Suala kuhusu serikali ya Zanzibar baada ya uchaguzi!

Suala kuhusu serikali ya Zanzibar baada ya uchaguzi!

Ngida1

JF-Expert Member
Joined
Aug 25, 2009
Posts
586
Reaction score
206
Kama tujuavyo kuwa Katiba ya Zanzibar inaweka wazi kuwa Zanzibar itakuwa na serikali ya Umoja wa Taifa inayoundwa na mshindi wa uchaguzi na aliyeshindwa.

Kutokana na uchaguzi huu wa 2015 tunajua wazi kuwa CUF haitopewa ushindi na kwahivyo Maalim Seif hatokubali kuwa sehemu ya serikali ya Dr Shein, suala ni kuwa, je, Dr Shein peke yake ataweza kuunda serikali kutokana na Katiba iliyopo?

Kama Dr Shein hatoweza, je, Zanzibar itaweza kukaa bila ya serikali kwa muda gani?

Au kitatokea kitu gani hapa hata business iwe as usual?

Rais mpya wa Tanzania atakaechaguliwa atafanya nini juu ya suala hili kwenye backyard yake?
 
Magufuli kwenye kupatanisha na kusuluhisha mtoe....hilo hayumo na hana uwezo
 
hizo propaganda za kueneza ccm imeshinda mziache mara moja. Zanzibar cuf imeshinda na bara haijulikani nani mshindi.!!

Kaka, tunasema kuwa CUF haitopewa serikali Zanzibar sio kwa kupenda lakini hivyo ndivyo ilivyo na utakuja kuona hivyo kesho au kesho kutwa!
Zanzibar na Bara are two separate countries apart in one country called Tanzania!
 
Kaka, tunasema kuwa CUF haitopewa serikali Zanzibar sio kwa kupenda lakini hivyo ndivyo ilivyo na utakuja kuona hivyo kesho au kesho kutwa!
Zanzibar na Bara are two separate countries apart in one country called Tanzania!

Dah,yaani watu mnajiaminisha mpaka basi na wakati ukweli unaonekana!!!
 
hizo propaganda za kueneza ccm imeshinda mziache mara moja. Zanzibar cuf imeshinda na bara haijulikani nani mshindi.!!

Yaani ndugu yangu ndio hivyoo washapanga na wanajua kama tu vile Dodoma zilivyokuja za chinichini Lowassa kakatwaa mwisho wa siku ikawa kweli. Kukupeenda hatuachii Lowassa wee hatukuachii.
 
Kama anashinda mwingine anatangazwa mwingine haina haja ya kufanya uchaguzi na kupoteza resources for nothing
 
hizo propaganda za mtoa hoja ni zakijinga tena akome aliyemwambia shein hataachia nchi ni nani?
zanzibar ni ya shein?uchaguz ni kushinda nakushindwa atakaa pemben awe mpinzan kama hataki akae pemben ccm itafute mtu mwingine makamu wa rais wa kwanza
 
Kama tujuavyo kuwa Katiba ya Zanzibar inaweka wazi kuwa Zanzibar itakuwa na serikali ya Umoja wa Taifa inayoundwa na mshindi wa uchaguzi na aliyeshindwa.
Katiba ya Zanzibar ipo wazi katika hili-- kwanza, condition ya kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais sio lazima awe yule ambae aligombea Urais kupitia chama kilichoshika nafasi ya pili (provided wapo at least 10% of votes) bali yeyote kutoka chama husika ambae ana sifa za kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi! Hivyo basi, Seif akilemba halafu wenzake wakamzunguka; mambo yataenda kama kawa!

Lakini kubwa zaidi, katiba imesema wazi ikiwa chama kilichoshika nafasi ya pili hakitatoa mtu-- Ibara ya 39A Ibara ndogo ya kwanza inasema:
Endapo, ndani ya siku saba mara baada ya Rais kushika madaraka, chama kinachostahiki kutoa Makamo wa Kwanza wa Rais, kitashindwa kuwasilisha kwa Rais jina la uteuzi wa Makamo wa Kwanza wa Rais, Rais, bila ya kujali masharti ya kifungu cha 39(1) na (3) cha Katiba, atawacha wazi nafasi ya Makamo wa Kwanza wa Rais na kuteua Makamo wa Pili wa Rais.
Hivyo basi, kwa mujibu wa hiyo Ibara, yeyote atakayeshika nafasi ya pili na akasusa; yule atakayetangazwa kwamba ni Rais anaendelea kuunda serikali kama kawaida ambayo itakuwa na Makamu wa Pili peke yake!!

NB: Ibara ya 39(1) na 3 ndizo zinaongelea uwepo wa Makamu wa Kwanza wa Rais.
 
Dunia nzima inajua Seif ndiye mshindi Zanzibar hilo halina ubishi,kwanini hasipewe !!yale mambo aliyofanyiwa chaguzi zilizopita ya kuibiwa hayapo tena
 
Katiba ya Zanzibar ipo wazi katika hili-- kwanza, condition ya kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais sio lazima awe yule ambae aligombea Urais kupitia chama kilichoshika nafasi ya pili (provided wapo at least 10% of votes) bali yeyote kutoka chama husika ambae ana sifa za kuwa Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi! Hivyo basi, Seif akilemba halafu wenzake wakamzunguka; mambo yataenda kama kawa!

Lakini kubwa zaidi, katiba imesema wazi ikiwa chama kilichoshika nafasi ya pili hakitatoa mtu-- Ibara ya 39A Ibara ndogo ya kwanza inasema:
Hivyo basi, kwa mujibu wa hiyo Ibara, yeyote atakayeshika nafasi ya pili na akasusa; yule atakayetangazwa kwamba ni Rais anaendelea kuunda serikali kama kawaida ambayo itakuwa na Makamu wa Pili peke yake!!

NB: Ibara ya 39(1) na 3 ndizo zinaongelea uwepo wa Makamu wa Kwanza wa Rais.
Mfano CUF ama CCM imesusu hiyo serikali isiyokuwa na makamu wa kwanza wa rais itadunda bila mawaziri kutoka upande wa pili? Tumewahi kushuhudia CUF kususia baraza la wakilishi utawala wa Salmin Amour.
 
Maalim seif rais amepata kura 200,077 wakati shein kura 178,363 hivyo amemzidi dr shein kwa kura 21714. Ushindi wa maalim seif ni asilimia 52.87 anasubiri kutangazwa na kuapishwa tu
 
Mfano CUF ama CCM imesusu hiyo serikali isiyokuwa na makamu wa kwanza wa rais itadunda bila mawaziri kutoka upande wa pili? Tumewahi kushuhudia CUF kususia baraza la wakilishi utawala wa Salmin Amour.
Serikali itakosa tu social and political legitimacy lakini itakuwa serikali halali kisheria! Ibara ya 42A inaeleza kwamba endapo Mawaziri kutoka upande wa pili hawatatokea ndani ya siku 7 tangu uteuzi wao, Rais ataacha nafasi hizo wazi na ikiwa wataendelea kutotokea kwa muda wa siku 90; kifungu kinachomtaka ateue mawaziri kwa kuangalia uwiano wa majimbo wa vyama vilivyotakiwa kuunda serikali; hicho kifungu kinapigwa chini na Rais anateua watu wengine.

Kwahiyo ikitokea yeyote amesusia; shughuli za serikali zitaendelea kama kawaida ingawaje kutokana na kukosa social and political legitimacy; inaweza kujikuta inapata external pressures hususani zile za kuitaka wakae mezani! Don't forget; vifungu vingi ili viweze kupita bungeni/baraza la wawakilishi; kinachohitajika is just a coloumn/ waliohudhuria bungeni na sio kuangalia idadi ya wabunge/wajumbe wote wa baraza! Kwa maana hiyo, shughuli za Baraza la Wawakilishi nazo zitaendelea kama kawaida hata ikitokea kuna upande umesusa.
 
Back
Top Bottom