Soseji ni kitafunwa kinachopendwa sana,na hutumika sana kama sehem ya kifungua kinywa.Ni namna nyingine ya kuhakikisha unapata protini kwenye kifungua kinywa.
Hata ivyo soseji huweza kutumika kama sehem ya mlo wowote wa siku,kikubwa ni aina ya upishi au uandaaji ufanane na mlo wenyewe. kuna namna nyingi sana za kuandaa soseji,unaweza kuchemsha, kukaanga, kuchoma na hata kuoka.
Ingawa kuchemsha soseji ni njia rahisi,ya haraka na uacha soseji na harufu nzuri watu wengi hukosea sana namna ya kuchemsha soseji nakufanya wale soseji zisizokua na ladha nzuri na hazinukii viungo kabisa,na ndio maana utasikia wengi wakisema soseji hazina ladha.Ladha ipo tatizo ni uandaaji.
Njia. 1.weka soseji kwenye sufuria,weka maji kidogo sana kiasi cha kufikia nusu ya soseji zako endapo soseji zote zimegusa sufuria kwa chini (kama ilivyo katika picha).kama unachemsha paketi zima la soseji 12 basi weka maji robo kikombe.
ukiweka maji mengi zinapochemka ile ladha nzuri ya soseji hubaki kwenye maji,na kufanya ule soseji zisizokua na ladha wala harufu nzuri
2.Chemsha soseji kwa moto mdogo sana na hakikisha umefunika sufuria.
Lengo ni kuhakikisha joto (moto) linaingia ndani ya soseji ili kuivisha.unapofunika unatunza joto lote libaki kwenye sufuria na joto hilo huivisha soseji haraka.
Pia kufunika kunafanya harufu nzuri ya soseji isipotee
Ni vyema kujua kwamba soseji huiva haraka sana,na huitaji joto dogo tu ili kuiva.
3.Chemsha soseji adi maji yote yakauke .maji yakikauka inamaana utamu wote wa soseji umebaki kwenye soseji.ukiacha maji basi asilimia kubwa ya utamu utabaki kwenye maji
Hii ni moja ya sababu kwanini unachemsha kwa maji kidogo sana.
Mpaka hapo tayari kwa kula,utakula soseji zenye ladha nzuri na harufu inayovutia.
MAKOSA MADOGO YA KIUPISHI YANATOSHA KUPOTEZA LADHA YA CHAKULA
Soseji ziko,za aina tafauti, kuna za kuchoma ambazo ukichemsha hazifai. Hizi alizoonyesha dr MziziMkavu zinafaa kuchemsha ama kukaanga (kwa mafuta madogo sana hasa ukitumia a non-stick frying pan.
Soseji ziko,za aina tafauti, kuna za kuchoma ambazo ukichemsha hazifai. Hizi alizoonyesha dr MziziMkavu zinafaa kuchemsha ama kukaanga (kwa mafuta madogo sana hasa ukitumia a non-stick frying pan.
ni muhimu kusoma label chap chap ukiwa markiti.zile sausage za kuchoma zina spices nyingi sana, ila unaweza kuzikaanga kwa mafuta kidogo sana na moto mdogo sana.
majuzi nimepata surprise hapo, nimechukua tuna fish in salty water nikijua nimebeba my usual tuna fish in olive oil. namimina kwenye frying pan nashangaa ni maji. vitunguu vikalowaaa. vile mwalimu na kungwi wangu farkhina, nikachakachua na hiyo tuna na noodles wala haikuwa kituko.