STAR TV: Iombeni radhi Zanzibar kwa kuitusi pamoja na kiongozi wao

Baraghash

JF-Expert Member
Dec 18, 2012
2,713
1,790
Jana asubuhi kwenye StarTV katika kipindi cha Tuongee asubuhi, chenye mada " sakata la Sukari" upande wa Dsm, alialikwa Mchambuzi wa mambo ya uchumi na siasa , aliebatizwa jina na mwenyekiti mwenza, kuwa "mzee wa data" Renatus Mkinga.

Katika muendelezo wa majadiliano, mara kwa ghafla na jazba,akatoka kwenye mada, akaanza kuisakama Zanzibar, kwa ruhusa ya muongozaji, Nd.Yussuf, kwa lugha ya kifedhuli, kiburi na isio na staha kwa Rais mstaafu wa Zanzibar Dr. Salmini Amour na utwala wake uliodumu miaka 10

Mkinga huku akiongozwa na mtangazaji Yussuf Kamoto alisema " Zakaria alimtia mfukoni Rais wa Zanzibar Dr Salmin Amour na utawala wake na alikuwa halipi kodi .......Zanzibar kuna maghala mengi ( wakati huu) yanayoficha sukari ya nyumbani na viwandani , iliokwisha muda wa matumizi........wanaichanganya na halafu kuileta bara wakijua kuwa ni sumu kwa binadamu "

Ya Zakaria na mwachia mwenywe kama atamuomba Mkinga kuyathibitisha hayo alioyasema, au Serikali ya Zanzibar kutuhumiwa kuwa wanaratibu ufichaji wa sukari na uchakachuaji wake, lakini kinachouma na kukisemea ni kumdhalilisha Rais wetu, jasiri, Komandoo Dr Salmini Amour kusema alitiwa mfukoni.

Hili ni kosa kubwa kufanyiwa Kiongozi wa nchi, huku mtangazaji mdhamini akishabikia ( bila ya kumkemea)
Mtukanaji huyu anaeonekana yuko juu ya sheria na maadili na alishakataliwa na vituo kadhaa kwa tabia yake hiyo

Zanzibar inastahili kuombwa radhi, isipokuwa tu kama StarTV ina sera za kuwatusi viongozi wa Zanzibar na watu wake.

Nakumbuka Mwl. Nyerere alipotuhumiwa kutiwa mfukoni na mgiriki mmoja, sote tunakijua kilichotokea ikabidi hata Rais Makarios wa Cyprus aingilie kati!
 
Mtoa mada unajichanganya sana !
Hapo nani anayetakiwa kuomba radhi, huyo aliyefanya ufisadi, au aliyeibua ufisadi wenye kuhatarisha maisha ya watu ?
 
Hahaaa hivi yule mzee anavyopayuka wanampendea nini?
Huwa nasikia akifoka kwenye tv ya nyumba ya jirani,mimi simsikilizi mtu asiyeenda na hoja bali anayo mambo yake aliyokuja nayo
 
Nimechanganyikiwa hapo pa kumhusianisha mtu aliyeacha urais miaka zaidi ya 15 na uhifadhi wa sukari wa sasa.
Nimekelewa, lakini aliemhusisha ni Mkinga, tena kwa jina. hoja hapa ni kutiwa mfukoni Rais wa nchi. Nyerere kila wakati alipenda kuikumbusha hadithi hiyo ya kutiwa mfukoni ijapokuwa iifanyika miaka mingi. Ahsante kwa mchango
 
Nimekelewa, lakini aliemhusisha ni Mkinga, tena kwa jina. hoja hapa ni kutiwa mfukoni Rais wa nchi. Nyerere kila wakati alipenda kuikumbusha hadithi hiyo ya kutiwa mfukoni ijapokuwa iifanyika miaka mingi. Ahsante kwa mchango

Mkuu kwani ni mara ngapi imetamkwa kwamba Kikwete na Familia yake wamewekwa mfukoni na HSC?

Tena mbaya zaidi ni kipindi ambacho Kikwete alikuwa ni Presidaa, kuna makanusho yoyote yalifanyika?

Kumbuka Gazeti la Dira.
 
Mtoa mada unajichanganya sana !
Hapo nani anayetakiwa kuomba radhi, huyo aliyefanya ufisadi, au aliyeibua ufisadi wenye kuhatarisha maisha ya watu ?
ngoja wasiombe radhi ndio utamjua fiisadi nani na malaika nani. Nani hapo alifichua ufisadi kuwa Komandoo alitiwa mfukoni na Zakaria. hilo ni tusi tu
 
Nadhani angetuthibitishia hayo aliyoyasema halafu akishindwa ndo aombe radhi.
Pili, huyu Zacharia ndo nani haswa? Maana namsikia sikia tu
 
Mkuu kwani ni mara ngapi imetamkwa kwamba Kikwete na Familia yake wamewekwa mfukoni na HSC?

Tena mbaya zaidi ni kipindi ambacho Kikwete alikuwa ni Presidaa, kuna makanusho yoyote yalifanyika?

Kumbuka Gazeti la Dira.
na wangapi wameshasitakiwa makosa ya mtandao kwa makosa mepesi zaidi ya hili. Ni kuomba radhi si kukanusha kwa vile jambo limeshafanyika.
 
Nadhani angetuthibitishia hayo aliyoyasema halafu akishindwa ndo aombe radhi.
Pili, huyu Zacharia ndo nani haswa? Maana namsikia sikia tu
Zakaria ni mtanzania, lakini kwa lugha za Mkinga anaitwa Mtanzania mwenye asii ya kiasia, bahati mbaya hatumsikii mtanzania mwenye asili ya kisomali
 
Mtoa mada unajichanganya sana !
Hapo nani anayetakiwa kuomba radhi, huyo aliyefanya ufisadi, au aliyeibua ufisadi wenye kuhatarisha maisha ya watu ?
Ndugu yangu Martinez, nani aliyefanya ufisadi? Kwa hiyo kwa maoni yako kwa kusema hivyo Mkinga ameibua ufisadi? Kama ndivyo hivyo basi tuna safari ndefu sana kama taifa! BTW Startv ni kituo cha kuonea huruma, wafanyakazi wanafanya kazi bila kulipwa mishahara, hivyo wakati mwingine akili zinakuwa nje ya kazi kabisa!
 
Ukawa hadi kufikia 2020 mtakuwa vichaa
Ukawa hadi kufikia 2020 mtakuwa vichaa

USSR;
Kweli nyani! Kha! Haonagi kundule! Hivi ambaye mpaka 2020 atakuwa tiyari kichaa ni nani kati yako na UKAWA? We wakumbuka maneno ya yule mzee wenyu wa Bunda? Si uliona alivyo galagazwa na kile kisichana?? Naye aliyasemaga maneno ya kufanana na hayo yako. UKAWA wanadunda ila yeye hata uropokaji wa chama hakupewa. Tunza mdomo ndugu
 
Back
Top Bottom