Pukudu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2011
- 3,148
- 2,219
Timu ya Stand Utd ya mkoani Shinyanga iko katika hatari ya kushuka daraja ikiwa na point 28. Na hii ni baada ya kupoteza mechi zke Tatu za ugenini za hivi karibuni.
Stand Utd kama timu zingine zilizokuwa ligi kuu Zina changamoto nyingi kubwa ni kipato. Pamoja na udhamini wa BinSlum kupitia matairi ya Double Star, Exim Bank, Vodacom, Azam TV bado imekuwa na hali ngumu kifedha ambayo imechangia kufanya Vibaya.
Usiku wa leo nimekuwa na hali ya usononi na stress ambayo imenisukuma kuandika uzi huu, kwa upande wangu Stand Utd nilianza kuipenda tangia ikiwa ligi ya wilaya, nimehudhuria mechi na mazoezi kwenye viwanja vya Buluba, Shycom na Sabasaba. Kwa wakazi wa Shinyanga tunajua kashkash timu iliyopitia kuanzia ubingwa wa wilaya, mkoa, hadi kuwa mabingwa wa mikoa na kwenda ligi daraja la kwanza na kupanda Ligi Kuu. Kumbuka stand Utd kwenye ngazi zote ilifanikiwa kupanda Bila kusuasua. Kwa nini tulegee ligi kuu?
Kusuasua kwa timu yetu kunatokana na matatizo mengi je? Ni uongozi? Ukata? Ushirikina? Wachezaji? Siasa? SHIREFA na SHIDEFA au wapenzi na mashabiki?
Kwa upande wangu naona unafiq wetu wadau umechangia na hii ni kutokana na kulea uovu, kukaa kimya na kujipa moyo mambo yatakuwa poa?
NB. hata Stand ikishuka sitashabikia Mwadui F. C ntahamishia mapenzi yangu Boko Haram F. C
Sio kama natafuta mtu wa kumuangushia jumba bovu, Bali naona ni bora tufunguke tuseme ukweli. Nawasubiri wadau aka Wana! Wa Chama la Wana. Najua wake watakaonichukia kwa kusema ntakachosema na nnajua wengi mtanifahamu ila poa tu.
Stand Utd kama timu zingine zilizokuwa ligi kuu Zina changamoto nyingi kubwa ni kipato. Pamoja na udhamini wa BinSlum kupitia matairi ya Double Star, Exim Bank, Vodacom, Azam TV bado imekuwa na hali ngumu kifedha ambayo imechangia kufanya Vibaya.
Usiku wa leo nimekuwa na hali ya usononi na stress ambayo imenisukuma kuandika uzi huu, kwa upande wangu Stand Utd nilianza kuipenda tangia ikiwa ligi ya wilaya, nimehudhuria mechi na mazoezi kwenye viwanja vya Buluba, Shycom na Sabasaba. Kwa wakazi wa Shinyanga tunajua kashkash timu iliyopitia kuanzia ubingwa wa wilaya, mkoa, hadi kuwa mabingwa wa mikoa na kwenda ligi daraja la kwanza na kupanda Ligi Kuu. Kumbuka stand Utd kwenye ngazi zote ilifanikiwa kupanda Bila kusuasua. Kwa nini tulegee ligi kuu?
Kusuasua kwa timu yetu kunatokana na matatizo mengi je? Ni uongozi? Ukata? Ushirikina? Wachezaji? Siasa? SHIREFA na SHIDEFA au wapenzi na mashabiki?
Kwa upande wangu naona unafiq wetu wadau umechangia na hii ni kutokana na kulea uovu, kukaa kimya na kujipa moyo mambo yatakuwa poa?
NB. hata Stand ikishuka sitashabikia Mwadui F. C ntahamishia mapenzi yangu Boko Haram F. C
Sio kama natafuta mtu wa kumuangushia jumba bovu, Bali naona ni bora tufunguke tuseme ukweli. Nawasubiri wadau aka Wana! Wa Chama la Wana. Najua wake watakaonichukia kwa kusema ntakachosema na nnajua wengi mtanifahamu ila poa tu.