Soon Diadora na Simba wanahamia kwenye raba. Mpo tayari?

Soon Diadora na Simba wanahamia kwenye raba. Mpo tayari?

DELETED ACCOUNT

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
9,805
Reaction score
15,472
Mdogo mdogo tunatoa vyombo vya kiulayaulaya. Niliwahi kuwaambia Italy ndiyo Mecca ya fashion na kamwe hawatoi vitu vibovu.

Baada ya kuwaonjesha jezi moja tu tena imevaliwa na mchezaji mmoja, nchi nzima imezizima inaongelea huo uzi. Hakukuhitajika sijui video za Amapiano, sijui warembo waliojichubua, sijui wasanii wala nini. Mchezaji mmoja na picha moja mgando baaasi. Na hapo unaambiwa hizo ni jezi za kuvaliwa mwezi mmoja tu halafu tunatupa tunaanza upya. Kuna watu wanatafuta kurogwa aisee.

Tunakaribia kuingia kwenye raba. Mimi tayari nimeshakusanya collection yangu ya Diadora. Wajanja tunapenda kuvaa vitu exclusive siyo unavaa kitu, kila mtaa unakutana na washamba washamba wana kitu hiko hiko.

1000108295.jpg


Diadora wanaenda kutengeneza pesa hadi wachanganyikiwe. Watanzania wakishapenda kitu hauwaambii lolote. Natabiri baada ya miaka 3 hivi itakuwa brand maarufu zaidi ya mavazi Tanzania.
 
Je ni wabongo wangapi wana uchumi wa kununua kiatu kimoja moja kwa dola 200 sidhani kama wana toleo la chini ya dola 100

Watatoa "Special for Africa; Special for Simba fans"!
Inabidi watengeneze bidhaa kulingana na soko. JayRutty akijipanga kuanzia kwenye jezi, raba na pamba za kawaida, Diadora itashika soko la mavazi. Kazi yake itabaki tu kucontrol bidhaa feki maana nazo zitakuwa nyingi.
 
Back
Top Bottom