Idofu
Senior Member
- Oct 24, 2022
- 124
- 214
Nimemsikiliza Waziri Mbarawa Bungeni, nimemsikiliza Msigwa, nimewasikiliza baadhi ya wabunge wa CCM Bungeni, bado naona hawajakata kiu ya Watanzania kuhusu hilo Suala.
Swali ambao najiuliza, kwanini Mwanasheria Mkuu amebaki kimya? Kwa nini wale wabunge angalau wanaoheshimika mbele wananchi wamebaki kimya kwenye hili sakata? Bahati mbaya sana Waziri husika hana ushawishi mbele wa wananchi na Watanzania kwa ujumla, kuendelea kumtegemea Mbarawa kuwa atawaelimisha wananchi, tunajidanganya.
Hili suala sio dogo kabisa, chama kiwazue wanasiasa ndani ya CCM kulizungumzia na badala yake, watumike watendaji walioko Serikalini kuja kutolea ufafanuzi.
Rais wetu wa Awamu wa Sita alianza vizuri sana, lakini kwa hili la Bandari limefuta mema yake yote aliyoyafanya ndani ya miaka miwili!
Swali ambao najiuliza, kwanini Mwanasheria Mkuu amebaki kimya? Kwa nini wale wabunge angalau wanaoheshimika mbele wananchi wamebaki kimya kwenye hili sakata? Bahati mbaya sana Waziri husika hana ushawishi mbele wa wananchi na Watanzania kwa ujumla, kuendelea kumtegemea Mbarawa kuwa atawaelimisha wananchi, tunajidanganya.
Hili suala sio dogo kabisa, chama kiwazue wanasiasa ndani ya CCM kulizungumzia na badala yake, watumike watendaji walioko Serikalini kuja kutolea ufafanuzi.
Rais wetu wa Awamu wa Sita alianza vizuri sana, lakini kwa hili la Bandari limefuta mema yake yote aliyoyafanya ndani ya miaka miwili!
