Suala la mahusiano: Wanawake wengi tunafeli

Suala la mahusiano: Wanawake wengi tunafeli

Sasa MANKA kuna dada yako mmoja ameshanidangia, labda nayo ni njia ya utafutaji. Hapa kinachotafutwa ni pesa chaliii yangu.Endelea kuwaelimisha aiseee, siyo vizuri hivyo wanavyofanya. Tunaishia kuwa kizazi cha watu wa hovyo hovyo, ma single mothers kila kona, watoto hawawajui hata baba zao, ukimwi na mambo mengine kadha wa kadha.
 
Wazee nimewasoma huko juu naona tu mnamwaga sifa kwa Manka...

Manka kuwa makini hawa watu sio wazuri washaskia una 24 basi maudenda yashawatoka wanasifia sifia mwandiko wako tu.
sawa daby niko makiniii
 
Tamaa kupenda mambo makubwa kuliko uwezo wetu vinatuponza mno na mambo ya kuiga kushikwa akili, wanawake wengi tuko hivyo

Hiyo iwe hata kwa wanaume, tutambue unapompendea mtu kwa kitu tuseme pesa labda au shape au sura au uzur wake hapo unakua umemtamani hujampenda, upendo wa dhati hauangalii kitu cha kupenda unajikuta unampenda tu mtu kwa jinsi alivyo
Naona mmeamua kuongea maneno yenye busara. Tumieni hii nafasi kuwafundisha wenzenu, hakuna kitu kibaya kama "bhanaae ndo ishakuwa hivyo". Kukata tamaa ni kubaya sana. Hata kama binti ulianza kwenye mahusiano ya kupewa kila kitu unachokitamani in a blink of an eye mambo hubadirika.
Na nawapa siri sasa mwanaume aliyekupenda na anayemaanisha kuwa nawe hawezi kukupatia kila unachohitaji kwa muda unaotaka. Lazima tuwapime wapenzi wetu, je ninapokuwa sina ananichukuliaje? Nikiona anamtazamo wa kung'ang"aniza au kununa pale ninapokuwa sina kitu huyo hafai, ndipo pale fikra za kuwa nawe bila malengo zinazaliwa.
Uhusiano wowote wahitaji creativity, protection, care and the last thing ni persereverance.
 
Ila pia kumbuka si kila ambaye hana pesa ndo ana mapenzi ya kweli.

Na si kila mwenye pesa eti hana mapenzi ya kweli.

Na hakuna ubaya katika kutaka vile uvitakavyo kwa mpenzi maana kinyume na hapo utakuwa zoa zoa.

Ila hebu tuambie dada Manka, mapenzi ya kweli ndo nini hasa?

Maana tunasisitizwa tuwe na wenye mapenzi ya kweli; ndo wakoje?
 
Naona mmeamua kuongea maneno yenye busara. Tumieni hii nafasi kuwafundisha wenzenu, hakuna kitu kibaya kama "bhanaae ndo ishakuwa hivyo". Kukata tamaa ni kubaya sana. Hata kama binti ulianza kwenye mahusiano ya kupewa kila kitu unachokitamani in a blink of an eye mambo hubadirika.
Na nawapa siri sasa mwanaume aliyekupenda na anayemaanisha kuwa nawe hawezi kukupatia kila unachohitaji kwa muda unaotaka. Lazima tuwapime wapenzi wetu, je ninapokuwa sina ananichukuliaje? Nikiona anamtazamo wa kung'ang"aniza au kununa pale ninapokuwa sina kitu huyo hafai, ndipo pale fikra za kuwa nawe bila malengo zinazaliwa.
Uhusiano wowote wahitaji creativity, protection, care and the last thing ni persereverance.
Facts words,sisi kama mabinti tunahitaji kuwa na familia baadae tena imara anza sasa hv punguza marafiki wasio na faida,acha kulinganisha masuhiano yako na ya marafiki zako tambua wanaume nibtofauti na kila aliyeanzisha mahusiano kulikuwa na makubaliano,Acha kuiga kila kitu na tamaa zisizo na msingi hata wale wanaotupenda kwelu tunashindwa kuwajua,Tuonyeshe kupenda wanaume zetu kwa hali zote kitu ambacho ukipendi toka kwake kama mavazi,muonekano na vitu vingine ongea naye taratibu na mbadilishe awe unavyotaka amini huwezu pata mwanaume aliyekamili kila sector?Ukimpata wa hvyo yupo aliyemtengeneza na hapo kwako atapita tu sio mkaaji
 
Habari za jioni
Swala la mahusiano limekuwa changamoto sana hasa kwa sisi wanawake tunaishia kulalamika wanaume wote ni wachezeagi tatizo liko kwetu tubadilike.

Tuzingatie hili swala kabla hujaanzisha mahusiano mapya lazima ujiulize mahusiano unayotaka kuanzisha ni ya namna gani?yakufikia ndoa au kupotezeana siku.

Tuache kuweka vitu mbele kwa kuangalia pesa na ukaangali utafaidika na nn katika mahusiano unayotaka kuingia.Anza kwanza ndo hayo maswala yaje baadae

Tuache kuweka vigezo nataka mwanaume wangu awe hv na awe na hiki na kile,Umemuumba wewe?awe na kila kitu unachokitaka vitu vingine vinatengnezwa ndani ya mahusiano.Tujitambue aisee

Angalia mapenzi ya kweli pesa inakuja baadae utaenjoy ukishatengeneza mahusiano imara wala utaombaomba utapata kwa mwanaume wako kwa sababh ataona yuko na mtu sahihi na muda sahihi.

NB:Mapenzi ya kweli yapo wanawake tubadilike ili haya majina ya slay queen&wadangaji tusiitwe
Hongera sana kwa kuliona hili. Mawazo yako yanaangalia mbali sana, kama kutakuwa hakuna mahusiano yenye uimara kizazi kijacho kitakuwa cha ajabu sana na watawalaumu wanawake wa sasa kwakutopanda mbegu njema ndani yao.
Nasi wanaume tubadirike tuwasaidie wenza wetu pale tunapoona wanaenda tofauti na matarajio yetu. Let's take a moment ya kuwarekebisha kabla ule msemo wa "Ninampenda lakini kwa tabia zake wacha nimtumie tu, nitapata mwingine mwenye tabia hii na ile" Wanawake ni viumbe vyepesi kubadirika. Let's base on the positive side of the things na sio kuwaharibia zaidi.
 
Ila pia kumbuka si kila ambaye hana pesa ndo ana mapenzi ya kweli.

Na si kila mwenye pesa eti hana mapenzi ya kweli.

Na hakuna ubaya katika kutaka vile uvitakavyo kwa mpenzi maana kinyume na hapo utakuwa zoa zoa.

Ila hebu tuambie dada Manka, mapenzi ya kweli ndo nini hasa?

Maana tunasisitizwa tuwe na wenye mapenzi ya kweli; ndo wakoje?
Zurie
Mapenzi ya kweli yapo sana na unaweza kuyapata hata kwa mwanaume mwenye hela.Lakini mapenzi hayo yanatengenezwa kuanzia mwanzo lazima ujue unaingia kwenye mahusiano ya namna gani?
Mwanamke lazima uwe clean tabia za kimjini mjini uziache,uongo,tamaa na kujiona wewe ni bora hakuna zaidi yako.wanaume wanatupima na vitu vidogo sana na tunafeli
 
Teh, mada kama hizi lazima upate support kubwa ya Me, ila bottom line kuhonga ni wajibu
 
Acha kashfa hope una dada wewe maisha yamebadilika wanaume wenyewe mnagegedwAaa

Sasa kwani kuwa na dada ndio kuondoa ukweli kuwa mwanamke no chombo Cha starehe ....nae anagegedwa tuu. Maisha yabadilike lakini kugegedwa ndio kazi yenu namba moja. Kukaa ofisini ni mbwembwe tuu
 
Teh, mada kama hizi lazima upate support kubwa ya Me, ila bottom line kuhonga ni wajibu
Hatujakataa and that's our nature, it's been created within us by God, but kuhonga hakuingiliani na kujenga tamaa na mwishowe kugeuka tabia ya mwanamke. Hata mkeo anapohitaji kitu flani na ukampatia hiyo nayo pia ni part ya kuhonga in one way.
Namuunga mkono dada Manka na Madame S kwasababu wimbi la wanawake wasiotambua futures zao ni wengi sana. Bora wewe na mimi hatuchoki mapema kama wao wakishatumika kupitiliza, kuna kijana atakayependa kuingia kwenye ndoa na mwanamke aliyejichosha kisa tamaa zake? Atapenda kuona mwanamke wake ni muhitaji kupitiliza yakwamba kila akionacho huko nje au kwa mtu fulani, rafiki zake naye anataka? Nadhani jibu ni hapana... When it comes to marriage you know how determinants We become.
 
Kunywa buyu LA mbege nakuja lipa,umeandika ukweli mtamu kwa sisi wanaume,na ukweli mchungu kwa wanawake
 
Hatujakataa and that's our nature, it's been created within us by God, but kuhonga hakuingiliani na kujenga tamaa na mwishowe kugeuka tabia ya mwanamke. Hata mkeo anapohitaji kitu flani na ukampatia hiyo nayo pia ni part ya kuhonga in one way.
Namuunga mkono dada Manka na Madame S kwasababu wimbi la wanawake wasiotambua futures zao ni wengi sana. Bora wewe na mimi hatuchoki mapema kama wao wakishatumika kupitiliza, kuna kijana atakayependa kuingia kwenye ndoa na mwanamke aliyejichosha kisa tamaa zake? Atapenda kuona mwanamke wake ni muhitaji kupitiliza yakwamba kila akionacho huko nje au kwa mtu fulani, rafiki zake naye anataka? Nadhani jibu ni hapana... When it comes to marriage you know how determinants We become.
Mwanaume kumpatia mwanamke kitu sio kosa ila inakuja pale unapokuwa na mahusiano huwezi kupata kitu mpk pesa itumike hapo ndo tunasema toa pesa upate kitu au mkono mtupu haulambwi?Lakini pale unapokuwa na mahusiano na mpz wako anakusaidia mambo tofauti tofauti na mengine hata yasiyohitaji pesa hiyo inaitwa mapenzi kusaidiana
 
wanawake wenye mtazamo huu wamekuwa ni "viumbe" walio hatarini kutoweka kama vile vifaru weupe mbugani!
 
Back
Top Bottom