Spika Makinda hakumtendea haki mh.Halima Mdee.

Kwa wale waliofuatilia mjadala wa leo asubuhi bungeni, bila shaka wataungana nami kusema spika hakutenda haki ktk uamuzi alioutoa.
Kilichotokea ni kwamba mh. Ngeleja alitoa maneno ya kuudhi au kejeli alipokuwa akichangia na alitamka kwa kejeli kwa kuifananisha bajeti mbadala ya kambi ya upinzani na bajeti ya maandalizi ya harusi.Baada ya matamshi hayo na katika hali ya kushangaza mh.spika alimuacha aendelee kuchangia bila kumkatisha kwa maana ya kumtaka afute kauli yake kitu ambacho hakikuwa sahihi.Cha ajabu ni pale mh.Mdee aliposimama na kutoa taarifa kusahihisha upotoshaji wa Ngeleja na yeye bila shaka kwa kutaka kulipiza kisasi akaamua kumkejeli Ngeleja kwa kusema inaonekana Ngeleja ana uchungu wa kukosa uwaziri.Ghafla spika baada ya kauli hiyo ya mh Mdee akasimama na kumtaka afute kauli yake hiyo akidai kuwa kama hiyo ndio hoja bora asiendele kuchangia.Baada ya kauli hiyo ya mh spika, mh Mdee alikubali kufuta maneno yake.Sasa huu kama sio upendeleo au kutokutenda haki tusemeje?Mbona mh.Ngeleja alipotamka kuwa bajeti ya upinzani ni kama bajeti ya maandalizi ya harusi hakumtaka afute kauli yake!
Kwa kifupi spika,naibu wake na wenyeviti wa bunge hawatendi haki na kamwe wasitarajie kuwa bunge litakuwa na nidhamu kama mambo yataachwa yaendelee kama yalivyo.
Simamieni haki na usawa kwanza kabla ya kudai nidhamu ya wabunge mnaowaongoza.Vinginenyo ipo siku ngumi zitaibuka humo bungeni.

Kwa wenzetu CCM harusi inaandaliwa kwa mabilioni ya fedha labda ndiyo maana Spika aliamua kuwa biased kwa Ngereja. Umesahau vijisenti?
 
Toka lini ccm Dhaifu na Spika dhaifu akatoa haki akitoa nayo itakua Dhaifu, Issue hapa ni Mapambano mpaka kieleweke
 
Wote waseme lakini siyo Ngeleja, ameshasahau kipindi kama hiki cha bajeti kilivokuwa kigumu mpaka akasababisha Jailo kusimamishwa kazi. Mi nadhani huyu jamaa anamatatizo, sie tunasubiri uchunguzi kukamilika vile walivojiandalia mapokezi kama mashujaa baada ya kutimuliwa uwaziri.
 
Mwigulu Nchemba aliiita bajeti mbadala ya upinzani rubish hadi akafikia kuitupa chini. M/kiti Mambumba akawa anacheka tu. Imagine kama Mbunge wa CDM angeiita bajeti ya Mgimwa rubish halafu akaitupa chini ingekuwaje?

Mwigulu alimuita M/kiti wa CDM mcheza disco, imagine kama mbunge wa CDM ingemuita M/kiti wa nyinyiemu mgonjwa wa kifafa?

Mwigulu akamuita Tundu Lissu mwanasheria wa wachawi, imagine kama mbunge CDM angemuita Prof Maji Marefu Mchawi wa CCM, au angemuita Wassira mzee wa Gombe hivi kweli huyo M/kiti Sylivetser Mambumba angecheka kama alivyomchekea Mwigulu.

Binadamu huwa tuna hulka ya kusympathize na mtu/watu wanaonewa na wenye/mwenye nguvu. Kwa UPENDELEO huwo wa wazi lazima watanzania wengi watakuwa sympathize na CDM hilo tu linaweza kuifanya CDM IPENDWE na CCM ichukiwe.
 
Spika dhaifu kutoka chama dhaifu kinachoongozwa na mwenyekiti dhaifu hutetea wabunge dhaifu kwa kutumia tafsiri dhaifu za kanuni dhaifu wanapotoa hoja dhaifu...
duh! Nimecheka sina mbavu, hii imetulia!
 
Makinda na Makinda yake wanatumia wingi wao kutuburuza lakini 2015 watasaga meno ni swala la muda tu...
 
kwa hii, naendelea kukubali kuwa mnyika alichokisema ni sahihi "...udhaifu wa bunge na wabunge...hii kauli....dhaifu sitaifutaa" ahahaa ktmbe alimaanisha kwel. Mmhh

viongozi wa bunge la jmtanzania ni dhaifu.....haki huinua taifa bali dhambi ni aibu ya watu wote.....tendeni haki viongoziiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii...makindaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.....ndugaiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii....mnatukera sanaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Back
Top Bottom