika,
hadi sasa shirika linalochapisha magazeti ya Serikali (DAILY NEWS NA HABARI LEO) halina Mtendaji Mkuu, toka alipoondolewa Mtendaji aliyekuwepo. Tangazo la kumtafuta mtendaji mpya mwenye sifa na hadhi ya kuongoza liliondolewa katika mazingira tatanishi. Hivi sasa shirika hilo limeyumba kiuongozi jambo ambalo limesababisha kushuka kwa uzalishaji. Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali kuanzisha mchakato wa kumpata Mtendaji mkuu wa shirika hilo mwenye sifa na hadhi, kabla ya mwaka huu haujamalizika. MAENDELEO YA VIJANA Benki ya Taifa ya Vijana Ianzishwe.

Mheshimiwa Spika, sehemu kubwa ya watu wa taifa hili ni vijana, tukiendeleza vijana basi tutakuwa tumeendeleza sehemu kubwa ya taifa. Ni muhimu kama taifa tuweke vipaumbele vya makusudi vya kibajeti vya kuhakikisha vijana wanapewa kipaumbele cha kutosha na kujengewa mazingira mazuri ya kujikomboa.

Mheshimiwa Spika,
ili kuanza kujenga mazingira mazuri ya kuchochea ajira nyingi kwa vijana kupitia shughuli za ujasiriamali na shughuli nyingine za kiuchumi, Kambi rasmi ya Upinzani, inaitaka Serikali ianzishe Benki ya Taifa ya Vijana. Tunapendekeza kuwa mchakato wa kuanzishwa kwa benki hiyo uanze ndani ya mwaka wa fedha wa 2011/2012, na benki hiyo iwe na masharti nafuu kwa manufaa ya vijana. Mchakato wa Baraza la Vijana la Taifa.

Mheshimiwa Spika, kwa mara ya kwanza Serikali iliahidi kuanzisha Baraza la Taifa la Vijana kupitia Sera ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 1996, na tangu wakati huo kila mwaka Serikali imekuwa ikiahidi hivyo hivyo, lakini hadi leo hakuna kilichofanyika.

Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani haiko tayari tena kuona Serikali hii ikiwapotezea muda vijana wa nchi hii. Tunamtaka Waziri atoe kauli ya moja kwa moja ya kuhakikisha kuwa mchakato wa kuanzishwa kwa Baraza la Taifa la Vijana unaanza mara moja na Baraza linapatikana ndani ya mwaka huu wa fedha. Haja ya Mabadiliko Idara ya Maendeleo ya Vijana.

Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani inaamini kuwa hali mbaya ya maendeleo ya vijana nchini, pia inachangiwa na uongozi dhaifu usiokuwa na ubunifu wa kutosha wa Idara ya Maendeleo ya Vijana, ambao kwa takribani miaka 10 umekuwa na watu walewale kwenye nyadhifa takribani zote ikiwemo ile ya Mkurugenzi. Kwa hiyo, tunataka Serikali kuifanyia mabadiliko ya viongozi Idara hii ili kuleta ari na ubunifu mpya kikazi. Sanjari na hilo, tunapendekeza Idara hii iongezewe nguvu na raslimali. SEKTA YA UTAMADUNI.

Mheshimiwa Spika, ni ukweli ulio wazi kuwa sekta ya utamaduni kwa sasa imepoteza mwelekezo kwa sababu mipango mingi ya maendeleo haizingatii umuhimu wa utamaduni wetu kwa tafsiri pana. Maendeleo ya jamii yoyote ile yanategemea utamaduni wa nchi husika, hivyo Kambi ya Upinzani inasisitiza kuwa ni lazima Serikali irudi nyuma na kujitathimini vizuri katika sekta ya Utamaduni.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tunaishi katika kipindi muhimu cha mpito wa historia na utamaduni ya tangu kizazi cha uhuru na kile kilichozaliwa baada ya uhuru, ni muhimu kuhakikisha kuwa historia na utamaduni wetu, unakusanywa, unachambuliwa na kuhifadhiwa vizuri kwa ajili ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo; Kambi rasmi ya Upinzani inapendekeza kuwa Serikali iunde Kamisheni Maalum ya Rais ya Historia, ambayo pamoja na mambo mengine, iwe na majukumu yafuatayo:

(i)Kufanya utafiti wa watu wote waliotoa mchango mkubwa wa kihistoria katika kupigania Uhuru wa Tanganyika, Mapinduzi ya Zanzibar na Muungano ili waweze kukumbukwa na michango yao kuenziwa.

(ii)Kutambua maeneo, majengo, na sehemu mbalimbali zenye umuhimu mkubwa wa kihistoria.

(iii)Kupitia matukio muhimu ya historia yetu ili yaweze kuelezewa katika mwanga wa kihistoria. Hii ni pamoja na Uhuru, Mapinduzi, Muungano, Uasi wa Jeshi, Azimio la Arusha, Operesheni Vijijini, Vita ya Kagera, Enzi za soko huria, n.k.

(iv)Kukusanya vielelezo mbalimbali vyenye umuhimu mkubwa wa kihistoria kutoka watu binafsi, taasisi binafsi na nje ya nchi ili hatimaye vitu hivyo, viweze kuingizwa katika historia yetu kwa ajili ya kuwa ni urithi wa vizazi vijavyo.

(v)Kuandika ripoti maalum juu ya historia yetu na matukio mbalimbali ili yaweze kutunzwa kama sehemu ya historia yetu maalum.

(vi)Kutoa mapendekezo ya jinsi ya kuenzi utamaduni wetu muhimu pamoja na watu mbalimbali ambao walichangia katika matukio mbalimbali kwa namna ya pekee na ambao historia yetu haijawakumbuka ipasavyo.

SEKTA YA SANAA


Mheshimiwa Spika,
nianze kwa kutangaza maslahi kwenye sekta hii, kuwa mimi ni msanii wa muziki wa kizazi kipya (Bongofleva) na nimekuwa kwenye fani hii kwa muda mrefu sasa. Kwa uzoefu wangu na kwa niaba ya Kambi rasmi ya Upinzani, nachukua fursa hii kuieleza serikali kwamba: "Sanaa si mapambo au burudani tu kama ilivyozoeleka, bali Sanaa ni ajira inayoweza kubadilisha maisha ya Mtanzania yeyote anayejihusisha nayo na inaweza kabisa kuwa moja ya vyanzo vikubwa vya mapato ya Bajeti ya Serikali, ikiwa Serikali yenyewe itadhamiria kwa dhati kufanya mapinduzi makubwa katika tasnia hii".

Mheshimiwa Spika, taarifa mbalimbali kutoka nchini Marekani za mwaka 2007 zilionyesha kuwa; "Makampuni yanayotengeneza na kuuza kazi za hatimiliki yataendelea kuwa moja ya nguvu kubwa za uchumi wa Marekani, kwani mapato yatokanayo na filamu, muziki, michezo ya video, na mifumo ya kompyuta yanachangia zaidi ya asilimia 6.5 ya Pato la Taifa na kuajiri takribani watu milioni 5.4…" mwisho wa kunukuu.

Mheshimiwa Spika,
ni dhahiri kuwa sekta ya Sanaa ikifanyiwa mapinduzi makubwa inaweza kabisa kuwa moja ya vyanzo vikubwa vya bajeti ya Serikali yetu na kuchangia maendeleo ya taifa hili. Ikiwa Sanaa inachangia kwa kiasi kikubwa uchumi wa taifa kubwa kama Marekani; Je, Tanzania tuna maendeleo gani ya kujivunia hata tupuuze Sanaa? Bado hatujaipa sekta hii umuhimu wake unaostahili.

Mheshimiwa Spika, wasanii pamoja na Serikali bila kujua, wamekuwa wakinyonywa kimapato na wadhamini, wazalishaji, na wasambazaji wa kazi za Sanaa, hususan kwenye biashara ya kuuza muziki na filamu. Kwa mujibu wa utafiti wa Dkt. Jehovaness Aikaeli ambaye ni mchumi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), alisema sekta ya muziki pekee ikifanyiwa maboresho, inaweza kuiingizia Serikali mapato ya kodi ya wastani wa shilingi bilioni 50 kwa mwaka.

Mheshimiwa Spika,
tafiti chache zilizowahi kufanyika, ukiwemo utafiti wa Taasisi ya RULU/BEST – AC, wa mwaka 2007/08, zimeonyesha kuwa Wasanii na Serikali kwa pamoja, wamekuwa wakipoteza mapato mengi yatokanayo na biashara ya kazi za sanaa, hususan muziki na filamu kama ifuatavyo: ·Maharamia wameendelea kurudufisha santuri na kanda za muziki, filamu na kazi nyingine za sanaa, na kujipatia mapato haramu kwa jasho la Wasanii, lakini hakuna hatua kali zinazochukuliwa kukomesha hali hii. ·

Wasanii wengi wamekuwa wakiingia mikataba isiyo na manufaa kwao baina yao na Wadhamini, Wazalishaji, Wasambazaji wa kazi za Sanaa na hivyo kunyonywa kimapato, kwa sababu tu ya kukosa uelewa mzuri wa masuala ya mikataba na kutokuwepo udhibiti wa kutosha wa Serikali. ·Serikali kwa mwaka 2007 pekee, ilipoteza mapato ya muziki, ya jumla ya shilingi bilioni 71.

·Kodi inayokusanywa na Serikali katika Sekta ya Muziki, inapatikana katika asilimia 12 tu ya kiwango cha mapato kinachotakiwa kulipiwa kodi kwenye sekta hiyo. ·Wakati wa utafiti iligundulika kuwa ni asilimia 12.5 tu ya Wafanyabiashara wa kazi za Sanaa, ndio waliokuwa wamelipa mirabaha, asilimia 87.5 hawakuwa wamelipa.

Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na wizi na uharamia huu wa kazi za Sanaa na kuokoa mapato ya Wasanii na ya Serikali, Kambi rasmi ya Upinzani inapendekeza yafuatayo:


COSOTA iwe Mamlaka.

Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani inapendekeza kuwa Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki Na.7 ya mwaka 1999 ifanyiwe marekebisho kwa lengo la kuipa meno zaidi ya kulinda haki na kuhakikisha Wasanii wananufaika na kazi zao. Moja ya mapendekezo ni kuifanya COSOTA kuwa chombo chenye nguvu zaidi katika kulinda kazi za Wasanii kuliko ilivyo hivi sasa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyokatika sehemu ya marekebisho tunayopendekeza, Kambi rasmi ya Upinzani tunataka Sura Na. 218 ya Sheria ya Hakimiliki na Hakishiriki, ifanyiwe marekebisho ili kuunda Mamlaka ya Hakimiliki Tanzania (COPYRIGHT REGULATORY AUTHORITY OF TANZANIA (CORATA) badala ya kuiacha COSOTA kama ilivyo hivi sasa.

Mamlaka haya yakishaundwa yatakuwa na nguvu zaidi ya kushughulikia mambo mbalimbali ya kazi za wasanii,yawe ndio msimamizi na mratibu wa masuala ya Hakimiliki kwa kushirikiana na vyama vya msingi vya wasanii vilivyopo chini ya BASATA,kama vile Chama Cha Muziki Wa Dansi Tanzania(CHAMUDATA) na kile cha wasanii wa muziki wa kizazi kipya yaani Tanzania Urban Music Association (T.U.M.A), tofauti na sasa ambapo COSOTA imebakiwa na kazi ya kusajili kazi za wasanii na kukosa nguvu ya kuzilinda.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuwa mwenye Hakimiliki ana jukumu la kulinda haki zake kwa kwenda mahakamani pale anapoona haki yake imepokwa na mtu au kikundi chochote, bado ipo haja ya kuhakikisha kuwa Polisi wetu wa upelelezi wanahusika moja kwa moja katika kulinda haki za Wasanii. Mathalan, nchini Marekani hawana polisi wa kulinda hakimiliki moja kwa moja, lakini Shirika lao la Upelelezi (FBI), limekuwa likifanya uchunguzi wa mara kwa mara kuhusu hakimiliki za wasanii, kila kunaporipotiwa suala la wizi wa kazi za msanii, na limekuwa linahusika moja kwa moja katika kutoa ushahidi na kusaidia kupatikana kwa haki ya msanii husika.

Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani inapendekeza kuwa taasisi za Serikali, Polisi na Forodha washirikiane kwa karibu na Mamlaka ya Hakimiliki na Hakishiriki tunayotaka ianzishwe (CORATA), kukomesha uharamia wa kazi za Sanaa. Forodha watengeneze utaratibu wa kutoza kodi kikamilifu kwenye kazi za muziki, filamu na Sanaa nyingine zote zinazouzwa nje ya nchi. Na mashirika ya uzalishaji wa kazi za muziki –waunde ushirikiano na taratibu zao za kukabiliana na uharamia wa kazi za sanaa kwa mapana yake.

Mheshimiwa Spika,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwezi Februari mwaka huu, wakati akizindua kampeni ya kuzuia malaria ambayo iliwashirikisha baadhi ya wasanii, aliahidi kuundwa kikosi kazi (task force) kitakachowashirikisha COSOTA, Polisi, Tume ya ushindani, TRA, BRELA, Wizara ya Viwanda na Biashara pamoja na wasanii mbalimbali wanaojihusisha na sanaa ili kutafuta ufumbuzi dhidi ya uharamia na wizi wa kazi za Sanaa.


Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani inaitaka wizara kuliarifu Bunge hili, je kikosi kazi hicho kiko wapi mpaka leo? Na kama kiliundwa, kiliundwa kwa taratibu zipi, na kwanini suala hilo haliko wazi?

Mradi wa Stickers kwenye kazi za Sanaa

Mheshimiwa Spika, mbali na marekebisho hayo ya kisheria na kimfumo tuliyopendekeza, Kambi rasmi ya Upinzani pia tunaitaka Serikali ndani ya mwaka wa fedha wa 2011/2012, itenge fedha za kutosha kwa ajili ya kuanzisha utaratibu rasmi wa kuwa na Stickers kwa ajili ya kazi zote za Sanaa, hususan kwenye kanda na Santuri za muziki, filamu, na kazi zote za Sanaa zinazoshikika na kuuzika. Hapa tunashauri kuwa mamlaka tunayotaka ianzishwe, yaani COPYRIGHT REGULATORY AUTHORITY OF TANZANIA) ishirikiane kwa karibu na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kuandaa utaratibu mzima wa kuwa na Stickers hizo na jinsi ya kuusimamia.

Mheshimiwa Spika,
Kambi rasmi ya Upinzani inaamini kuwa utaratibu rasmi wa kuwa na Stickers ukitumika sekta ya Biashara ya Kazi za Sanaa inaweza kupata mafanikio ya kuridhisha ndani ya muda mfupi. Mfano mzuri ni Sticker yenye nembo ya TRA inayowekwa kwenye bidhaa za Konyagi. Faida kubwa ambayo itapatikana kwa kuwa na Stickers kwenye kazi za Sanaa ni kuwa stickers hizi zitawezesha kubaini kazi halisi (Original) iliyofanywa na msanii mhusika dhidi ya kazi za bandia zilizorudufishwa au kughushiwa.

Sambamba na hilo, mapato ya Wanamuziki, Watunzi wa filamu na washirika wao pamoja na Serikali yataongezeka na hivyo mchango halisi ya sekta hii kwenye uchumi wa nchi utakuwa wazi. Mheshimiwa Spika, pia tuna taarifa kuwa Wasanii wengi kutoka nje ya nchi wanaofanya maonyesho mbalimbali hapa nchini wamekuwa hawatozwi kodi licha ya kulipwa fedha nyingi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Spika, tunaitaka Serikali kuanzia mwaka wa fedha wa 2011/2012, ihakikishe kuwa Wasanii hao wa nje ya nchi ambao wamekuwa wakilipwa dola laki 1hadi dola laki 4 kwa onyesho moja hapa nchini, wawe wanatozwa kodi ya kutosha, ili fedha hizo ziongezee bajeti kuu ya Serikali na kuwasaidia Watanzania wengi maskini.

Mheshimiwa Spika, tunaitaka Serikali kwa kushirikiana na vyombo husika, iweke utaratibu wa kuhakikisha kuwa pale Msanii wa ndani anapofanya onyesho au kazi ya pamoja na Msanii kutoka nje, basi kuwe na mgawanyo mzuri na wa haki wa mapato kati ya Msanii huyo wa Nje na Msanii Mzawa.

Mheshimiwa Spika, ili kuboresha Sekta nzima ya Sanaa nchini, na kuhakikisha inaongeza ajira zenye tija, na kutoa mchango mkubwa katika ukuaji uchumi, Kambi rasmi ya Upinzani inapendekeza hatua zifuatazo zichukuliwe; ·Serikali ndani ya mwaka wa fedha wa 2011/2012,pamoja na kufanyia kazi tafiti zilizokwishafanywa na wadau mbalimbali wa sanaa, ifanye utafiti mahsusi na wa kina kuhusu Sekta nzima ya Sanaa (Feasibility Study), ili kubaini fursa na vikwazo vyote vilivyopo, na kuainisha njia na mikakati kabambe ya kuboresha na kuisimamia sekta husika, kwa manufaa ya Wasanii na uchumi wa nchi. ·

Kupitia matokeo ya utafiti huo, Wizara ndani ya mwaka wa fedha 2011/2012, iandae Mpango mahsusi wa Maboresho ya Sekta ya Sanaa, ambao pamoja na mambo mengine, ulenge kuziba mianya yote ya upotevu wa mapato ya Sanaa na kuchochea ajira nyingi na zenye tija kwa vijana.

·Chuo Kikuu cha Sanaa cha Bagamoyo kipandishwe hadhi na kuwa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Kawawa cha Bagamoyo (Kawawa Memorial University – Bagamoyo). Lengo liwe ni kuhakikisha kuwa chuo hiki kinatoa mafunzo yote ya hali ya juu ya mambo ya sanaa, michezo na utamaduni kwa vijana wa Kitanzania na wale wanaotoka ng'ambo, huku tukimuenzi Hayati Mzee Rashid Mfaume Kawawa, kwa mchango wake mkubwa katika taifa hili alioutoa kwenye uongozi na Sanaa. ·

Serikali ihakikishe kuwa asilimia 90 ya bajeti zote za Wizara, Idara, Taasisi na Wakala wa Serikali zinazotengwa kwa ajili ya kunaksisha ofisi, iwe inatumia kazi za sanaa na samani zinazopatikana hapa Tanzania au zinazotokana na ubunifu wa Watanzania. Hii itachochea ajira katika kazi za Sanaa na kuweka ushindani wa kibiashara ambao utainua ubora wa kazi hizo.

·Masomo ya Sanaa yarudishwe katika ngazi zote za elimu katika shule za binafsi na serikali, ili kuchochea ubunifu na umahiri wa vijana katika kazi za sanaa na kuinua vipaji vyao mbalimbali. ·Serikali ihakikishe mafunzo ya Sanaa yanatolewa kwa vyuo vya elimu ili kuweza kupata walimu wa kutosha wa sekta hii. ·Mashindano ya ubunifu wa kazi za Sanaa yaanzishwe yakiwa ni sehemu ya mashindano ya michezo ya UMISHUMTA na UMISETA.

Kashfa ya Nyumba ya Sanaa


Mheshimiwa Spika,
Nyumba ya Sanaa ilianzishwa mnamo 1972 kwa madhumuni ya kutoa mafunzo ya Sanaa kwa vijana, wanawake na wasiojiweza pamoja na kutafuta masoko ya Sanaa na kazi za mikono. Hata hivyo, kuanzia mwaka 1995 kumekuwepo hali ya kutoelewana baina ya wajumbe wa Bodi ya wadhamini baada ya kutiliana shaka wenyewe kwa wenyewe, pia kati ya Bodi ya Wadhamini na Wanachama waanzilishi wa Nyumba ya Sanaa.

Mheshimiwa Spika,
matokeo ya hali hiyo ni kufunguliwa kwa kesi mahakamani. Katika kesi hiyo, iliyotolewa hukumu tarehe 24 Februari, 2005, Msajili aliamua kufuta rasmi usajili wa Bodi ya Wadhamini ya Nyumba ya Sanaa akiwataka wakabidhi mali na shughuli za NYUMBA kwa asasi mbadala. Uchunguzi uliofanywa na Kambi rasmi ya Upinzani umebaini kuwa tangu kutolewa kwa hukumu hiyo, Bodi haijawahi kukasimisha amali na majukumu ya Nyumba ya Sanaa kwa asasi mbadala, na badala yake imeendelea kuwepo na kupelekea Nyumba hiyo kuendeshwa kama kampuni binafsi kwa faida ya wajumbe wachache wa Bodi.

Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani ina taarifa kuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo iliyofutwa na baadhi ya wajumbe wake wameleta mwekezaji ambaye wameshaingia naye ubia kimkataba, kwa ajili ya kujenga jengo la ghorofa katika eneo lenye jengo la sasa. Izingatiwe hapa kuwa mwekezaji atapaswa kulivunja au kubadilisha mfumo wa jengo la sasa la Nyumba ya Sanaa, ndipo aweze kujengwa la ghorofa.

Mheshimiwa Spika
, Kambi rasmi ya Upinzani, inaitaka serikali na Bunge lako tukufu lizingatie yafuatayo; ·Tujue kuwa Nyumba ya Sanaa hivi sasa inawanufaisha wachache ambao si walengwa waliokusudiwa. Tufahamu kwamba wanufaika hawa hawana rekodi ya uwekezaji katika Nyumba ya Sanaa, hivyo wanavuna matunda yaliyopandwa na wengine hasa kupitia ushirikiano mwema baina ya serikali ya Tanzania (kupitia Ikulu), Norway (kupitia shirika la NORAD) na Uholanzi (kupitia shirika la NOVIB).

·Tutambue kuwa Nyumba ya Sanaa ilikuwa ni mlango wa masoko ya Sanaa na kazi za mikono, hivyo kutokuwepo kwake kunakwamisha juhudi za wazalishaji kazi za sanaa wa Tanzania kuweza kushiriki vyema masoko na hasa soko la pamoja la Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Spika
, kwa kuyazingatia yote hayo na kwa manufaa ya wadau wote wa Sanaa na taifa zima kwa ujumla, Kambi rasmi ya Upinzani inaitaka serikali ichukue hatua zifuatazo kuhusiana na Nyumba ya Sanaa:-

Mheshimiwa Spika, kwanza tunataka Nyumba ya Sanaa irudishwe Serikalini kwa Mdhamini Mkuu wa Serikali ili mchakato wa uanzishwaji wa Bodi huru ya kusimamia malengo yake anuai ufanyike. Uhuishaji wa Nyumba ya Sanaa utachangia sana kuongeza ajira na pato la taifa, hivyo kupunguza tatizo la uzururaji na kilio cha masoko ya kazi za sanaa.

Mheshimiwa Spika,
kwa kuwa tangu kufutwa kwake mnamo mwaka 2005, Nyumba ya Sanaa imeendelea kufanya biashara pamoja na kuingia mikataba ya biashara mpaka sasa, Kambi rasmi ya Upinzani tunaitaka serikali ifanye tathmini na ilipwe kodi kutokana na faida ya biashara zilizoendeshwa mara baada ya kusitishwa uendeshaji wake.

Mheshimiwa Spika,
Kambi rasmi ya Upinzani tunaitaka Serikali isitishe mara moja uvunjwaji wa jengo lililopo sasa, kwani ni utalii na ni alama ya taifa inayoonyesha jinsi serikali za Norway na Tanzania zilivyothamini juhudi za wasanii na wazalishaji kujikwamua kiuchumi na kuchangia pato la Taifa. Tunataka Nyumba ya Sanaa ifufuliwe upya bila kubadili malengo yaliyopelekea kujengwa kwake, na badala yake kila kitu kiboreshwe kwa kuheshimu malengo yale yale.

Tunaamini Serikali hii inayojiita Serikali sikivu, itaheshimu matakwa ya Watanzania hususan Wasanii ambao pasipo shaka yoyote ile wanataka Nyumba yao irudi kwenye mikono salama kama tulivyopendekeza.


Ahadi ya Studio ya Wasanii


Mheshimiwa Spika,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, kupitia Bunge Tukufu la Jamhuri ya Muungano alitangaza kuwa amewapa Wasanii Studio ya kufanyia kazi zao. Hata hivyo, baadaye wananchi na wadau wengi wa sanaa, nikiwemo mimi binafsi, tulishangaa kusikia Studio hiyo wamepewa NGO binafsi ya Tanzania House of Talent (THT)! Pia Rais aliahidi na kutoa nyumba ya Serikali kwa Wasanii ambayo ingetumika kuendeshea Studio husika, lakini nyumba hiyo ya Serikali iliyotolewa na Rais sasa iko chini ya THT na ndio makao ya THT!

Mheshimiwa Spika,
Kambi rasmi ya Upinzani inahoji, kwanini ahadi hizo zitolewe kwa kikundi kimoja tu cha THT, tena kilichojikita zaidi katika biashara ya kazi za Sanaa, wakati ahadi hizo za Rais zililenga Wasanii wote wa Tanzania? Kambi rasmi ya Upinzani inatambua na kuthamini mchango wa THT katika Sekta ya Sanaa ya nchi hii, lakini si sahihi kwa taasisi hiyo binafsi kupewa jukumu la kuhodhi Studio na Nyumba iliyotolewa na Rais kwa ajili ya Wasanii wote.

Mheshimiwa Spika,
badala yake, Kambi rasmi ya Upinzani inapendekeza kuwa Studio na Nyumba hiyo iliyotolewa na Rais iwe chini ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA)kwa manufaa ya Wasanii wote na si THT peke yao kama ilivyo sasa. Tunatahadharisha kuwa hili lisipozingatiwa, jina la Rais na hadhi ya Urais itachafuka kwa kuonekana kufanya kazi kwa maslahi ya watu binafsi (THT) badala ya kufanya kazi kwa maslahi ya umma (Wadau wa Sanaa).

SEKTA YA MICHEZO


Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya Upinzani inaamini kuwa Michezo ni Afya, Michezo ni Burudani, Michezo ni Ajira na Michezo ni Uchumi. Hata hivyo, mwenendo na hali halisi ya Sekta ya Michezo nchini, vinadhihirisha kuwa sekta hii imekuwa ikichukuliwa kuwa ni ya burudani pekee. Timu zetu za taifa zifungwe au zitolewe kwenye michuano ya kimataifa, limekuwa ni jambo la kawaida, hakuna hatua zozote kali zinazochukuliwa kuwajibishana wala kuweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha hali ya kufanya vibaya haijurudii tena.

Mheshimiwa Spika, ushahidi kuwa Sekta ya Michezo haijapewa umuhimu unaostahili upo wazi. Taifa letu limeendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu, kwa timu zetu za taifa kuendelea kufanya vibaya na kuambulia mafanikio kidogo kwenye michuano ya kimataifa. Kama taifa tumeshindwa kuzalisha walimu wa kutosha wa michezo mbalimbali, na mbaya zaidi hata walimu wachache wazalendo hususan wa mpira wa miguu, wenye ujuzi na umahiri wa kuridhisha wamekuwa hawapewi motisha, pindi wanapoteuliwa kufundisha timu za taifa. Badala yake, Serikali imekuwa ikitumia gharama kubwa kuwapa ajira Walimu wa kigeni.

Kambi ya Upinzani inamtaka Mhe. Waziri alieleze Bunge katika kipindi chote timu ya taifa ya vijana ilipokuwa chini ya kocha Tinoco toka Brazil, mkataba wake kwa mwezi alilikuwa akilipwa kiasi gani na Kocha wa sasa Jamhuri Kiwelu (Julio) mzawa analipwa kiasi gani?


Mheshimiwa Spika, Kambi ya Upinzani inaitaka Serikali ilieleze Bunge ni kwanini kocha wa netiboli, Simone Mcknnis raia wa Australia aliyetia saini Septemba mwaka jana kwa mkataba wa miaka mitatu kufundisha mchezo huo alikatiza mkataba wake na kuondoka kurudi kwao Australia kwa kile kilichoelezwa kuwa serikali kushindwa kutimiziwa masharti ya mkataba wake na haswa malipo yake.

Mheshimiwa Spika,
mkakati wa kuagiza makocha kutoka nje, ni sharti uende sambamba na mpango wa kuwapatia ujuzi na uzoefu makocha wetu wa ndani ili pale makocha wa nje wanapoondoka tuweze kuwatumia makocha hao wazalendo kuendeleza michezo nchini.

Kambi ya Upinzani, inashauri kuwa pale ambapo makocha wa kigeni wanapoajiriwa nchini kufundisha timu mbalimbali basi wapewe sharti la kuwa na wasaidizi ambao ni wazawa ili mikataba yao itakapomalizika basi wazawa wabakie na ujuzi na kuweza kuendeleza michezo husika. Aidha, Kambi ya Upinzani inatoa hoja kuwa Bunge hili tukufu liweze kuutambua mchango mkubwa uliofanywa na makocha wazalendo na ikiwezekana waweze kupata nishani ya Bunge kutokana na mchango mkubwa kwenye sekta ya michezo.

Mheshimiwa Spika
, miaka 50 baada ya Uhuru, Tanzania ina uwanja mmoja tu wenye hadhi ya kimataifa ambao ni Uwanja wa Taifa wa Dar es Salaam uliojengwa kwa msaada wakati wa Serikali ya Awamu ya Tatu. Lakini kiwanja hicho sawa na viwanja vingine nchini kimekuwa hakiendeshwi vizuri hata kulitia aibu taifa kwa huduma mbovu, ikiwemo ya kukatika kwa umeme kama ilivyotokea hivi karibuni wakati wa fainali za michuano ya Kombe la Kagame ambalo Tanzania ilikuwa mwenyeji. Mamlaka ya Viwanja vya Michezo ianzishwe. Mheshimiwa Spika, Serikali ianzishe Mamlaka ya Viwanja vya Michezo nchini, na kuipa jukumu la kusimamia na kuendesha viwanja vyote vya michezo vilivyopo. Aidha, Mamlaka hiyo kwa kushirikiana na vyombo mbalimbali vya Serikali, ipewe jukumu la kuhakikisha kila mwaka inajenga Vituo vya Kisasa vya Mazoezi na Hosteli kwa ajili ya Wanamichezo, na angalau kiwanja kimoja kikubwa cha michezo chenye hadhi ya kimataifa inayolingana na hadhi ya Uwanja mpya wa Taifa uliopo Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika,
kwa pendekezo hilo, baada ya miaka tisa, nchi yetu itakuwa na jumla ya viwanja 10 vya kimataifa. Mbali ya kuchochea maendeleo ya michezo nchini na kuajiri Watanzania wengi kutoa huduma mbalimbali, Viwanja hivi pia vitakuza hadhi ya nchi na kuiwezesha nchi kukidhi vigezo vya kuwa Mwenyeji wa michuano mikubwa ya kimataifa kama kuandaa Kombe la Mataifa ya Afrika (CAN).

Mheshimiwa Spika,
kwa hiyosanjari na mpango huo wa Ujenzi wa Viwanja vya Kisasa, Kambi rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuweka lengo la kuhakikisha Tanzania inakuwa Mwenyeji wa Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ligi za Ndani (CHAN) mwaka 2018, na mwenyeji wa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2019. Aidha, Serikali iandae programu na kampeni kabambe ya kuhakikisha timu ya taifa ya mpira wa miguu (Taifa Stars) inaandaliwa vema na kupatiwa mechi nyingi na ngumu za kujipima nguvu, kwa ajili ya kuhakikisha inafuzu kuingia kwenye michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2014 iliyopangwa kufanyika nchini Brazil.

Mheshimiwa Spika, pili viwanja vyote vya michezo, kama Uwanja wa Majimaji Songea, Sheikh Amri Abeid Arusha, Uwanja wa Jamhuri Morogoro, Uwanja wa Jamhuri Dodoma, ule unaoitwa Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza, na viwanja vingine vyote vilivyomilikishwa kwa CCM, virejeshwe Serikalini na viwe chini ya Mamlaka ya Viwanja vya Michezo tunayotaka ianzishwe, ili viboreshwe na kutumika kwa maslahi ya Watanzania wote.

Mheshimiwa Spika,
badala ya kutegemea tu vituo vya michezo vichache vilivyoanzishwa na sekta binafsi, Kambi rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali iandae mpango wa kukuza vipaji vya wanamichezo wadogo kwa kuanzisha vituo vya michezo (Sports Academy) katika kila halmashauri kwa kushirikiana na Mamlaka ya Viwanja vya Michezo tuliyopendekeza ianzishwe.

Mheshimiwa Spika, pamoja na hali mbaya ya sekta ya michezo nchini, bado zipo timu na wapo wachezaji ambao wamekuwa wajitutumua na kufanya vizuri kwenye ushindani wa kimataifa. Kambi rasmi ya Upinzani inachukua fursa hii kuzipongeza timu za soka za Simba na Yanga kwa kufanikiwa kufika fainali ya Kombe la Kagame baada ya kuzitoa timu nyingine za Afrika Mashariki na Kati.

LUGHA YA KISWAHILI NA UTAMADUNI WETU
Mheshimiwa Spika, Kuhusu maendeleo ya Kiswahili, Tanzania inasifika kwa kuongea Kiswahili fasaha, lakini leo ukiingia katika tovuti yeyote duniani, ukiuliza Kiingereza utaambiwa asili yake ni Uingereza, Kifaransa asili yake Ufaransa, Kijapan asili yake Japan, Kijerumani asili yake Ujerumani, Kispanyola asili yake Hispania, lakini unapouliza Kiswahili, wanasema asili yake ni Kenya.

Mheshimiwa Spika
, elimu bora hutolewa kwa lugha ya taifa inavyosemwa na karibu kila mtu, na lugha hiyo hapa kwetu ni lugha ya Kiswahili. Kwa mujibu wa wataalamu na watafiti wa masuala ya lugha na maendeleo(Kwa mfano Prof. Kahigi), ni kwamba hakuna nchi yoyote Duniani ambayo imeendelea kwa lugha ya kukopa. Hivyo basi, Tanzania haiwezi kuendelea kwa kutumia lugha ya Kiingereza tuu katika kutoa elimu kwa vijana wetu kwa hiyo lugha zote mbili zitumike kikamilifu katika kufundishia. Hata hivyo, Kambi ya Upinzani tunapongeza taasisi zote ambazo zimeendelea kukikuza Kiswahili.

Mheshimiwa Spika,
hivi tumeshindwa hata kulinda huu utamaduni wetu wa asili? Kwa sababu hata juhudi ambazo Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) wanazifanya kuendeleza Kiswahili duniani, zinaishia kutolisaidia taifa kwa sababu ya mtazamo wa serikali juu ya lugha ya kufundishia shule za sekondari na vyuo vya juu.

Mheshimiwa Spika
, baada ya kusema hayo, kwa niaba ya kambi ya upinzani, naomba kuwasilisha.
...........................
Joseph O. Mbilinyi (Mb)
Waziri Kivuli Habari, Utamaduni, Michezo na Vijana
11.08.2011

ZAIDI Soma post hii
 
Hivi analitendea haki jimbo lake la mbeya kwa
kuzungumza sana kuhusu wasaniii???????????
 
Wakuu hakuna mtu anaweza kupuuza suala la 'vijana' kwa ujumla jinsi lilivyo timing bomb! We are witnessing it lively from UK! It also happened to Tunisia Mass Revolution na sehemu nyingine nyingi duniani! Mjadala wa bajeti ya Maendeleo ya Habari, Vijana, Michezo na Utamaduni ilipaswa kuwa one of the well attended sessions. Ukitaka kujua umuhimu wake, soma hii hotuba ya Sugu leo bungeni. Nondo.

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI MHE.JOSEPH MBILINYI, (MB) WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO, KUHUSU MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA WA FEDHA 2011/2012

VIAMBATANISHO


Kiambatanisho Na 1
MAPENDEKEZO YA WADAU YA
MUSWADA WA
SHERIA YA HAKI YA KUPATA HABARI, 2011
MPANGILIO WA VIFUNGU
Kifungu Maelezo
SEHEMU YA I
UTANGULIZI
1.Jina fupi na mwanzo wa kutumika 2.Mipaka ya kutumika Sheria 3.Kufuta sheria zinazozuia haki ya kupata habari 4.Malengo 5.Tafsiri
SEHEMU YA II
HAKI YA KUPATA HABARI
6.Haki ya kupata habari 7.Haki ya kupata habari ure 8.Wajibu wa kutoa habari 9.Wajibu wa kuchapisha habari 10.Uteuzi wa maafisa wa habari 11.Ukaguzi wa kumbukumbu 12.Kutojua sheria 13.Kupata habari 14.Kukubali au kukataa kutoa habari 15.Uhamisho wa ombi la kupata habari 16.Mamlaka ya kutoa habari 17.Kukataa kutoa habari
SEHEMU YA III
KINGA YA USIRI
18.Habari zenye kinga ya usiri 19.Kupewa habari zenye kinga ya usiri 20.Kizuizi kwa kinga ya usiri
SEHEMU YA IV
KUUNDWA KWA TUME YA HABARI
21.Kuundwa kwa Tume 22.Kazi za Tume 23.Wajumbe wa Tume 24.Kamati ya Uteuzi 25.Sifa za kuteuliwa kuwa mjumbe wa Tume 26.Ukomo wa kuwa Kamishina 27.Kuondolewa kwenye Tume 28.Mamlaka ya Tume 29.Mashitaka dhidi ya Wajumbe wa Tume 30.Uchunguzi na kusikiliza mashauri 31.Kufika mbele ya Tume 32.Masjala ya Taifa ya Habari
SEHEMU YA V
RUFAA DHIDI YA KUNYIMWA HABARI
33.Utaratibu wa rufaa za ndani 34.Haki ya rufaa kwenye Tume ya Habari 35.Mamlaka ya Mahakama Kuu 36.Wajibu wa kuthibitisha ushahidi
SEHEMU YA VI
KINGA, MAKOSA NA ADHABU
37.Utoaji wa habari kwa nia njema 38.Kinga kwa wapiga filimbi 39.Udanganyifu na upotoshaji wa habari 40.Hifadhi na uwekaji wa kumbukumbu 41.Kuharibu habari kinyume cha sheria
SEHEMU YA VII
MENGINEYO
42.Kuanzishwa kwa Jukwaa la Wadau wa Habari 43.Sheria ya Vyombo vya Habari 44.Mamlaka ya kutunga kanuni
JEDWALI





SHERIA YA HAKI YA KUPATA HABARI, 2011
MUSWADA
wa
Sheria kuhusu haki ya kupata habari, utawala bora, wajibu wa taasisi binafsi na za umma kutoa habari, haki ya kupata habari na kuhusu mambo mengine yahusianayo na habari. Imetungwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
[…………………………….]
SEHEMU YA I
UTANGULIZI
Jina fupi na kuanza kutumika 1. (1) Sheria hii itaitwa Sheria ya Haki ya Kupata Habari, 2011 na itaanza kutumika ndani ya siku tisini baada ya kutungwa kwenye tarehe itakayopangwa na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali na Waziri anayehusika na mambo ya habari.
(2) Neno ‘kutungwa’ kwa mujibu wa kifungu hiki linamaanisha hatua ya muswada kupitishwa na Bunge na kukubaliwa na Rais.
Mipaka ya kutumika Sheria 2. Sheria hii itatumika Tanzania Bara.
Kufuta sheria zinazozuia haki ya kupata habari 3. (1) Bila kuathiri vifungu vingine vya Sheria hii, kifungu au sheria yoyote inayozuia upatikanaji wa habari au kuweka kinga ya usiri kwenye habari zinazoshikiliwa na taasisi ya umma au binafsi vimefutwa.
(2) Bila kuathiri Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, vifungu vya Sheria hii vitakuwa na nguvu dhidi ya vifungu vya sheria nyingine yoyote inayohusu haki ya kupata habari.
(3) Hakuna kifungu katika Sheria hii kinachozuia kutolewa kwa habari na taasisi binafsi au ya umma hata kama habari hizo zimewekewa kinga ya usiri ilmradi mamlaka husika inayo mamlaka ya kisheria kufanya hivyo.
Malengo 4. Malengo makuu ya Sheria hii yatakuwa :
(a)kutekeleza haki ya kikatiba ya kupata habari zinazoshikiliwa na taasisi za umma na binafsi kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 kwa kila namna inayowezekana;
(b) kuimarisha utawala wa kidemokrasia kwa kuweka masharti yanayoziwajibisha taasisi za umma na binafsi kutoa habari;
(c) kuweka utaratibu wa kisheria wa kuwawezesha wanajamii kupata habari zilizo mikononi mwa taasisi za umma na binafsi bila kucheleweshwa na kwa gharama nafuu;
(d) kuweka utaratibu wa kisheria wa kuwawezesha watendaji wa taasisi za umma na binafsi kutekeleza wajibu wao wa kukuza utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu na haki za kijamii; (e) kuweka utaratibu wa kisheria unaoziwajibisha taasisi binafsi na za umma kuchapisha mara kwa mara habari zilizonazo;
(f) kuunda masjala ya taifa ya habari zote zinazoshikiliwa na taasisi binafsi na za umma; na (g) kukuza na kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari nchini.
Tafsiri 5.Katika Sheria hii, isipokuwa pale ambapo imeelezwa wazi kinyume cha maana iliyoainishwa hapa-
“kupata habari” inajumuisha kukagua shughuli za habari, kuandika kumbukumbu na nukuu, kupata nakala halisi au kuchukua sampuli za vitu;
"Tume” maana yake ni Tume ya Habari iliyoundwa kwa mujibu wa kifungu cha 21 cha Sheria hii;
"Kamati” maana yake ni Kamati ya uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Habari kwa mujibu wa kifungu cha 24cha Sheria hii;
"Kamishna” maana yake ni mjumbe wa Tume ya Habari iliyoundwa kwa mujibu wa kifungu cha 21 cha Sheria hii;
"Katibu Mtendaji” maana yake ni mtendaji mkuu wa Sekretariati ya Tume ya Habari aliyeajiriwa kwa mujibu wa aya ya 4 (1) na (6) ya Jedwali la Sheria hii;
"habari zenye kinga ya usiri” maana yake ni habari ambazo kwa mujibu wa kifungu cha 18(1) cha Sheria hii imekatazwa zisitangazwe; “habari” maana yake ni elimu iliyopatikana kutokana na kujifunza, ujuzi, uchunguzi au mafunzo; uelewa wa matukio ambao umepatikana au kupokelewa kwa kupeana taarifa, ghani za kishushushu au taarifa za habari; mkusanyiko wa chembechembe za mambo ya kweli na takwimu; takwimu zilizoandaliwa, kuhifadhiwa au takwimu zinazotumwa na kuhifadhiwa kwenye kompyuta au kuhifadhiwa kwa mfumo wowote wa kielektroniki; mfumo wa kimahesabu wa kuhakiki ukweli katika matokeo ya majaribio; mada yoyote iliyo katika hali au umbile lolote ikijumuisha kumbukumbu, makabrasha, maandiko yaliyohifadhiwa kwenye mafaili, dondoo, barua pepe, maoni, ushauri, taarifa kwa waandishi wa habari, sekula, amri, vitabu vya kumbukumbu za safari za vyombo vya usafiri, mikataba, ripoti, mada za kitaaluma, sampuli, modeli, takwimu, mada yoyote iliyohifadhiwa kwa njia ya elektroniki na habari zozote zinazohusu taasisi binafsi au ya umma;
"afisa wa habari” maana yake ni afisa aliyeteuliwa kushughulikia habari katika taasisi binafsi au ya umma, na kwa mujibu wa sheria hii;
"Waziri” maana yake ni Waziri katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwenye dhamana ya mambo ya habari;
”afisa” maana yake ni mtu yeyote aliye mwajiriwa wa taasisi binafsi au ya umma bila kujali aina ya ajira yake kuwa ni ya muda mfupi au ya kudumu na inamaanisha pia mkuu wa taasisi hiyo;
“mtu” maana yake ni binadamu, shirika au taasisi kwa mujibu wa mtu kisheria, na inajumuisha taasisi binafsi, taasisi za umma, taasisi zisizo za kiserikali, taasisi za kijamii na taasisi za kidini;
"iliyoainishwa kisheria” maana yake ni jambo lolole lililoainishwa kisheria kwa kanuni zilizotungwa kwa mujibu wa Sheria hii;
"taasisi binafsi" maana yake ni mtu binafsi au binadamu na inajumuisha kampuni, shirika au asasi zisizo za kiserikali iliyokwishafanya au inayofanya shughuli au biashara nchini Tanzania lakini haijumuishi taasisi ya umma;

"taasisi za umma" inajumuisha-
(a)Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au kamati yoyote ya Bunge; (b)Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na idara zilizoundwa na Rais;
(c)Baraza la Mawaziri lililoundwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977; (d)Wizara, idara, kitengo cha Wizara au ofisi binafsi ya Waziri popote ilipo;
(e)mamlaka ya kijiji, mtaa, kata, miji au jiji; (f)asasi za Serikali, idara na vitengo vinavyotekeleza majukumu ya umma;
(g)mahakama; (h)shirika lililoundwa na Sheria ya Bunge, shirika au kampuni ya umma; na (i)taasisi yoyote nyingine au kitengo kilichoundwa na Sheria hii, kanuni zilizotungwa chini ya Sheria hii au sheria nyingine;
"Waziri mwenye dhamana" maana yake ni Waziri ambaye mamlaka au dhamana juu ya jambo fulani imekabidhiwa kwake.
SEHEMU YA II
HAKI YA KUPATA HABARI
Haki ya kupata habari 6. (1) Kila mtu ana haki ya kupata habari na anao uhuru wa kutafuta, kupokea na kutuma habari kwa njia yoyote ikiwa ni pamoja na vyombo vya habari bila kujali mipaka ya nchi.
(2) Vyombo vya habari vya aina yoyote ile ni huru na vitakuwa na haki ya kutafuta, kupata na kutangaza taarifa na habari zinazoshikiliwa na taasisi za binafsi na za umma bila vizuizi.
Haki ya kupata habari bure 7.Haki ya kupata habari ni haki ya binadamu kwa hivyo habari zitatolewa bure bila kujali mfumo wa utoaji wake.
Wajibu wa kutoa habari 8.(1) Kwa mujibu wa masharti ya sheria hii, taasisi binafsi na za umma zinawajibika kutoa habari kwa kila mtu kwa haraka kama itakavyowezekana.
(2)Ni wajibu wa kila taasisi ya umma au binafsi yenye kushikilia habari kutoa habari hizo mara kwa mara katika vipindi vilivyopangwa bila kikwazo chochote.
(3)Utoaji wa habari wa mara kwa mara utafanywa kwa njia zifuatazo:
(a)mikutano ya hadhara na mikusanyiko ya watu iliyopangwa pamoja na programu za elimu ya umma kwenye vyombo vya habari;
(b)matangazo kupitia vyombo vya habari nchini; (c)kuchapwa katika Gazeti la Serikali;
(d)kuchapwa katika Tovuti ya Serikali pamoja na tovuti ya taasisi binafsi au ya umma inayohusika; (e)mikutano ya mara kwa mara ya waandishi wa habari na watendaji wa vyonbo vya habari katika eneo husika; na (f)machapisho ya mara kwa mara yanayowafikia wanajamii kutoka taasisi husika ya binafsi au ya umma:
Ilmradi kwamba njia hizi sio njia pekee, na hivyo habari zinaweza kutolewa au kufichuliwa kwa njia zaidi ya moja.
(4) Nakala ya kila habari itakayochapishwa na taasisi binafsi au ya umma itapelekwa kwa Tume ya Habari kuhifadhiwa kwa kumbukumbu bila kufanyiwa badiliko lolote na itahifadhiwa katika hali yake ya asili.
Wajibu wa kuchapi-sha habari 9. (1) Ndani ya miezi kumi na mbili baada ya Sheria hii kuanza kufanya kazi au baada ya kuundwa kwa taasisi ya umma, na baada ya hapo kila mwaka, kila taasisi ya umma itawajibika kuchapisha kwa lugha ya Kiswahili na kusambaza kwa umma kadri inavyowezekana chapisho lenye habari zifuatazo:
(a)anwani, simu, nambari ya faksi, na anwani za barua pepe za maafisa wake wote wa habari, kama zipo;
(b)maelezo ya kina kuhusu jinsi wanajamii wanavyoweza kupata habari zinazoshikiliwa na taasisi hiyo ya umma;
(c)maelezo kuhusu habari na vichwa vya habari zote zinazoshikiliwa na taasisi hiyo ya umma;
(d) orodha ya habari zote zinazoshikiliwa na taasisi ya umma ambazo mtu anaweza kuzipata bila kuwajibika kuomba kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na sheria hii;
(e)regista ya habari zote zilizopokelewa na taasisi hiyo ya umma ikielezwa wazi habari hizo zinahusu jambo gani na maudhui yake;
(f)maelezo kuhusu njia za malalamiko zilizopo kwa mtu aliyenyimwa haki zake kutokana na taasisi ya umma kushindwa kutekeleza wajibu wake kwa mujibu wa vipengele vya sheria hii; na
(g)maelezo mengine yoyote kama yalivyoainishwa kwenye kanuni za sheria hii kwa minajili ya kuhimiza upatikanaji wa habari na taarifa ambazo zinashikiliwa na taasisi hiyo ya umma.
(2)Kila taasisi ya umma itachapisha mara kwa mara, na si chini ya mara moja kwa mwaka, na kwa namna ambayo kila mtu anaweza kupata, habari zote muhimu ambazo zimepatikana ukiacha zile zilizochapishwa kwenye chapisho lililotajwa kwenye kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki na chapisho hilo la nyongeza litaainisha habari zote zikiwa ni pamoja na habari zifuatazo:
(a)maelezo kuhusu muundo, malengo, wajibu na mambo ya fedha ya taasisi; (b)maelezo ya kina kuhusu huduma na kazi za taasisi kwa jamii;
(c)maelezo kuhusu njia za moja kwa moja za kufanya maombi na kuleta malalamiko kwa wanajamii pale taasisi inaposhindwa kutekeleza wajibu wake na maelezo kuhusu maombi na malalamiko ya wanajamii yaliyokwishaletwa na kufanyiwa kazi na taasisi; (d)chapisho linaloainisha kwa lugha rahisi utaratibu wa uwekaji na uhifadhi wa habari za taasisi, fomu mbalimbali za taasisi ikiwa ni pamoja na utaratibu wa kuomba habari za taasisi;
(e)maelezo kuhusu mamlaka na wajibu wa maafisa wakuu mbalimbali wa taasisi na taratibu za ufanyaji wa maamuzi ndani ya taasisi; (f)kanuni zozote zile, sera, maamuzi, miongozo na kitabu cha uendeshaji wa shughuli za taasisi;
(g)maudhui ya maamuzi mbalimbali ya taasisi na sera zinazotumika ambazo huigusa jamii ikiwa ni pamoja na sababu ya maamuzi na sera hizo, ufafanuzi wake na makabrasha yanayoeleza chanzo na misingi ya maamuzi na sera hizo; na (h)utaratibu wowote au kanuni zinazowawezesha wanajamii kutoa hoja au maelezo yao kwa taasisi kwa nia ya kushawishi mabadiliko au maboresho ya sera au uendeshaji wa taasisi husika.
Uteuzi wa maafisa wa habari 10. (1) Kwa madhumuni ya Sheria hii, kila taasisi binafsi na ya umma itateua afisa au maafisa wa kutosha ambao watashughulikia utoaji wa habari kwa watu wanaoomba kupewa habari zinazoshikiliwa na taasisi hiyo.
(2)Maafisa wanaohusika na habari, pamoja na shughuli nyingine walizopewa kwa mujibu wa sheria hii, watakuwa pia na wajibu wa kufanya mambo yafuatayo:
(a)kuendeleza ndani ya taasisi husika taratibu za utendaji bora wa kazi hasa kuhusiana na uwekaji na uhifadhi wa kumbukumbu na pia uteketezaji wa kumbukumbu zilizopitwa na wakati;
(b)kutoa habari zinazoshikiliwa na taasisi walimoajiriwa;
(c)kupokea na kushughulikia maombi ya habari, kuwasaidia waombaji wa habari kuzitambua na kuzipata habari wanazozihitaji; na
(d)kupokea na kushughulikia malalamiko kuhusu utendaji kazi wa taasisi husika kuhusu mambo ya utoaji wa habari kwa mujibu wa Sheria hii.
Ukaguzi wa kumbukumbu 11.(1) Tume ya Habari kwa ushauriano na Jukwaa la Wadau wa Habari itatunga kanuni zitakazoainisha aina nyingine za habari ambazo taasisi binafsi na za umma zinawajibika kuchapisha kwa mujibu wa kifungu cha tisa cha sheria hii na itafafanua haki, manufaa, adhabu na hasara nyingine ambazo mtu anaweza kupata au kukosa.
(2)Kanuni zitakazotungwa kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki zitaweka masharti kwa taasisi binafsi na za umma kuelimisha jamii kuhusu uwepo wa machapisho ya habari yaliyotajwa kwenye Sheria hii.

(3)Tume ya Habari itafanya ukaguzi mara kwa mara, angalau mara moja katika kila miezi kumi na mbili, ili kuhakikisha kwamba taasisi binafsi na za umma zinazingatia masharti ya kifungu cha 8 na cha 9 cha Sheria hii.
Kutokujua sheria 12. Kama habari zinatakiwa kuchapishwa ili kuwafikia wanajamii kwa mujibu wa sheria hii kwa kuwa ni habari kuhusu kanuni, mwongozo au mila ya utendaji wa jambo ambalo ni jukumu la taasisi ya umma na haikuchapishwa na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali kama iliyoagizwa kwenye kifungu hiki, basi mwanajamii atakayekosea kutenda kwa kuwa hakujua kanuni, mwongozo au mila husika hatawajibishwa au kunyimwa haki, kama hali hiyo ingeepukwa kama uchapishaji na tangazo katika Gazeti la Serikali ungekuwa umefanyika.
Kupata habari 13. (1) Mtu anayetaka kupata habari kutoka taasisi binafsi au ya umma anaweza kufanya hivyo kwa kuwasilisha ombi kwa njia ya mdomo, maandishi au elektroniki kwa taasisi husika.
(2) Afisa anayeshughulikia habari, ambaye ombi la mdomo limetumwa kwake, ataliainisha ombi hilo kimaandishi.
(3)Itakuwa ni wajibu wa afisa habari wa taasisi binafsi au ya umma kumsaidia mwombaji kutambua habari anayoomba au kumpatia mwombaji fununu anazopashwa kuzifahamu ili kumwezesha kutambua habari anazozitaka.
(4)Taasisi ya umma au binafsi iliyoombwa kutoa habari inayo haki ya kumwarifu mtu wa tatu ambaye haki au maslahi yake yanaguswa na utoaji wa habari zilizoombwa.
(5)Mwombaji anayo haki ya kueleza mfumo au njia ya kupatiwa habari, kwa njia ambazo zaweza kutumika kutoa habari ambazo ni pamoja na njia ya mdomo, kuona na kusoma, kupewa nakala kwa maandishi, kanda ya sauti, nakala ya elektroniki au kanda ya video, au njia yoyote nyingine.
(6)Pale ambapo mwombaji ameomba apewe habari kwa njia fulani, basi atapewa habari kwa njia hiyo isipokuwa kama utoaji wa habari kwa njia hiyo utaathiri ubora wa habari au kuingilia haki miliki ya mtu binafsi.
(7)Itakuwa ni wajibu wa afisa anayeshughulikia habari, aliyekabidhiwa ombi la habari, kumsaidia mwombaji ambaye: hajui kusoma, au ni mlemavu, au ni mdhaifu wa mwili; ili kumwezesha kuwasilisha ombi lake kwa mujibu wa sheria hii.


(8)Afisa wa habari akishapokea ombi la habari kama ilivyoainishwa kwenye kifungu kidogo (5) cha kifungu hiki ataainisha ombi hilo la mdomo kimaandishi kwa mujibu wa sheria hii na kumpatia mwombaji nakala yake pamoja ya risiti papo kwa hapo. (9)Mwombaji hatatakiwa kwa namna yoyote ile kueleza sababu ya ombi au matumizi ya habari anazoziomba.
Kukubali au kukataa kutoa habari

14.(1) Ombi la kupewa habari lazima likubaliwe au kukataliwa ndani ya siku tatu za kazi au haraka kama inavyowezekana ilmradi isitokee kwamba uamuzi ukacheleweshwa zaidi ya siku saba tangu ombi kupokelewa.
(2)Pale ambapo ombi la kupewa habari limekataliwa, mwombaji atapewa taarifa ya uamuzi wa kukataliwa au kuahirishwa kwa siku ya kupewa habari kwa maandishi, uamuzi wa kukataliwa utaje vifungu vya sheria vilivyotumika katika kutoa uamuzi wa kukataa ombi na utaje pia haki ya mwombaji kukata rufaa.

(3)Kama taasisi itashindwa kutoa uamuzi wa kutoa au kutotoa habari ndani ya muda uliowekwa na kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki itachukuliwa kuwa taasisi hiyo imekataa ombi la kutoa habari bila sababu ya maana na mwombaji atakuwa na haki ya kukata rufaa. (4) Kwenye rufaa, isipokuwa kama itathibitishwa vinginevyo, itachukuliwa kwamba taasisi husika haikuwa na sababu ya maana ya kukataa kutoa habari.

(5)Mtu ambaye amepewa taarifa ya kukataliwa kupewa habari kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (2) cha kifungu hiki anaweza kukata rufaa kwenye chombo kilichoteuliwa na taasisi husika kwa mujibu wa kifungu cha 33 (1) cha Sheria hii;


(6)Kushindwa kwa taasisi ya umma au binafsi kutoa habari kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (3) cha kifungu hiki kutaipa Tume haki ya kutoa adhabu ya faini isiyozidi shilingi laki tano au kifungo kisichozidi miezi sita au vyote kama moja ya nafuu zitakazotolewa na Tume kwenye rufaa; (7)Hakuna ombi la kupata habari litakalokataliwa kwa sababu kwamba halitoshelezi.
Uhamisho wa ombi la kupata habari 15.(1) Pale ambapo ombi la habari limepelekwa kwa taasisi ya umma au binafsi ambayo siyo yenye habari husika, basi taasisi hiyo italihamisha ombi hilo kwenye taasisi inayohusika na itamuarifu mwombaji kuhusu uhamisho wa ombi lake kwenda kwenye taasisi husika.
(2)Pale ambapo ombi la habari limehamishiwa kwenye taasisi nyingine ya umma au binafsi kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki, basi itachukuliwa kuwa ombi hilo liliwasilishwa kwenye taasisi hiyo nyingine ilmradi uhamisho utafanywa haraka baada ya ombi kupokelewa na kwa vyovyote vile muda huo usizidi siku tatu za kazi tangu ombi kupokelewa.
Mamlaka ya kutoa habari 16. Uamuzi kuhusu ombi la habari kutoka kwenye taasisi ya umma au binafsi utatolewa na afisa wa habari wa taasisi husika isipokuwa kama Waziri, Afisa Mkuu wa Shirika au afisa mwingine yeyote ndiye mhusika mwenye mamlaka pekee ya kutoa habari zilizoombwa.
Kukataa ombi la kupata habari 17.(1) Pale ambapo ombi la habari kutoka taasisi binafsi au ya umma limekataliwa kwa msingi kuwa mwombaji hana haki ya kupata habari husika, taasisi husika itatoa taarifa kwa maandishi kuhusu uamuzi huo na taarifa hiyo itataja mambo yafuatayo:
(a)itaeleza uamuzi uliofikiwa kwenye kila hoja ya ombi na kuweka wazi misingi na sababu ya uamuzi;
(b)itataja jina na cheo cha afisa wa taasisi husika aliyetoa uamuzi;
(c)pale ambapo uamuzi unahusu kunyimwa habari zenye kinga ya usiri kwa mujibu wa Sheria hii, uamuzi huo utaeleza kwa nini habari hizo zina kinga ya usiri;
(d)pale ambapo uamuzi ni kwamba habari husika hazijawahi kuwepo, basi utaelezea kuwa juhudi za kina zilifanywa kuzipata bila mafanikio; na (e)itamwarifu mwombaji kuhusu haki yake ya kukata rufaa kwenye Tume ya Habari.
(2)Litakuwa kosa la jinai litakaloadhibiwa kwa faini isiyozidi shilingi laki tano au kifungo kisichozidi miezi sita, au vyote viwili, kwa afisa yeyote wa taasisi binafsi au ya umma kuvunja masharti ya kifungu cha 17(1) cha Sheria hii.
[h=5][/h] [h=5]SEHEMU YA IV[/h] [h=5]KINGA YA USIRI[/h]
Habari zenye kinga ya usiri 18.(1) Habari zifuatazo zimepewa kinga ya usiri, hivyo ni siri kwa watu wote isipokuwa watungaji wake, isipokuwa pale vifungu vya Sheria hii au sheria nyingine yoyote vinaamuru vinginevyo, yaani-
(a)kama kutolewa kwake kutaathiri ulinzi na usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au mahusiano yake na nchi ya nje;
(b)kama maudhui yake ni yale yaliyowekewa kinga ya usiri ili zizitolewe katika mashauri yoyote mahakamani kwa msingi wa hifadhi ya siri za kitaalamu;
(c)kama habari zinahusu utafiti unaofanyika au ambao uko mbioni kufanyika au ambao unafanywa kwa niaba ya mtu wa tatu, na ikiwa kama kutolewa kwa habari hizo kutaathiri utafiti huo, kumfichua mtu wa tatu au kumfichua mtu ambaye anafanyiwa utafiti na kumuathiri vibaya;
(d)kama kutolewa kwa habari kutasababisha mambo yafuatayo:
(a)dharau kwa mahakama;
(b)kuvunja kinga na haki za Bunge (c)kukwamisha uzuiaji au ufichuaji wa vitendo vya jinai; (d)kukwamisha utekelezaji wa haki;
(e)kusaidia utendaji wa kosa lolote la jinai; (f)kuathiri vibaya maslahi halali ya dola au mtu binafsi;
(g)kuvunja haki ya faragha ya mtu binafsi; (h)kuhatarisha usalama wa maisha ya mtu aliyetajwa katika habari zilizoombwa; na
(i)kuvunja haki miliki na haki za wagunduzi au haki zingine za aina hiyo zilizomo katika habari iliyoombwa.
(2)Kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki hakihusu habari ambazo zina taarifa ambazo ni takwimu, maelezo ya kitaalamu, taarifa za kisayansi au taarifa ambazo zimeishatolewa kwa umma au ni za uchambuzi wa mtaalamu aliyetoa maoni yake ya kitaalamu.
Kupewa habari zenye kinga ya usiri 19.(1) Bila ya kuathiri masharti ya kifungu 18(1) cha sheria hii na sheria yoyote nyingine, taasisi binafsi na ya umma zitatoa habari zenye kinga ya usiri pale ambapo kwa kuangalia mazingira ya habari zilizoombwa, ni kwa maslahi na faida ya umma kutoa habari husika licha ya athari au hasara itakayosababishwa na utoaji huo kwa mtu binafsi au kwa kikundi cha watu.
(2)Tume ya Habari itakuwa na mamlaka ya kuamua kama habari zina kinga ya usiri au la na kama kulingana na mazingira ya shauri lenyewe, zenye kinga ya usiri zinaweza kutolewa kwa maslahi ya umma.
(3)Msingi utakaotumika kuamua kama habari zenye kinga ya usiri zitolewe au la ni kama utoaji au kutotoa ni kwa maslahi ya umma, na msingi huo hautatumika vibaya kukataa habari zinazoshikiliwa na taasisi ya umma au binafsi zisitolewe.
(4)Katika kifungu hiki “maslahi ya umma” ni pamoja na haki ya jamii kujua, kufichua rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma, kufichua njama za kutenda makosa ya jinai, kulinda usalama wa watu binafsi, kulinda mazingira na uhai, haki ya mwenendo wa haki wa mashauri mahakamani na ufichuaji wa vitendo vya kifisadi vinavyomomonyoa imani ya umma kwa mfumo wa kidemokrasia wa utawala.
(5)Afisa wa habari au mwombaji habari anaweza kupeleka shauri lolote kwa Tume ya Habari katika eneo ilipo taasisi ya umma au binafsi kwa uamuzi kama habari zilizoombwa zina kinga ya usiri au la na kama zinaweza kutolewa kwa mwombaji.
(6)Mtu yeyote ambaye hakuridhishwa na uamuzi wa Tume ya Habari ana haki ya kukata rufaa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kizuizi kwa kinga ya usiri

20.(1) Masharti ya kifungu cha 18(1) ya Sheria hii yatatumika pale tu ambapo athari inayolindwa na kinga ya usiri itatokea au inatazamiwa kutokea wakati au baada ya ombi la habari kuamuliwa.
(2)Habari zenye kinga ya usiri zitatolewa baada ya kupita miaka kumi tangu kuwepo kwake, ilmradi kwamba masharti ya kifungu hiki kidogo hayatahusu habari zilizowekewa kinga na kifungu cha 18(1) (a).
SEHEMU YA IV
KUUNDWA KWA TUME YA HABARI
Kuundwa kwa Tume 21.(1) Inaundwa Tume huru ya Habari ambayo itakuwa na mamlaka ya kushughulikia masuala yote yanayohusu haki na uhuru wa kupata habari kwa mujibu wa Sheria hii.
(2)Katika utekelezaji wa wajibu wake chini ya Sheria hii, Tume haitaingiliwa na mtu yeyote isipokuwa kwa amri ya Mahakama Kuu na itatekeleza majukumu yake chini ya mwavuli wa Bunge.
(3)Tume itakuwa: (a)ni shirika lenye uhai wa kudumu kwa mujibu wa sheria; (b)na mamlaka ya kushitaki au kushitakiwa kwa jina lake yenyewe; na (c) na mamlaka ya kuhodhi, kumiliki, kuuza na kununua mali zinazohamishika na zisizohamishika kwa jina lake na kwa mujibu wa sheria. (4) Jedwali la Sheria hii litaelekeza utaratibu wa mwenendo wa shughuli, mahesabu, taarifa ya mwaka, ajira na ujira wa wajumbe na wa watumishi wa Tume.
Kazi za Tume 22.(1) Kazi za Tume ya Habari zitakuwa kama ifuatavyo:
(a)kuanzisha na kutunza Masjala ya Habari ya Taifa pamoja na masjala ndogo za habari ili kurahisisha upatikanaji wa habari wakati wowote kadri Tume itakavyoona inafaa; (b)kutunga kanuni za kulazimisha taasisi za umma na binafsi kuwasilisha habari zake kwenye Tume;
(c)kutoa habari zilizowasilishwa na taasisi za umma na binafsi kwa jamii kwa mujibu wa sheria hii; (d)kupokea malalamiko kutoka kwa jamii kuhusu kunyimwa habari na taasisi za umma au binafsi;
(e)kufuatilia na kufanya tafiti kuhusu vitendo vinavyoathiri uhuru wa habari; (f)kuishauri Serikali na taasisi za umma na za binafsi kuhusu masuala ya haki ya kupata habari pamoja na mifano ya kuigwa kwenye utoaji wa habari kwa umma;
(g)kuongoza mchakato wa Serikali katika kuridhia mikataba ya kimataifa inayohusu uhuru wa habari; (h)kuongoza usimamizi na uimarishwaji wa misingi ya uhuru wa habari;
(i)kuchapisha vijarida vya mwongozo na mifano bora kuhusu wajibu wa taasisi za umma na binafsi kutoa habari kwa mujibu wa sheria hii; (j)kutengeneza na kufanyia marekebisho ya mara kwa mara kwa ushirikiano na Jukwaa la Wadau wa Habari, mwongozo kuhusu kanuni za utendaji kazi katika kuhifadhi, kusimamia na kuteketeza kumbukumbu na hati katika Masjala ya Taifa ya Habari, pamoja na kuhamishwa kwa kumbukumbu kupelekwa kwenye hifadhi ya kumbukumbu za Taifa;
(k)kuandaa mafunzo kwa ajili ya maafisa habari na maafisa wengine wa umma kuhusu mwenendo, kanuni na taratibu za kufuatwa katika kutekeleza Sheria hii; (l)kushirikiana na Jukwaa la Wadau wa Habari kuendesha elimu ya uraia ili kuiwezesha jamii kuielewa sheria ya haki ya kupata habari;
(m)kushauriana na taasisi za umma na binafsi, vyombo vya habari na umma kwa ujumla kuhusu matatizo yanayotokana na utekelezaji wa sheria hii; (n) kupokea ushauri, kushauriana au kupokea na kutathmini mapendekezo ya Jukwaa la Wadau wa Habari; na (o)kutekeleza majukumu mengine kadri itakavyoelekezwa na Bunge.
(2)Tume ya habari itaanzisha na kusimamia, kadri itakavyoona inafaa, utaratibu wa kushauriana na kushirikiana na Mamlaka ya Kudhibiti Mawasiliano (TCRA), Jukwaa la Wadau wa Habari pamoja na asasi nyingine yoyote iliyoanzishwa na sheria yoyote ikiwa na kazi zinazofanana na zile zilizotajwa katika kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki.
Wajumbe wa Tume 23.(1) Tume ya Habari itakuwa na wajumbe tisa, wote wakiwa na utaalamu, kwa mujibu wa elimu yao au uzoefu, kwenye masuala ya habari, sheria, jinsia, vyombo vya habari, au fani nyingine zinazofanana na hizo, ambao wanafahamika kuwa watu wenye uadilifu, heshima, nidhamu na umahiri wa hali ya juu.
(2)Tume inaweza, kumhusisha au kuomba ushauri wa mtu yeyote aliyebobea kwenye fani fulani katika utendaji kazi yake isipokuwa kazi ya kusikiliza na kuamua mashauri, ilmradi mtu huyo asiwe kamishna wa Tume. (3)Tume yaweza kuteua na kukasimu mamlaka yake ya kusikiliza na kuamua mashauri kwa mujibu wa Sheria hii kwa mtu yeyote kadri itakavyoona inafaa, ilmradi mtu huyo awe mwenye sifa za kuteuliwa kuwa kamishna wa Tume. (4)Mtu atakayeteuliwa chini ya kifungu kidogo cha (2) na (3) cha kifungu hiki, atalipwa marupurupu kadri itakavyoamuliwa na Tume.
Kamati ya Uteuzi 24.(1) Kutakuwa na Kamati ya Uteuzi ambayo itakuwa na wajumbe wafuatao:
(a)mwakilishi mmoja wa Wizara inayoshughulikia mambo ya katiba na sheria;
(b)mwakilishi mmoja wa baraza huru la habari lilioundwa na waandishi wa habari; (c)mwakilishi mmoja wa shirikisho la wamiliki wa vyombo vya habari;
(d)mwakilishi mmoja kutoka katika vyama vya kitaalamu vya waandishi wa habari; (e)mwakilishi mmoja kutoka kwenye vyuo vikuu vinavyotoa elimu ya uandishi wa habari;
(f)mwakilishi mmoja wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora; (g)mwakilishi mmoja kutoka chama cha kitaalamu cha wanasheria cha Tanganyika (TLS); na (h)mwakilishi mmoja kutoka kwenye asasi zisizokuwa za kiserikali zinazoshughulikia haki za binadamu.
(2)Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi atachaguliwa na wajumbe waliotajwa kwenye kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki.
(3)Waziri kwa kushirikiana na Jukwaa la Wadau wa Habari atatunga kanuni kuhusu uteuzi wa wajumbe wa Kamati ya Uteuzi na taratibu zitakazotumika kuwateua wajumbe wa Tume ya Habari. (4)Kamati ya Uteuzi itapeleka majina ya wajumbe tisa wa Tume ya Habari, likiwamo jina la mwenyekiti wa Tume, kwa Waziri ambaye atayawasilisha majina hayo bungeni kwa taarifa.
(5)Kamati ya Uteuzi itahakikisha wajumbe wa Tume ni wawakilishi wa wadau. (6)Kamati ya Uteuzi ni lazima izingatie uwiano wa kijinsia katika uteuzi wa wajumbe wa Tume.
(7)Kwa mujibu wa kanuni zilizotungwa chini ya kifungu cha 24 (3) cha Sheria hii, Kamati ya uteuzi itaundwa ndani ya siku tisini baada ya kuanza kutumika sheria hii na itadumu kwa miaka mitano ilmradi hakuna mjumbe wa kamati hii atakayeteuliwa kwa zaidi ya vipindi viwili vya utumishi.
Sifa za kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Tume 25.(1) Mtu hatateuliwa kuwa mjumbe wa Tume ya Habari iwapo:
(a)siyo raia wa Tanzania;
(b)hajafikia umri wa miaka kumi na nane; (c)ameajiriwa katika utumishi wa umma au katika idara yoyote ya Serikali;
(d)ni kiongozi wa Taifa au mwajiriwa wa chama cha siasa au anashikilia wadhifa wowote wa kuchaguliwa katika Serikali Kuu au Serikali za Mitaa; (e)ni mmiliki au mwajiriwa wa vyombo vya habari;
(f)ni muflisi kwa mujibu wa sheria; na (g)ametiwa hatiani na mahakama kwa makosa ya rushwa, makosa ya kutokuwa mwaminifu au makosa ya uvunjaji wa maadili.
(2)Kamati ya Uteuzi inaweza kuteua mtu ambaye, isipokuwa kwa masharti ya kifungu cha 25 (b), (c) na (d) cha Sheria hii, angekuwa na sifa za kuwa Kamishna na kumpa mtu huyo fursa ya kuondokana na sifa zinazopingana na kuteuliwa kwake ilmradi kipindi cha kuondokana na sifa hizo kisizidi siku tisini tangu kuteuliwa kwake. (3)Mtu yeyote atakayeteuliwa kuwa kamishna wa Tume kwa mujibu wa sheria hii atakula kiapo, mbele ya Jaji Mkuu, cha uaminifu na utunzaji wa siri za Tume au taarifa za siri anazozipata kutokana na utendaji wa kazi zake kwenye Tume.
Ukomo wa kuwa Kamishna 26. Wajumbe wa Tume ya Habari watashika wadhifa huo kwa muda wa miaka mitano mfululizo na wanaweza kuteuliwa tena kwa kipindi cha mwisho cha miaka mitano.
Kuondole-wa kwenye Tume 27.(1) Mjumbe wa Tume ya Habari ataacha kuwa mjumbe ikiwa:
(a)atajiuzulu;
(b)hatahudhuria vikao vitatu mfululizo bila sababu yoyote ya msingi; (c)atakuwa kichaa;
(d)atatenda kosa la ukiukaji wa majukumu yake chini ya sheria hii; (e)akifariki;
(f)muda wa kuwa mjumbe ukimalizika kwa mujibu wa Sheria hii; au (g)atapata sifa zinazopingana na haki ya kuwa kamishna wa Tume ya Habari kwa mujibu wa Sheria hii.
(2) Nafasi ya kila mjumbe atakayeacha kuwa mjumbe wa Tume, kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki, itajazwa ndani ya siku tisini kwa kufuata utaratibu uleule kama uliotumika kumteua mjumbe aliyeacha. (2)Mabadiliko yoyote ya wajumbe wa Tume kwa mujibu wa kifungu hiki ni lazima yawasilishwe bungeni kwa taarifa.
Mamlaka ya Tume 28.(1) Mamlaka ya Tume ya Habari itakuwa kama ifuatavyo: (a) kusimamia utekelezaji wa sheria hii;
(b)kusikiliza malalamiko kutoka kwa umma yanayohusu kunyimwa habari; (c)kuruhusu upatikanaji wa habari zinazohifadhiwa na Tume;
(d)kuanzisha na kusimamia masjala ya taifa ya habari na masjala ndogo; (e)kutunga kanuni kama ilivyoagizwa na Sheria hii; (f)kupokea taarifa na kuanzisha uchunguzi kuhusu matukio ya kunyimwa habari.
Mashitaka dhidi ya Wajumbe wa Tume 29. Hakuna mjumbe yeyote wa Tume ambaye atatiwa hatiani yeye binafsi kwa ajili ya kitendo chochote atakachofanya au kukataa kufanya akiwa na sababu za msingi wakati akitekeleza majukumu, kazi au mamlaka ya Tume.
Uchunguzi na kusikiliza mashauri 30.(1) Tume itakuwa na mamlaka ya awali ya kisheria katika kusikiliza malalamiko yote ya kunyimwa habari, kuruhusu utoaji wa habari zenye kinga ya usiri, mamlaka ya kusikiliza rufaa zinazotoka kwenye vyombo vya taasisi za umma na binafsi vyenye mamlaka ya kusikiliza rufaa za ndani, na mamlaka ya kufanya uchunguzi muhimu kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu yake chini ya Sheria hii.
(2)Tume inaweza, wakati wa kusikiliza malalamiko, kuitisha ushahidi wowote mbele yake na kuamuru mashahidi kutoa ushahidi mbele yake. (3)Usikilizaji wa malalamiko mbele ya Tume utazingatia kanuni za haki za asili.
(4)Upande wowote ambao hautaridhishwa na maamuzi ya Tume ya Habari wakati ikisikiliza malalamiko kwa mara ya kwanza, anaweza kupeleka shauri Mahakama Kuu kwa njia ya rufaa, maombi ya maelekezo au marejeo.
(5)Wakati wote wa kusikiliza malalamiko au rufaa, akidi itakuwa ni wajumbe watatu na miongoni mwao mjumbe mmoja lazima awe mwanasheria. (6)Wakati wa kusikiliza na kuamua mashauri wajumbe watamchagua mmoja wao kuwa mwenyekiti.
(7)Tume inaweza kukaimisha kazi zake chini ya sheria hii kwa afisa au kamati yake yoyote ilmradi Tume haita kaimisha majukumu yake ya kusikiliza na kuamua mashauri na rufaa isipokuwa kwa mujibu wa masharti ya kifungu cha 23(3) cha Sheria hii. (8)Iwapo upande wowote utakaidi amri ya kutoa ushahidi au kufika mbele ya Tume, basi kadri itakavyokuwa, Tume itaendelea kusikiliza hoja za upande mmoja na upande uliokaidi hautakuwa na haki ya kukata rufaa dhidi ya hukumu ya Tume.
Kuhudhuria mbele ya Tume

31. Mtu yeyote anaweza kuhudhuria mbele ya Tume, yeye mwenyewe au kwa kutumia mwakilishi wake anayetambuliwa kisheria, ili kutoa au kutetea malalamiko yaliyowasilishwa mbele ya Tume.
Masjala ya Taifa ya Habari 32.(1) Kutakuwa na rasilimali itakayotambuliwa kuwa ni Masjala ya Taifa ya Habari ambayo itasimamiwa na kuendeshwa na Tume ya Habari iliyoanzishwa kwa mujibu wa sheria hii.
(2)Masjala ya Taifa ya Habari itahifadhi habari zote za umma na inaweza kuwa na masjala ndogo ndogo kadri Tume itakavyoona inafaa.
(3)Kila taasisi ya umma italazimika kuwasilisha aukusajili kwenye Tume, habari zote za umma katika kipindi cha siku tatu za kazi tangu kupatikana kwa habari husika. (4)Mtu yeyote atakuwa na haki ya kupata habari moja kwa moja kutoka Masjala ya Taifa ya Habari. (5)Afisa yeyote wa taasisi ya umma atakayekaidi kutekeleza masharti ya kifungu kidogo cha (3) cha kifungu hiki atakuwa ametenda kosa la jinai na ataadhibiwa kwa kulipa faini isiyozidi shilingi laki tano au kifungo cha miezi sita.
1.
[h=6][/h] [h=6]SEHEMU YA V[/h] [h=6]RUFAA [/h]
Utaratibu wa rufaa za ndani

33.(1) Kila taasisi ya umma na binafsi itaweka mfumo wa rufaa ndani ya taasisi husika kwa kuteua watu ambao hawakuhusika na utoaji wa maamuzi yanayopingwa ili wasikilize rufaa.
(2)Mwombaji habari anaweza kuomba rufaa ya ndani kwenye taasisi binafsi au ya umma dhidi ya uamuzi wa kunyimwa habari au sehemu ya habari au dhidi ya uamuzi wa kutoza ada ili kupewa habari. (3)Mtu wa tatu anaweza pia kukata rufaa kupinga uamuzi wa taasisi wa kutoa habari binafsi zinazomhusu.
(4)Rufaa ya ndani lazima iwasilishwe katika muda wa siku tatu za kazi baada ya uamuzi unaopingwa kutolewa na kupokelewa na mwombaji wa habari au baada ya kukabidhiwa taarifa ya uamuzi wa kukataliwa. (5)Rufaa inaweza kuwasilishwa kwa mdomo, maandishi au kwa njia za kielektroniki ilmradi kwamba rufaa za mdomo zitaainishwa kimaandishi na chombo cha rufaa cha taasisi husika.
(6)Watu wote ambao walipewa taarifa ya ombi la habari kwa mujibu wa kifungu cha 13(3)cha Sheria hii watapelekewa taarifa kuhusu kukatwa kwa rufaa ya ndani kuhusiana na habari zilizokuwa zimeombwa na wanayo haki ya kuleta utetezi au maelezo yao. (7)Mwombaji wa habari ataarifiwa kuhusu kukatwa kwa rufaa ya ndani na mtu wa tatu na atakuwa na haki ya kuleta utetezi wake au maelezo.
(8)Rufaa ya ndani itaamuliwa haraka iwezekanavyo lakini kwa vyovyote vile ndani ya siku saba za kazi tangu kuwasilishwa kwa hati ya rufaa. (9)Mrufani na mtu yeyote wa tatu wataarifiwa kwa maandishi kuhusu uamuzi wa rufaa na pia kuhusu haki yao ya kukata rufaa kwenye Tume ya Habari ndani ya siku saba baada ya uamuzi wa rufaa ya ndani kufanywa au baada ya kupokea taarifa ya uamuzi wa rufaa ya ndani kwa mujibu wa kifungu cha 17(1) cha Sheria hii. (10)Chombo kilichopewa mamlaka ya kusikiliza rufaa za ndani kitaupa kila upande haki ya kusikilizwa na kitatoa uamuzi wake kwa maandishi kikitoa sababu za kukubali au kukataa rufaa.
Haki ya rufaa kwenye Tume ya Habari 34.(1) Upande wowote ambao rufaa yake ya ndani imekataliwa una haki ndani ya siku saba za kazi kukata rufaa kwenye Tume ya Habari, ilmradi kwamba Tume hiyo itakuwa na mamlaka ya kuruhusu kukata rufaa nje ya muda.
(2)Mtu yeyote wa tatu ambaye alipewa taarifa kuhusu kukatwa kwa rufaa ya ndani ataarifiwa pia kuhusu kukatwa kwa rufaa kwenye Tume ya Habari na atakuwa na haki ya kutoa hoja.
(3)Mwombaji wa habari ataarifiwa kuhusu rufaa yoyote iliyokatwa kwenye Tume ya Habari na mtu wa tatu na atakuwa na haki ya kutoa hoja. (4)Bila kujali masharti ya sheria hii au sheria nyingine yoyote, hakuna habari zitakazozuiliwa kutolewa mbele ya Tume ya Habari kwa sababu zozote zile, ilmradi kwamba Tume haitafichua kwa mtu yeyote habari zozote zilizowekewa kinga ya usiri.
(5)Rufaa kwenye Tume ya Habari itaamuliwa ndani ya siku saba za kazi tangu kupokelewa kwa hati ya rufaa. (6)Mkata rufaa na mtu yeyote wa tatu wataarifiwa kwa maandishi kuhusu uamuzi wa rufaa na pia kuhusu haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Tume ya Habari.
(7)Uamuzi wa Tume ya Habari utatekelezwa na mahakama za wilaya kana kwamba ni hukumu na amri za mahakama hizo. (8)Chombo cha rufaa kitawapatia warufani haki ya kusikilizwa na kitatoa uamuzi wake kwa maandishi kikitaja sababu za kukubali au kukataa rufaa.
Mamlaka ya Mahakama Kuu 35.(1) Upande wowote unaweza, ndani ya siku 30, kukata rufaa Mahakama Kuu dhidi ya uamuzi wa Tume ya Habari. (2) Bila kujali masharti mengine ya sheria hii au ya sheria nyingine yoyote, hakuna habari zitakazozuiliwa kuwasilishwa mahakamani kwa misingi yoyote ile, ilmradi kwamba mahakama haitafichua habari zilizowekewa kinga ya usiri na sheria hii kwa mtu yeyote.
Wajibu wa kuthibitisha ushahidi 36. Katika mashauri yaliyoletwa chini ya sehemu hii ya sheria, taasisi ambayo iliombwa kutoa habari ndiyo yenye wajibu wa kuthibitisha ushahidi unaoonesha kwamba uamuzi wake wa kukataa kutoa habari ni halali, ilmradi kwamba Tume ya Habari na Mahakama Kuu vitaona kwamba ni kwa masilahi ya umma kwamba habari husika zitolewe, basi vitaamua kutojali uthibitisho wa ushahidi ili kuruhusu kutolewa kwa habari husika.
SEHEMU YA VI
KINGA, MAKOSA NA ADHABU
Utoaji wa habari kwa nia njema 37.Hakuna mtu atakayefunguliwa mashitaka ya makosa ya jinai au daawa, au atakayepata athari ya kuchukuliwa hatua za nidhamu kazini kwa kutoa habari kwa nia njema katika utekelezaji wa wajibu wake kwa mujibu wa Sheria hii.
Kinga kwa wapiga filimbi 38.(1) Mtu ambaye kwa dhamira ya kuzuia kupatikana kwa habari kwa mujibu wa sheria hii anaathiri, kuharibu, au kubadili habari au kumbukumbu au anazuia kupatikana kwa habari, anatenda kosa la jinai na kustahili adhabu ya faini isiyozidi shilingi milioni mbili au kifungo kisichozidi miaka mitatu au vyote endapo atapatikana na hatia. (2) Hakuna mtu atakayechukuliwa hatua za kisheria, kiutawala au za kiajira kutokana na kutoa habari za taasisi ya umma au binafsi bila mamlaka ya mwajiri wake ikiwa taarifa hizo zinaonesha ufisadi unaotendeka au zinafichua vitendo vya rushwa, utawala mbovu, matumizi mabaya ya madaraka, ubadhirifu, uhatarishaji wa afya ya jamii na uharibifu wa mazingira ilmradi alitoa habari hizo kwa nia njema akiamini kuwa habari hizo ni kweli na ni ushahidi wa vitendo vya kifisadi.
Udanganyi-fu na upotoshaji wa habari 39.Mtu ambaye kwa dhamira ya kutoa habari zisizo za kweli, kusema uongo au kupotosha ukweli anagushi au kubadili habari kwa mujibu wa sheria hii anatenda kosa la jinai na akitiwa hatiani anastahili kupewa adhabu ya faini isiyozidi shilingi milioni mbili au kifungo kisichozidi miaka mitatu au vyote.
Hifadhi na uwekaji wa kumbukumbu 40.(1) Kila taasisi ya umma au binafsi itawajibika kuhifadhi na kuweka habari zake kwa namna ambayo inafungamana na haki ya kupata habari iliyolindwa na Sheria hii.
(2)Taasisi ya umma au binafsi itatunza habari zinazohusu shughuli zake na nakala za habari zote za kiofisi ilizonazo, au zilizo chini ya mamlaka na hifadhi yake, zitahifadhiwa na kutunzwa kwa kipindi ambacho kitaelekezwa kwa mujibu wa Sheria hii.
Kuharibu habari kinyume cha sheria 41.(1) Mtu ambaye kwa kudhamiria anaharibu au kuathiri habari ambazo zimeamriwa kuhifadhiwa na kutunzwa kwa mujibu wa kifungu kidogo cha 28 cha sheria hii, anatenda kosa la jinai ambalo akipatikana na hatia anastahili adhabu ya faini isiyozidi shilingi laki tano au kifungo kisichozidi miezi sita au vyote. (2) Mtu ambaye kwa kudhamiria anaharibu au kuathiri habari ambazo zimeamriwa kuhifadhiwa na kutunzwa kwa mujibu wa kifungu kidogo cha 28 cha sheria hii wakati tayari kuna ombi la habari hizo anatenda kosa la jinai ambalo anastahili adhabu ya faini isiyozidi shilingi milioni mbili au kifungo cha miaka miwili au vyote.
SEHEMU YA VII
MENGINEYO
Kuanzi-shwa kwa Jukwaa la Wadau wa Habari 42.(1) Kutakuwa na jukwaa ambalo litajulikana kwa jina la “Jukwaa la Wadau wa Habari” ambalo litakuwa huru na sehemu muhimu ya ushiriki wa umma katika tasnia ya habari kwa ajili ya kuishauri Serikali na Tume katika masuala yahusuyo habari.
(2)Jukwaa la wadau wa Habari litajumuisha wananchi kupitia sekta mbalimbali ili kuruhusu ushiriki wa wananchi katika masuala ya habari ilmradi kwamba asasi zote za kiraia zitakazojumuika ni pamoja na Baraza huru la habari na jumuiya ya wamiliki wa vyombo vya habari;
(3)Jukwaa la Wadau wa Habari litakuwa na hadhi ya mshiriki asiye na kura katika vikao na shughuli za Tume na litakuwa mshauri mkuu wa Tume. (4)Jukwaa la Wadau wa Habari litakuwa msimamizi mkuu wa maslahi ya jamii katika shughuli za habari na litawajibika kuwasilisha bungeni taarifa kivuli ya mwaka kuhusu masuala ya haki ya kupata habari na utekelezaji wa Sheria hii.
(5)Jukwaa la Wadau wa Habari litakuwa taasisi binafsi na huru lenye katiba yake na litajiendesha lenyewe kwa fedha za wadau, wafadhili na/au ruzuku ya Serikali.
Sheria ya vyombo vya habari 43. Bunge linaweza kutunga sheria ya huduma ya vyombo vya habari itakayozingatia na kutekeleza haki ya uhuru wa vyombo vya habari ili kusimamia na kuruhusu ukuaji wake ilmradi hakuna sheria yoyote itakayokuwa halali kama sheria hiyo inabana uhuru wa habari.
Mamlaka ya kutunga kanuni

44.(1) Tume kwa kushirikiana na Jukwaa la Wadau wa Habari itakuwa na mamlaka ya kutunga kanuni kwa ajili ya kurahisisha matumizi ya Sheria hii.
(2)Kanuni zote zitakazotungwa chini ya sheria hii zitawasilishwa bungeni kwa taarifa ndani ya siku sita za kazi za kikao cha Bunge kinachofuatia kutangazwa kwa kanuni hizo kwenye Gazeti la Serikali. (3)Tume inaweza kutunga kanuni chini ya kifungu kidogo cha (1) cha kifungu hiki kwa ajili ya mambo yafuatayo:
(a)kanuni za maadili ya wajumbe wa Tume na Sekretarieti yake; (b)sifa za kuchaguliwa kwa wajumbe wa chombo cha kusikiliza rufaa za ndani;
(c)mfumo mzuri wa uchunguzi na utatuzi wa malalamiko yaliyoletwa mbele ya Tume ya Habari; (d)ajira za wafanyakazi;
(e)marupurupu ya Sekretarieti; (f)taratibu za kutekeleza na kukazia maamuzi yake; (g)taratibu za kupata habari zilizohifadhiwa na Tume ya Habari na habari zilizohifadhiwa katika masjala zilizoanzishwa chini ya Sheria hii; na (h)fomu na jinsi ya kuwasilisha malalamiko chini ya Sheria hii.
JEDWALI
Chini ya kifungu cha 21(4)
Kanuni za vikao 1.(1) Tume itamchagua Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wake na itatunga kanuni zinazohusu uendeshaji wa vikao vyake na masuala mengine kadri itakavyoona inafaa katika kurahisisha utendaji wa kazi. (2)Tume itakutana mara kwa mara, angalau mara moja kila mwezi, kujadili na kutathmini shughuli zake za kawaida, isipokuwa Tume inaweza kukutana wakati wowote kadri itakavyoona inafaa ili kukidhi shughuli zake.
(3)Mwenyekiti wa Tume ataitisha mkutano wa dharura iwapo atapokea maombi ya kuitishwa kikao kutoka kwa wajumbe wasiopungua watatu. (4)Makamu Mwenyekiti ataongoza kikao chochote cha Tume endapo Mwenyekiti hatakuwapo.
(5)Maamuzi ya Tume ya Habari yatafanywa kwa kura za wajumbe walio wengi na watakaopiga kura katika kikao, na endapo kura zitalingana, basi Mwenyekiti atakuwa na kura ya uamuzi zaidi ya yake ya hiari. (6)Katibu Mtendaji atahudhuria vikao vyote vya kamati kama mtendaji.
(7)Katibu Mtendaji atahakikisha kuwa miniti za kila kikao cha Tume zinahifadhiwa na kuwa zinathibitishwa katika kikao chake kinachofuata na kusainiwa na Mwenyekiti wa Tume. (8)Mwenendo wa Tume hautaathiriwa na kuwapo kwa nafasi iliyoachwa wazi na mjumbe yeyote wa Tume.
Masurufu ya Wajumbe 2. Wajumbe wa Tume watalipwa masurufu na marupurupu mengine kadri itakavyoidhinishwa na Bunge na watalipwa fidia kwa ajili ya gharama, ikiwamo usafiri, malazi na posho, ambazo watazitumia wakiwa katika utekelezaji wa kazi zao za ujumbe wa Tume.
Mamlaka ya kuajiri 3.(1) Tume itakuwa na mamlaka ya kuajiri wafanyakazi kadri itakavyoona inafaa kwa ajili ya kurahisisha utekelezaji wa kazi zake.
(2)Bila kuathiri masharti ya kifungu kidogo (1) cha kifungu hiki, Tume itakuwa na mamlaka ya kuajiri mtaalamu yeyote kwa ajili ya shughuli maalumu au kwa muda mfupi. (3)Tume itawalipa mishahara na posho wafanyakazi wake kadri itakavyoamua mara kwa mara.
Sekretari-eti ya Tume 4.(1) Kutakuwa na Sekretarieti ya kudumu ya Tume ya Habari, ambayo itakuwa chini ya usimamizi wa Katibu Mtendaji.
(2) Tume itamteua Katibu Mtendaji ambaye ataajiriwa na kuacha kazi kwa mujibu wa masharti ya uteuzi.
(3) Tume itaanzisha ofisi katika wilaya zote za Tanzania Bara kwa ajili ya ufanisi katika utekelezaji wa mamlaka na kazi zake.
(4)Tume inaweza kumteua mtu yeyote mwenye utaalamu katika fani maalum ili aisaidie katika utekelezaji wa kazi zake.
(5)Mtu atakayeteuliwa chini ya kifungu kidogo cha (4) atalipwa marupurupu kadri Tume itakavyoamua.
(6)Tume itawateua maafisa na waajiriwa wa Sekretarieti kwa kuwalipa mishahara na kwa masharti na kanuni kadri itakavyoamua ili kuleta ufanisi katika shughuli na kazi za Tume.
(7)Tume itafanya kazi nyingine zozote kadri itakavyoelekezwa na Mwenyekiti kwa maandishi ya mkono wake, au sheria nyingine yoyote.
Mahesabu ya Tume 5.(1) Tume itahakikisha kuwa zinahifadhiwa hesabu sahihi za fedha zake na kuhakikisha ukaguzi wa hesabu zake unafanywa mara ifikapo mwishoni mwa kila mwaka wa fedha na Mkaguzi aliyethibitishwa na Serikali.
(2)Nakala za taarifa za Mkaguzi zilizotajwa katika fasili ya (1) ni lazima ziwasilishwe kwa Waziri ambaye ataziwasilisha Bungeni kwa taarifa.
Taarifa ya mwaka 6. (1) Tume itaandaa, kila ifikapo mwishoni mwa mwaka wa fedha, taarifa ya mwaka kuhusu shughuli zake za mwaka huo na kuwasilisha taarifa hiyo kwa Waziri katika kipindi kisichozidi miezi mitatu baada ya mwaka wa fedha.
(2)Taarifa ya mwaka ni lazima itangazwe na kusambazwa kwa wingi. (3)Taarifa ya mwaka itakuwa na habari zifuatazo:
(a)habari zinazohusu malalamiko ya kunyimwa habari; (b)maelezo kuhusu adhabu zilizotolewa na Tume na maamuzi yake kuhusiana na adhabu hizo;
(c)habari zinazohusu malalamiko ya kunyimwa habari; (d)maelezo kuhusu adhabu zilizotolewa na Tume na maamuzi yake kuhusiana na adhabu hizo;
(e)maelezo kuhusu jinsi asasi za umma na za kiraia zilivyotekeleza sheria hii katika mwaka huo; (f)maelezo kuhusu jinsi Tume ilivyohusisha asasi za kiraia katika kukuza uwezo wake kama jamii inayotekeleza uhuru wa habari; na (g)mchanganuo wa jinsi Tume ilivyofikia malengo yake ya mwaka unaohusika na mwaka unaofuatia.
(4)Tume inaweza kuandaa na kuwasilisha taarifa maalum kwa Serikali kwa kuzingatia maslahi ya umma. (5)Vyanzo vya fedha na rasilimali za Tume zitajumuisha:
(a)mikopo na misaada itakayotengwa na Bunge kwa ajili ya Tume;
(b)fedha ambazo kwa njia yoyote ile zitalipwa kwa Tume chini ya sheria hii au sheria nyingine yoyote au kwa ajili ya utekelezaji wa kazi zake; na (c)Tume inaweza kuwekeza fedha zake kwa kadri itakavyoridhiwa na au kwa kuzingatia masharti yaliyowekwa na sheria za uwekezaji kuhusiana na kuwekeza kwa mdhamana.
(6)Waziri atawasilisha mbele ya Bunge, mapema iwezekanavyo baada ya kuzipokea, nakala za maelezo ya mapato na matumizi iliyotajwa katika Jedwali hili pamoja na nakala ya taarifa ya Mhasibu, taarifa kivuli ya Jukwaa la Wadau wa Habari. (7)Bunge linaweza kwa azimio kutoa maelekezo ya ujumla au ya bayana kwa Tume ambayo italazimika kutekeleza maelekezo hayo.



SABABU NA MADHUMUNI


Muswada huu unalenga kutunga sheria itakayomwezesha mtu yeyote kupata taarifa, jambo ambalo ni haki ya msingi kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri kutokana na mabadiliko ya Katiba ya mwaka 1984. Ibara ya 18 iliyorekebishwa mwaka huo ndiyo msingi wa vipengele vya Muswada huu ambao umegawanyika katika Sehemu Saba na Jedwali moja.

Sehemu ya I
ni mambo ya utangulizi, yaani jina fupi la Muswada, madhumuni na ufafanuzi wa baadhi ya maneno yanayotumika katika Muswada. Kifungu cha 2 kinaharamisha sheria zote zinazowekea vikwazo upatikanaji wa taarifa kutoka taasisi za umma au taasisi zingine.

Sehemu ya II inapambanua dhana ya uhuru wa kupata habari, sambamba na wajibu wa wanaohodhi habari kuzitoa kwa mtu yeyote anayeziomba. Kutakuwa na maafisa habari katika taasisi za umma na vyombo binafsi watakaowajibika kushughulikia maombi ya waombaji wa taarifa. Utaratibu unawekwa wa kufanya maombi, wa utoaji na ukataliwaji wa maombi. Lakini kutakuwa na mazingira mahsusi yanayoruhusu habari fulani zisitolewe, na suala hili linaelezwa katika Sehemu ya III ya Muswada huu ukipitishwa kuwa sheria. Hata hivyo, msamaha huu utadumu kipindi cha miaka kumi tu, na baada ya hapo kila taarifa itaweza kupatikana kama taarifa zingine.

Sehemu ya Nne inaanzisha Tume ya Habari kama chombo kinachojitegemea, kinachoweza kushitaki na kushitakiwa, ambacho kitasimamia utekelezaji wa haki ya wananchi kupata habari kutoka kwa chombo cha umma au taasisi binafsi. Wajumbe wa Tume watatokana na taaluma mbalimbali, kama vile sheria, jinsia, wanahabari, nk ambao watateuliwa kwa kipindi cha miaka mitano ( na wanaweza kuteuliwa tena mara moja tu) na Tume ya Uteuzi. Hakuna anayeweza kuteuliwa kuwa Mjumbe wa Tume kama si raia wa Tanzania, au umri wake ukipungua miaka 18, au akiwa mtumishi wa Serikali, au mfilisiwa-ambaye hajafutiwa ufilisi, n.k.

Sehemu ya V
inaweka mifumo ya rufaa, tangu ngazi ya uongozi wa chombo chenyewe kilichoombwa kutoa taarifa (rufaa ya ndani), na rufaa ya nyongeza kama hapana budi kwa Tume ya Habari, na kutoka hapo kwenda Mahakama Kuu. Ulazima wa kutoa habari unaweza kubatilishwa na Mahakama Kuu kama itabidi, baada ya pande zote kusikilizwa.

Sehemu ya VI inashughulikia kinga ya kutoshitakiwa kwa makosa ya jinai au ya daawakwa wajumbe na waajiriwa wa Kamisheni kwa utendaji wa nia njema na usio na hila kama Muswada huu utapitishwa kuwa sheria. Adhabu zimeainishwa katika Sehemu hii.

Sehemu ya VII
inahusu masuala mbalimbali, pamoja na uanzishwaji wa Jukwaa la Wadau wa Habari. Jedwali linafafanua utaratibu wa utendaji wa Tume, Sekretarieti, mahesabu ya Tume na ujira wa wajumbe wa Tume, na idhini ya kuwekeza fedha za Tume kwa kuzingatia Sheria ya Uwekezaji ya Wadhamini. Dar es Salaam,
 
CDM wote wako makini isipokuwa Shibuda, Mallah, J. Bayo na wenzao feki
 
Ameahidi kutengeneza wimbo kuhusiana na hotuba yake nzima stay tuned!wanamuita suuuguuu ahhhaaaa wanamuiata suguuu sugu sugu suguuu
 
Hivi analitendea haki jimbo lake la mbeya kwa<br />
kuzungumza sana kuhusu wasaniii???????????
<br />
<br />
Bila shaka anawatendea haki kwa sababu alichokuwa anazungumza ilikuwa ni hotuba kutoka kwa waziri kivuli(msemaji wa upinzani) wa habari,vijana,utamaduni na michezo. Kwa hakika ilibidi ajikite zaidi katika eneo la wasanii na tasnia ya habari kwa ujumla. Linapokuja swala la kuwasemea waliomchagua pia huchukua nafasi yake.
 
Mheshimiwa Sugu aendeleza Bifu kwa kuitaka serikali kuinyanganya THT studio na nyumba iliyotolewa na rais kwa wasanii ili irudishwe kwa baraza la sanaa la taifa. Hili limekuja wakati akiwasilisha hotuba ya upande wa upinzani bungeni katika wizara ya vijana na michezo.

Huu ni muendelezo wa mapambano katika Sugu na Ruge Mutahaba ambaye ni mmiliki wa THT ambaye Sugu anamlalamikia kumpiga chenga la macho katika dili la malaria na kupelekea mbunge huyo wa Mbeya mjini kutunga nyimbo ya kushambulia Ruge, THT na Clouds FM uliopewa jina la Anti-Virus.
 
Ni kweli mana RUGE hana uhalali wa kumiliki nyumba hiyo na studio,mana ilitolewa kwa wasanii wote ambayo kimsingi ilitakiwa kuwa chini ya BALAZA LA SANAA,sasa ila kwa usanii na ufisadi wa serikali ya CCM,RUGE kwasababu ni kada wa CCM anaimiliki yeye kwa faida yake yeye mwenyewe,nchi yetu tunaipeleka wapi jamani,sanaa yetu inaelekea wapi.
 
Na makinda anawafanyia haki wapiga kura wake?? Wanawakilishwa na nani?? Fikiria hilo kwanza then nenda mbeya mjini uone kafanya nini sugu sio unaongea kwa kutumia keyboard tu hapa!wasanii sio jamii ya tanzania?kaangalie ilani ya cdm uone dhamira yao ni nini kwa wananchi wa tanzania!
 
Yeah sugu ni jembe la ukweli sina wasiwasi juu yake big up CDM
 
Ametaka iundwe Mamlaka ya Michezo kusimamia uendeshaji na maendeleo viwanja vya mpira..kasikitika taifa kuwa na kiwanja kimoja chenye hadhi ya kimataifa nacho kinaendeshwa hovyo.

Ametaka kuwepo kwa nembo maalum katika kazi za wasanii wote yaani filamu na muziki ili wasanii wanufaike na kizi zao. Bado kakomaa na studio waliyopewa THT na JK pamoja na jengo la serikali.

Hakusahau kuomba wasanii wa kimataifa wanaoletwa wakatwe kodi.
 
Bravo sugu! kawasilisha vizur sana taarifa yake, ambayo kimsingi ipo detailed na kutoa way forward kuliko ya wazir mwenyewe na m/kiti wa kamati
 
Sugu ananikosha sana.anachonifurahisha mweshimiwa huyu ni kwamba, kila siku anakuwa zaidi kiupeo na kiuwasilishaji hoja na uchangiaji bungeni, ameongea mambo ya msingi sana na yenye kutetea pande zote za wizara husika tofauti na waziri husika aliyeongelea suala la mpira wa miguu.

Pongezi sana sugu, tuko pamoja mpaka kieleweke
 
Hivi analitendea haki jimbo lake la mbeya kwa
kuzungumza sana kuhusu wasaniii???????????
sugu analitendea sana haki jimbo lake pengine kupita wabunge wengi sana bungeni hasa wale wavaa rangi ya kijani.

Huwa akichangia hoja muda wote anajali jimbo lake na taifa kwa ujumla,na leo aliposimama kama waziri kivuli,ndo ameua kabisaaaaa kwa kuonekana umakini wake ambao unaimarika siku hadi siku.

Huyu mshkaji ameanza kunipa raha kwa harakati zake za utetezi anazozifanya, naamini kwa miaka hii mitano, watanzania tutaona mengi mazuri kupitia kwake.
 
Waziri huwa anajisahau na kuona wizara ni ya mpira wa miguu tu,jamaa mzima sana tena mbishi yuko chama imara ndiyo maana upeo wake unaongezeka kila siku.bravo man.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom