Star TV mtakumbukwa kwa uchochezi

Star TV mtakumbukwa kwa uchochezi

BONGOLALA

JF-Expert Member
Joined
Sep 14, 2009
Posts
16,511
Reaction score
11,911
Leo nimeona tangazo la ccm limerushwa star tv,huku sauti ya Mh.Tundu Lissu ikiwa katika tangaZo hilo.Jee ni sawa tangazo la ccm kutumia picha za lowasa au sauti ya Lissu bila ridhaa ya wahusika?
Huo ni uchokozi na uchochezi ulio wazi,swali kwani ccm hakuna watu wa kufanya matangazo hayo?
Kwa nini kampeni za ccm zimekua zinaiba au kuchukua attention toka upinzani kujitangaza?
 
Nimewashangaa sana hata mimi. Hivi huyu Diallo ana akili nzuri kweli? It really shocked me. Bahati mbaya nilikuwa naangalia dira ya dunia otherwise nilishaachana na hawa wajinga.
 
Star Tv ni malofa hawana weledi kabisa,kuna tangazo la Lowasa la richmond wanasema msimchague Lowasa chagueni Magufuli,wananchi walishafanya maamuzi kuweka ukawa madarakani nyie star tv mnajaribu kuzima moto wa gesi kwa kutumia shuka!
 
Hata mimi huwa nai tune kwa ajiri ya BBC otherwise sitazami star tv!
 
Kikwete, tcra na NEC, hawaoni huu kama uchochezi? Wako kimya wanamruhusu Diallo atumie kituo chake kuleta chuki. Lakini machafuko yakitokea kituo chake hakitapona
 
Hivi kuna watu bado wanaiangalia tu mpaka leo?
 
Star Tv ni malofa hawana weledi kabisa,kuna tangazo la Lowasa la richmond wanasema msimchague Lowasa chagueni Magufuli,wananchi walishafanya maamuzi kuweka ukawa madarakani nyie star tv mnajaribu kuzima moto wa gesi kwa kutumia shuka!

Makosa yamefanywa kweli. Lkn Wananchi gani unawasemea?
 
Makosa yamefanywa kweli. Lkn Wananchi gani unawasemea?

kwa kweli star TV wanaboa sana wanafikiri upande waliopo ndio utakuwepo wanatakiwa wajue mwisho wao tarehe 25 October star tv someni alama za nyakati, imefikia hata wale watangazaji majembe wote wametoka waliobaki wote vimeo kwa ufupi hawana mvuto, diallo endelea na mkakati wako yatakutokea puani, kwa sasa star TV hamna mvuto tens.
 
kama mchochezi ni tundu lissu kwani yeye ndio alikuwa akizunguka nchi nzima kusema lowassa ni fisadi halafu ghafla anageuka maneno yake star tv wanasaidia kuweka kumbukumbu sawa kwani hawa ndio viongozi wanaohaidi kuhusu mabadiko ila wakipata madaraka wanasahau kile walichoahidi isitoshe kama tundu lissu anaona hatendewi haki akashitaki yeye si wakili anajua sheria
 
Waweke na sauti ya Lissu aliyoitoa Morogoro Kuwa mwenye Richmond in mwenyekiti wa chama tawala

Kwa kuwa anachofanya Diallo ni kuonesha chuki ya wazi dhidi ya Lowassa hawezi kufanya hivyo. Halafu mnadai eti ni msomi. Msomi of what category? This guy is behaving like someone who has never seen the inside of a classroom halafu anajiita msomi? Maawe!
 
Mnasikilizaje vyombo vya habari kama hivyo?
 
Back
Top Bottom