Mr. SADC_TZ
Senior Member
- Nov 7, 2014
- 105
- 22
Aliyekuwa Mshambuliiaji wa mabingwa wa soka nchini Kenya Gor Mahia Dan Serenkuma amejiunga na kilabu ya Tanzania Simba SC.
Raia huyo wa Uganda alijiunga na kilabu hiyo ya Ligi ya Vodacom na kutamatisha kazi yake ya miaka mitatu katika ligi ya Kenya ambapo alianza kwa kuichezea Nairobi City Stars kabla ya kujiunga na Gor ambapo alikuwa kiungo muhimu katika ushindi wa ligi mara mbili.
''Nimefurahia miaka miwili na nusu katika kilabu ya Gor Mahia,lakini huu ndio wakati muhimu wa kuaga.Tumefurahia nyakati maalum na mafanikio pamoja,na habiki wamenisaidia sana hususan wakati mgumu'',Mfungaji huyo wa mabao mengi katika ligi ya Kenya aliandika katika mtandao wake wa Twitter.
''Ningependa kumshukuru kila mtu katika usimamizi wa kilabu kwa kunipa fursa muhimu ili kuonyesha kipaji changu.
Mchezaji huyo wa kimataifa katika timu ya Uganda Cranes alipigwa picha katika mtandao wa kilabu hiyo akifanyiwa majaribio pamoja na kupimwa afya na sasa anatarajiwa kujiunga na wachezaji wenzake katika barabara ya Msimbazi mjini Daresalaam tayari kwa maandalizi ya mechi za ligi ya Tanzania.
Wakati huohuo imebainika kwamba Kilabu ya Gor Mahia ilishindwa kumzuia mchezaji huyo.
Duru zimearifu kuwa mchezaji huyo aliandamwa na kilabu ya Gor mahia kufuatia ripoti za vyombo vya habari kwamba alitarajiwa kujiunga na Simba.
Lakini Gor Mahia haikuwasilisha ombi lolote la fedha kwa kuwa mchezaji huyo tayari alikuwa ameweka kandarasi yenye thamani ya shilingi millioni 3 pamoja na mshahara wa ksh.250,000 kwa mwezi na kilabu hiyo ya Tanzania ambapo atajiunga na mchezaji mwengine wa Gor Mahia Mungai Kiongera.
BBC Swahili
Kama sifa za magazetini, basi yanga ni kama wamenunua waandishi! Hebu tujikumbushe yaliyoandikwa kuhusu Jaja:-Ujio wa mshambuliaji mpya wa Simba SC, Daniel Sserunkuma unaibua maswali mengi kweli.Kutokana na Taswira ya ushindani ktk ligi yetu...je ataweza kuhimili changamoto za VPL.
-Kama Ushindani ktk ligi.
-Presha kutoka kwa mashabiki ya kumtaka afunge goli kila mechi.
-Sifa kutoka kwa Magazeti ya Udaku.
-Au tutegemee kama yaliyomkuta Mwenzake Hamisi Tambwe.
Msimu wa kwanza tu ..kawa Top scorer.... kashiba sifa kutoka kwa mashabiki na magazeti...sifa zikazidi..basi ndio kiwango kimeporomoka...!na hatimaye baada ya msimu mmoja arudi Gor Mahia.
Sserunkuma Na Mboob Wakikaa Pamoja Si Ndio Panatokea Mimba??
Kama sifa za magazetini, basi yanga ni kama wamenunua waandishi! Hebu tujikumbushe yaliyoandikwa kuhusu Jaja:
Jaja afunika mazoezini!
Jaja hapatoshi!
Jaja ni sheeeda!
Jaja haijapata tokea!
Nani kama Jaja!
Sasa badala ya kumzungumzia Tambwe aliyeng'aa walau msimu mmoja, hebu mzungumzie Jaja ambaye kuna mechi aligusa mpira mara nne dakika 80. Vivyo hivyo badala ya kumzungumzia SSerunkuma, hebu mzungumzie Emerson ambaye kwenye mazoezi yupo kikosi cha pili!
Sserenkuma mchezaji. Nashukuru simba kufanyia kazi ushauri wangu. Nilimwambia tangu ule usajili mkubwa uliopita tuachane na Kiongera kumchukue Dan 'Mzee' sserenkuma. Sijui kilitokea nini lakini nadhani wameliona sasa. Am happy
Mkuu lakini kumbuka huyu dogo ni kaanduje...kataweza kweli mikiki mikiki ya kina yondani na canavaro....mhhh...sijui lakini.
Je Yondan na Kanavaro ni warefu kuliko mabeki wote wa ligi ya Kenya . Mbona unaandika pointless, Messi mbona ananatesa SPAIN ni ngongoti. Nyie mlisajili Ngongoti Shikokoti liwafanyia nini?
Mboob ndp nani mkuu.....!
Uongozi wa Aveva umeamua kutufanyia kituko kingine ndugu zangu...huu usajili wa haka kachezaji kafupi...sina uhakika nao..simply because kachezaji kaliongoza kwa magoli kwenye kaligi ka kenya sasa nao simba ndio wameona mlango wa kupitia...haka kachezaji ni kafupi kwelikweli...nilikaona pale msimbazi kalikuwa kanaingia ndani kumwaga wino.
Najiulizaga hivi kweli kataweza kuwakabili akina Canavaro na Yondani.
kusema kweli simba yangu ya nsimuu huu ni Ashki Majnuni.Ngoja niende kwa mtani Yanga (kwa mkopo)...hadi msimu huishe.
We jamaa ni serunkuma kabisa kwa iyo unataka wamsajili hasheem thabeet au?
Mr. SADC_TZ kwani mpira huchezwa angani tu? Kenya kwenye mabeki ngongoti kama Shikokoti kawasumbua sana, iweje awashindwe mbilikimo wa Kandambili?
Subiri Mtani Jembe ndo utaona atawafanya nini nyinyi Kandambili. Na hatukuhitaji tena Msimbazi, ubaki huko huko.