Mcheza Karate
JF-Expert Member
- Jun 30, 2011
- 690
- 350
Kuna mengi yanasemwa kuhusu spika makinda kwa kuonyesha upendeleo wa wazi na dhati kwa serikali na chama tawala(CCM). Lakini la muhimu ni kufahamu kuwa spika makinda aliteuliwa kwa sifa zipi? Makinda aliteuliwa kwa sifa mbili kuu mosi ni "jinsia" na ya pili ni "utii" kwa chama chake. Mkinda angekuwa spika ule mwaka 1995 angekufa kwa presha. Mfano siku ya kuapishwa pius msekwa Masumbuko lamwai na Mabere marando wakiwa NCCR-mageuzi walimsumbua msekwa kwa kukataa kipo chake mara mbili mara ya tatu wakaridhia. Je makinda angeweza kwa kasi ile? Anachokifanya Makinda ni kusoma "gazeti" tu mbunge wa CCM akichangia au kutoa hoja lakini akisimama wa CHADEMA kutoa au kuchangia hoja na akaihoji serikali huinuka na kupiga yowe THIBITISHAAAAAAAA!!!!!!! Kwa tabia yake hiyo amejizolea marafiki wengi ni wale wavivu wa kutafakari. Kwa kweli MAKINDA ni lulu ya wanaoumwa akili na sio wale wenye weledi. Labla atabadilikaaa!!!