kuna kitu lazima ukitambue , hatusemi ya kuwa kamati hii isifanye kazi za kuchunguza UDA lakini si wakati huu kwani kutakuwa na mwingiliano wa kazi wa tume na kamati,
kamati ilistahili kufanya kazi baada ya kufahamu serikali kupitia kwa CAG wamefanya nini katika uchunguzi na nini maamuzi ya serikali , kwani ili lipo wazi kabisa kwa CAG anafahamika kwa utendaji wake na pindi tunapoingiza mikono mingine ni marudio ya kazi zile zile
kwa sasa taasisi zilizotumwa kuchunguza UDA ni kama zifuatazo
1.CAG
2.TAKUKURU
3.KAMATI YA ZITTO
4. Halmashauri ya jiji
5.Usalama wa taifa
je kwa mwenye kutazama kwa nini ifike wakati tukatumia mabilioni ya shillingi kufanya kitu kimoja wakati taifa linaupungufu mkubwa wa fedha na nchi inaelekea kwenye janga la ukosefu wa mafuta , kwanini tume zingine sisiende kwenye majanga mengine kama ukosefu wa mafuta