Wewe umesemadaa simba yangu ni shida. ligi imechezwa karibu msimu mzima yaani kamati ya usajili imeshindwa kutafuta mshambukliaji wa maana east and central afrika mpaka kwenda kuangukia kwa huyo babu wa zambia. ina maana hata CHALLENGE hawakuona mshambuliaji kijana. nahisi kuna watu wanafaidika haiwezekani timu kubwa kama simba na kwa sasa uchumi wao upo vizuri halafu mnakuwa na mchezaji mmoja tu tena babu wa miaka 34 anafanya majaribio. hivi kila siku kwa nini hao viongozi hawajiulizi kuwa timu inacheza vizuri dakika 60 tu na baada ya hapo inakata pumzi?. goli alilofunga huyo mzambia dhidi ya KMC la kawaida sana hata Jama Mba au Akufo angeweza kufunga lakini cha ajabu linapigiwa debe kwenye kila chombo cha habari. ushauri wangu kwa mo dewji; unda timu ya wataalamu wa scouting. hiyo kamati ya usajili ipo hapo kwa ajili ya kusajili tiu kila mwaka lakini sio kusajili kwa ajili ya miaka mitano ijayo. leo hii yanga wanasajili vijana kwenye timu yao sisi tunaongeza vibabu halafu tunategemea kuchukuwa ubingwa. ndio sababu ikifika raundi ya pili mwishoni timu inakuwa hoi ubingwa unaenda jangwani.
Hahahaha pape ndaw
Kuna lile li Akkufor pia lilikuwa linatupia sana Simba ikicheza na Burkinafaso ya MatomboHivi Pape Ndaw mechi za majaribio hakufunga??
Nimemkumbuka sana huyu foward matata toka mitaa ya msimbazi nasikia mnataka kumrudisha tena