Special Thread: CECAFA Senior Challenge Cup 2013

Special Thread: CECAFA Senior Challenge Cup 2013

Kipindi cha pili kimeanza...

Dk 47
Kenya 1 - 0 Sudan
 
Kenya wanafanya counter attack...Peter Opiyo anapiga shuti kali lakini linapita sentimita chache pembeni ya mlingoti na kuwa goalkick...

Dk 51

Kenya 1 - 0 Sudan
 
Dk 60
Kenya 1 - 0 Sudan

Kenya wamechachamaa washambulia kama nyuki kutoka pande zote za uwanja...wanacheza kwa moyo sana.
 
Kenya wanakosa goli la wazi...mpira unaopigwa na Lavatsa unagonga mwamba wa pembeni na kurejea uwanjani...

Dk 67

Kenya 1 - 0 Sudan
 
Goaaaaalllll

Allan Wanga anafunga bao safi la pili baada ya kumalizia vizuri krosi ya chini iliyopigwa toka wingi ya kulia na Philip Opiyo.

Dk 69
Kenya 2 - 0 Sudan
 
Sudan wameshikwa sana hii mechi...pasi haziendi za mbele...sioni namna yoyote kama watarudi.
 
Mara ya mwisho Kenya kubeba ndoo hii ilikuwa ni 2002 mashindano yakifanyika Mwanza Tanzania...

Naona leo ikiwa ni kumbukumbu ya miaka 50 ya uhuru wa Kenya, Kenya wanakaribia kubeba tena ndoo hii...ni suala la dakika chache tu sasa...
 
Dk 90
Kenya 2 - 0 Sudan

Zimeongezwa dakika 4 za nyongeza...
 
dakika zilizosalia hazitoshi hata kwa njiwa kumeza punje ya mtama....uwanja wa Nyayo ushaanza kuzizima kwa makelele na mwanamwali kashatolewa nje
 
Mpira umeishaaaa....

Kenya ndio mabingwa wapya wa Kombe la Chalenji la Cecafa 2013.

Mara ya mwisho Kenya kubeba ndoo hii ndani ya ardhi ya Kenya ilikuwa ni mwaka 1993.

Dk 90 + 3
Kenya 2 - 0 Sudan
 
Mara ya mwisho Tanzania kubeba hili kombe ni mwaka gani?
Mpira umeishaaaa....

Kenya ndio mabingwa wapya wa Kombe la Chalenji la Cecafa 2013.

Mara ya mwisho Kenya kubeba ndoo hii ndani ya ardhi ya Kenya ilikuwa ni mwaka 1993.

Dk 90 + 3
Kenya 2 - 0 Sudan
 
Back
Top Bottom