kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,991
- 17,888
Ikiwa imepita miezi 18 sasa tangu serikali ya muda ya Sudan iafiki kumkabidhi mtawala wa zamani wa nchi hiyo, Omar Hassan al Bashir, kwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), Waziri wa Masuala ya Federali wa Sudan ametangaza kuwa, Khartuom imechukua uamuzi wa kumkabidhi al Bashir kwa mahakama hiyo.
Buthaina Ibrahim Dinar Waziri wa Sudan wa Masuala ya Federali amewaambia waandishi wa habari kuwa, serikali imeamua kumkabidhi Omar al Bashir, rais aliyepinduliwa wa Sudan, pamoja na wahalifu wengine kwa mahakama ya ICC.
Wakati wa safari ya ujumbe wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai mjini Khartoum mwezi Februari mwaka jana, Fadhil Muhammad Saleh aliyeuwa msemaji wa serikali ya Sudan alitangaza kuwa, Khartoum imekubali suala la kuhukumiwa Omar al Bashir katika mahakama hiyo.
Mahakama ya KImataifa ya Jinai (ICC) yenye makao yake mjini Hague Uholanzi, mwaka 2009 hadi 2010 ilimtuhumu rais huyo wa zamani wa Sudan kuwa ametenda jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu katika eneo la Darfur. Hata hivyo al Bashir alikanusha tuhuma hizo na kuitaja mahakama ya ICC kuwa ni chombo cha kisiasa.
Tangu mwaka 2003 eneo la Darfur liliathiriwa na mapigano ya silaha baina ya vikosi vya jeshi la serikali na makundi ya waasi wenye silaha; ambapo ripoti zinasema kuwa, hadi sasa raia laki tatu wameuliwa na wengine karibu milioni 2.5 wamelazimika kuwa wakimbizi.
Jimbo la Darfur, magharibi mwa Sudan lililoathiriwa na machafuko
Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ni mahakama ya kwanza ya kudumu ya kimataifa inayoshughulikia uhalifu wa maangamizi ya kizazi, jinai dhidi ya binadamu, jinai za kivita na nyinginezo.
Jeshi la Sudan Aprili 11 mwaka 2019 lilimng'oa madarakani Omar Hassan al Bashir baada ya kupambana moto maandamano ya wananchi waliokuwa wakilalamikia hali mbaya kiuchumi na kijamii na kisha wakamfunga jela kwa makosa ya ufisadi.
Buthaina Ibrahim Dinar Waziri wa Sudan wa Masuala ya Federali amewaambia waandishi wa habari kuwa, serikali imeamua kumkabidhi Omar al Bashir, rais aliyepinduliwa wa Sudan, pamoja na wahalifu wengine kwa mahakama ya ICC.
Wakati wa safari ya ujumbe wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai mjini Khartoum mwezi Februari mwaka jana, Fadhil Muhammad Saleh aliyeuwa msemaji wa serikali ya Sudan alitangaza kuwa, Khartoum imekubali suala la kuhukumiwa Omar al Bashir katika mahakama hiyo.
Mahakama ya KImataifa ya Jinai (ICC) yenye makao yake mjini Hague Uholanzi, mwaka 2009 hadi 2010 ilimtuhumu rais huyo wa zamani wa Sudan kuwa ametenda jinai za kivita na jinai dhidi ya binadamu katika eneo la Darfur. Hata hivyo al Bashir alikanusha tuhuma hizo na kuitaja mahakama ya ICC kuwa ni chombo cha kisiasa.
Tangu mwaka 2003 eneo la Darfur liliathiriwa na mapigano ya silaha baina ya vikosi vya jeshi la serikali na makundi ya waasi wenye silaha; ambapo ripoti zinasema kuwa, hadi sasa raia laki tatu wameuliwa na wengine karibu milioni 2.5 wamelazimika kuwa wakimbizi.
Jimbo la Darfur, magharibi mwa Sudan lililoathiriwa na machafuko
Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ni mahakama ya kwanza ya kudumu ya kimataifa inayoshughulikia uhalifu wa maangamizi ya kizazi, jinai dhidi ya binadamu, jinai za kivita na nyinginezo.
Jeshi la Sudan Aprili 11 mwaka 2019 lilimng'oa madarakani Omar Hassan al Bashir baada ya kupambana moto maandamano ya wananchi waliokuwa wakilalamikia hali mbaya kiuchumi na kijamii na kisha wakamfunga jela kwa makosa ya ufisadi.