Nimekua nikufuatilia vipindi vya mahojiano ya Star Tv kuhusu Katiba mpya. Waandishi (wanaohoji) wanaonyesha wazi wapo katika mkakati wa kuinga mkono UKAWA maswali yao yote ni elekezi. Au ndio mkakati wa M/kiti mpya wa CDM kuiteka Star TV. Kwanza wanawaleta watu wenye kiwango cha chini sana cha uwezo wa uchambuzi na sanasana wanaonekana ni makada wa CDM. Mmoja alikua hata hajavua T-shirt yake ya mkutano mkuu wa CDM. Nyinyi watangazaji na mwandaaji wa vipindi hivyo mjue kazi zenu ziko chini ya kiwango. Tunataka kusikia hoja si msimamo wa kichama. Maswali yenu laini na ningemshauri CEO wenu amwajiri salama wa Mkasi ana uwezo mkubwa sana wa kuhoji.
Last edited by a moderator: