StarTimes Tanzania
JF-Expert Member
- Jun 11, 2013
- 260
- 141
- Thread starter
-
- #741
Naomba kuuliza maswali mawili 1) ni lini mtaingiza station za radio za Tanzania maana watumiji cc ni watanzania 2) kwanini ving 'amuzi vingine vina lugha ya kiswahili na vingine vina kifaransa na kiingeraza tu??? 0629088763
Hamjaamua kuwaunganisha wateja wenu wote kwenye huduma ya FTA. Kama mmeona wateja hawana hela na mmeamua kuwalipisha hiyo hela kila mwisho wa mwezi kwa channneli za bure ni zaidi ya wizi. Je, TCRA wanataarifa juu ya mpango wenu au ndo njia yenu ya kuwapiga wananchi kwa kisingizio cha kusema "wantanzia wengi hawana hela".Habari yako kwabwina pole sana kwa usumbufu unaoupata
Startimes tuna ving'amuzi vya aina mbili cha kwanza ni "FTA decoder" bei ya king'amuzi hiki ni Shilingi 89,000, ukiwa na king'amuzi hiki utafurahia chaneli zote za ndani bure kwa muda wote, hii ni kwa mujibu wa sheria na muongozo toka kwa mamlaka husika ikiwemo TCRA.
Kutokana na gharama ya 89,000 kuonekana kubwa na watu wengi kushindwa kuimudu, na ili kuhakikisha kila mtanzania anafurahia huduma ya Television bila kujali uwezo wake startimes kwa kuzingatia maombi na pia maoni toka wa wateja iliamua kupunguza bei ya ving'amuzi na kuwa na kingamuzi chenye bei maalumu, startimes ikaweka ving'amuzi vyenye bei maalumu 'STARTIMES SUBSDIZED DECODER', bei yake ni bei ya chini kulinganisha na bei ya soko (unalipia shilingi 34,000 kupata king'amuzi hiki, hii 34,000 ni hela ya huduma tu) , lengo kubwa ni kuhakikisha mteja anapata na king'amuzi kwanza. kupitia king'amuzi hiki mteja analipia gharama ya huduma tu ambayo anaweza kulipia kwa siku, wiki au mwezi ili kupata chanel za ndani na chaneli za nje.
Lakini baadae mteja mwenye king'amuzi hiki 'SUBSDIZED DECODER' akipata fedha anaweza kukibadilisha kuwa king'amuzi cha FTA, mteja anaweza kukibadilisha kwa kufika katika duka letu la startimes lililo karibu yake na kulipia 'PRICE DIFFERERENCE' (Tofauti ya bei kati ya SUBSDIZED Decoder na FTA Decoder) yaani 89,000-34,000 ambayo ni 55,000. ukifanya hivyo utakuwa sawa na aliyenunua king'amuzi cha FTA utafurahia chanel zote za ndani bure muda wote.
Startimes tumekuwa tukijitahidi kuwaeleza wateja wetu kabla hawajanunua ving'amuzi vyetu, tofauti ya ving'amuzi hivyi ili kumpa nafasi mteja kufanya chaguo sahihi, lakini tumekuwa tunapata changamoto nyingi sokoni kwani mawakala na maagenti wetu wengi hawatoi taarifa hizi kwa wateja ipasavyo. Tafadhahari tunaomba radhi kwa usumbufu wowote ulioupata kama hukupata maelezo haya, Pia tunakukaribusha katika duka la startimes kwa ajili ya kubadilisha king'amuzi chako kuwa cha FTA. Startimes tutaendelea kufuata sheria na mwongozo toka kwa mamlaka husika
Ahsante!
Haaaaahaaa kumbe ndo hutambulika kwa hili jina?!Habari zenu star times! Mimi naitwa Stanslaus kimpanti Niko moro, napenda kujua hapo awali mlikuwa mnatuachia chanels za ndani tbc1,startv,Chanel ten na ITV tunaangalia free baadaye sijui nini kilitokea, mkaziondoa ikabaki tbc1 pekee.
Hamjaamua kuwaunganisha wateja wenu wote kwenye huduma ya FTA. Kama mmeona wateja hawana hela na mmeamua kuwalipisha hiyo hela kila mwisho wa mwezi kwa channneli za bure ni zaidi ya wizi. Je, TCRA wanataarifa juu ya mpango wenu au ndo njia yenu ya kuwapiga wananchi kwa kisingizio cha kusema "wantanzia wengi hawana hela".
Ushauri wangu kama mmeona umasikini ni kikwazo cha kuuza kwa bei halali fanyeni mpango wa kila mwisho wa mwezi mteja anapolipa mnakata asilimia kadhaa ili kufidia bei ya king'amuzi alichonunua, pindi pesa halali imetimia mnamuachia chanel zake za local lakini siyo hivi mnavyofanya ni zaidi ya uhuni.
Imma swala lingine naomben kama inawezekana msimu ujao mtuwekee EPL
Na ktk kuonesha kwenu baadhi ya ligi kwann msitumie lugha adhim ya kiswahili
Habari zenu star times
Mm ni mkazi wa mbagala nzasa Dsm
Mmiliki wa kisimbuzi namba
018 1939 5671
Mimi ni mteja wenu tangia enzi na enzi Kabla hamjaleta TV zenye visimbuzi mm nilikiwa na nyie mpaka sasa mmeshazileta nipo na nyie nahisi record zangu mnazo huko...
Shida yangu au lalamiko langu la kwanza ni jinsi mnavyokuwa nyumba ktk kujibu malalamiko yetu kupitia huduma kwa wateja namaanisha tunavyopiga cm na mnavyokawia kupokea kingine ktk page zenu nikianzia na facebook pamoja na hapa mnakawia sana kutoa majibu kwa wateja wenu.
Tuachane na hayo shida yangu kuwa ipo ktk kunitolea channel za dini ya kiislam.... TvIman siioni na Africa TV siooni tatzo nini.....
Kingine naitaji kulipia jTv naomben mwongozo
Habari mnaona hiki changu nilinunua 82900/= TZS mwaka 2011 sasa je na hiki kinahusiana vipi nakuzimwa na kunibakishia TBC 1 tu pekee kama free channel ina maana nyie data hamna za ku track hizi vitu au mnafanya kazi kwa mazoea?
View attachment 663506
Sawa nashukuruhabari yako Mediocrist, pole kwa usumbufu ulioupata, ni kweli inaonyesha kingamuzi chako ni kile kinachotakiwa kuonyesha chanel za bure, tafadhari fika katika ofisi ya startimes iliyokaribu new ili waweze kukusaidia.
STARTIMES mara nyingi hatupendi kumwambia mteja alipie kabla hatujajua tatizo ni nini!
Habari star times,habari yako mkananguja kuingizwa kwa radio za Tanzania kunategemea pia na utayari wa watoa huduma, startimes tunapenda wateja wetu wapate huduma hipi. Pia unaweza kubadilisha lugha katika king'amuzi chako kwa kwenya SETTING kisha chagua LANGUAGE unayotaka
Habari star times,
Nimekuwa mteja wa kisimbuzi X (jina nalihifadhi) kwa muda sasa, lkn sifurahii matangazo yao, sasa nimeamua kuwa moja ya familia yenu!
Napenda kujua yafuatayo;
Mosi, bei yenu ya ving'amuzi ( mm Niko Nyegezi mwanza)
Pili, ubora wa vipindi vyenu (program zenu zikoje)
Tatu, bei ya malipo kwa mwezi (yaani vifurushi vyenu vinaanzia tsh ngapi)
Asanten sana naomba majibu pia!
habari tutumie namba yako ya kadiMimi napata tbc tu yaani dah