jamiimemba
Senior Member
- Oct 30, 2014
- 156
- 39
Ni vurugu ambazo vinatokea viwanja vya majimaji
=======
=======
Kimsingi dalili za kupigwa mabomu zilionekana hata kabla ya mechi kuanza kati ya Majimaji na Kurugenzi ya Mafinga. Leo polisi waliletwa wengi kias karibu kila mtu kujiuliza kuna nini leo. Mara baada ya mechi kuisha yakaanza malumbano kati ya polisi na watazamaji. Kisa chenyewe hasa ni kuzuia wananchi kupita eneo ambalo kulikuwa na gari la Mbunge Nchimbi. Hapo ikaonekana kana kwamba hawa polisi walikuja kumlinda Nchimbi. Wakaanza kuwazomea na kuwatukana kma vile kuwakejeli kuwa wameshindwa kulinda raia wanapoibiwa na kuvamiwa wanakuja kumlinda mtu ambaye hana madaraka yoyote yale kwa sasa kisa alikwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani. Hivi sasa polisi wamechukia kuzomewa