The Garang
JF-Expert Member
- Jan 16, 2018
- 2,333
- 4,152
Assalamu alaikum,
Mapenzi majani huota popote.
Imepita takribani Miaka zaidi ya 10 na kidogo tangu nilipokutana na msichana wangu wa kwanza, mdada aliyenifanya niinjoi maisha ya sekondari, mdada aliyenifanya niuze jina kwa mashikaji Hadi na walimu pia,mdada aliyenipa chachu ya kupambana katika masomo yangu.
"... Leo tunachagua viongozi wa darasa wa muda Hadi mtakapokaa ki mikondo, Nani mnapendekeza awe montress, anasimama dada mmoja na kupendekeza jina la mdada mmoja aliekuwa amekaa pembeni yake..."
Ilikuwa ni kauli iliyotoka Kwa kiranja mojawapo ikitutaka tupendekeze majina ya viongozi wa muda wa darasa.
Mdada anasimama ni mweupe, baby face na aibu kwa sana.
Kwa mara ya kwanza moyo ulipatwa na kitu kisicho chakawaida nilivomuangaliaa yule mtoto mapigo ya moyo yalinienda kasi.
Basi, wakapendekeza majina, worse or good enough hakuchaguliwa. Basi ikawa ni furaha yangu ni kawa natafuta kila namna ya kujiweka karibu yake niweze hata kuongea naye, kumuona class ilikuwa ndo Furaha yangu. Nlikuwa nakaa nyuma ya darasa ili niweze kumuona vizuri akiwa mbele, kuna wakati asipokuja shule nlikuwa naulizaa kwa namna ambayo anayeulizwa hatohisi lolote juu yangu. Akifanya kosa nlikuwa naumia kuona mtoto akipigwa nlikuwa natamani nipigwe kwa ajili yake binti wa watu asichapwe.
Mikondo imegawanywa bahati nzuri tukapangwa mkondo mmoja, maisha yakaendelea ye ndo alikuwa furaha yangu kwa muda wote Hadi namaliza shule.
Kipindi hicho Sijaitongoza mdada nasijui naanzia wapi kumuambiaa, basi siku zinaenda kuna jamaa yangu akaja shtukia kuwa namuelewa mtoto. Jamaa alijuaje??? Kipindi tuko teen tulikuwa tunaandika jina lako pamoja na la yule unayempenda halafu tunakokotoa asilimia ngapi zinapatikana.
Basi nikakokotowa pale na kupata asilimia zangu za kutoshaa , nshasahau ni ngapi ila zililikuwa za kunishawishi nifanye next move. Nikamaliza kokotowa nakuchana kikaratasi nikatupa chini.
Eeeewh bwanaa eeewh kuna jamaa yangu cjui alikuwa anatafuta nn akaona vile vikaratasi na akaunganishaa , hapo ndo akaliona jina la yule Binti ninaye mkubari.
Utoto mwingi taarifa zikasambaa kwa mashikaji,kuna siku Niko mapumziko ,hiyo Binti anaongeleshwa na wakaka wengine nikaja itwa, The Garang demu wako anaongeleshwa kule dirishani ,basi mie naenda karoho kanauma Sina la kufanya kisu butu.
Siku zimeenda mdada hajui kama nampenda, basi kuna jamaa yangu mmoja mkorofi akaenda kuniitia na kumpa maneno ya awali kuwa mdau The Garany namkubali, mtoto akawa Hana la kufanya. Basi siku nimekaa na wadau nikaitiwa mtoto huyu hapa ongea naye Domo zito hata cjui ilikuwajeee basi dogo akaondoka lakin akawa ashajua mdau namkubali.
Kuna siku nikajilipua nikaitiwa mtoto nikaenda kumpanga bint anagoma natamani Hadi niliee, basi nikaachana nae.
Mda umepita kidogo huku nikiwa nafanya attempts kadhaa, MWISHOWE Binti kamuagiza rafiki yake aje kunambia amekubali lakini iwe Siri, ukisikia Furaha ndo hapa sasa
Soma nikiwaa naandika sehemu inayofata
Mapenzi majani huota popote.
Imepita takribani Miaka zaidi ya 10 na kidogo tangu nilipokutana na msichana wangu wa kwanza, mdada aliyenifanya niinjoi maisha ya sekondari, mdada aliyenifanya niuze jina kwa mashikaji Hadi na walimu pia,mdada aliyenipa chachu ya kupambana katika masomo yangu.
"... Leo tunachagua viongozi wa darasa wa muda Hadi mtakapokaa ki mikondo, Nani mnapendekeza awe montress, anasimama dada mmoja na kupendekeza jina la mdada mmoja aliekuwa amekaa pembeni yake..."
Ilikuwa ni kauli iliyotoka Kwa kiranja mojawapo ikitutaka tupendekeze majina ya viongozi wa muda wa darasa.
Mdada anasimama ni mweupe, baby face na aibu kwa sana.
Kwa mara ya kwanza moyo ulipatwa na kitu kisicho chakawaida nilivomuangaliaa yule mtoto mapigo ya moyo yalinienda kasi.
Basi, wakapendekeza majina, worse or good enough hakuchaguliwa. Basi ikawa ni furaha yangu ni kawa natafuta kila namna ya kujiweka karibu yake niweze hata kuongea naye, kumuona class ilikuwa ndo Furaha yangu. Nlikuwa nakaa nyuma ya darasa ili niweze kumuona vizuri akiwa mbele, kuna wakati asipokuja shule nlikuwa naulizaa kwa namna ambayo anayeulizwa hatohisi lolote juu yangu. Akifanya kosa nlikuwa naumia kuona mtoto akipigwa nlikuwa natamani nipigwe kwa ajili yake binti wa watu asichapwe.
Mikondo imegawanywa bahati nzuri tukapangwa mkondo mmoja, maisha yakaendelea ye ndo alikuwa furaha yangu kwa muda wote Hadi namaliza shule.
Kipindi hicho Sijaitongoza mdada nasijui naanzia wapi kumuambiaa, basi siku zinaenda kuna jamaa yangu akaja shtukia kuwa namuelewa mtoto. Jamaa alijuaje??? Kipindi tuko teen tulikuwa tunaandika jina lako pamoja na la yule unayempenda halafu tunakokotoa asilimia ngapi zinapatikana.
Basi nikakokotowa pale na kupata asilimia zangu za kutoshaa , nshasahau ni ngapi ila zililikuwa za kunishawishi nifanye next move. Nikamaliza kokotowa nakuchana kikaratasi nikatupa chini.
Eeeewh bwanaa eeewh kuna jamaa yangu cjui alikuwa anatafuta nn akaona vile vikaratasi na akaunganishaa , hapo ndo akaliona jina la yule Binti ninaye mkubari.
Utoto mwingi taarifa zikasambaa kwa mashikaji,kuna siku Niko mapumziko ,hiyo Binti anaongeleshwa na wakaka wengine nikaja itwa, The Garang demu wako anaongeleshwa kule dirishani ,basi mie naenda karoho kanauma Sina la kufanya kisu butu.
Siku zimeenda mdada hajui kama nampenda, basi kuna jamaa yangu mmoja mkorofi akaenda kuniitia na kumpa maneno ya awali kuwa mdau The Garany namkubali, mtoto akawa Hana la kufanya. Basi siku nimekaa na wadau nikaitiwa mtoto huyu hapa ongea naye Domo zito hata cjui ilikuwajeee basi dogo akaondoka lakin akawa ashajua mdau namkubali.
Kuna siku nikajilipua nikaitiwa mtoto nikaenda kumpanga bint anagoma natamani Hadi niliee, basi nikaachana nae.
Mda umepita kidogo huku nikiwa nafanya attempts kadhaa, MWISHOWE Binti kamuagiza rafiki yake aje kunambia amekubali lakini iwe Siri, ukisikia Furaha ndo hapa sasa
Soma nikiwaa naandika sehemu inayofata