mkuu ukijishangaa wewe kuna wenzio wanapitia mazito kuliko wewe ndani ya miaka miwili wamepukutika namaanisha kufariki watu sita kwenye familia moja kwa kufatana, alianza mama yao hawakumaliza arobaini akafariki mdogo wao kwachangamoto ya uzazi wakapumzika miezi kadhaa akafariki kaka yao aliekua msaada sana kwao haukupita mwezi akafa mdogo wao wa mwisho haukupita mwaka akafa kaka yao aliebakia hakupishan sana na mdogo wake wakike hivi nikuambiavyo wamebaki wawili tu mmoja anaumwa mmoja haeleweki makaz maalum
viatu vyako ni vizito mno, lakini jikaze wewe ndio faraja ya mkeo, ndio faraja ya mama yako, hio itoshe kukupa nguvu na ujasiri wa kuyashinda hayo, Muombe sana Mungu akusaidie utavuka ukikaza kiume hayo ni majaribu hicho kikombe utakivuka kwa uwezo wake