Somo muhimu toka medani za kivita kwa wanasiasa

VAPS

JF-Expert Member
Jul 10, 2012
5,610
13,160
Kama taifa tuna vita kubwa kupambana na maadui Ujinga, maradhi, umasikini (Ngazi ya Mtu, Kaya, Kijiji, Mtaa na Taifa).

Nifafanue kidogo ujinga mbali ya kusoma na kuandika lipo la ustawi na utawala bora. Hivyo hitaji la katiba bora linategemea hekima, busara, akili na utashi wetu kama taifa kujitambua.

Habari muhimu za adui ni vyenzo muhimu katika kupanga mashambulizi.Hivyo mbali ya tekinolojia watajitahidi wawezavyo kupandikiza watu wao ili kuweza kupata taarifa za adui kwa wakati.

Niwapongeze sana CHADEMA japo ni haki yenu, mbinu iliyotumika ni fursa muhimu kwa chama. Msipoteze muda wapeni baraka. Ndani masaa haya machache kubalini ofa uteuzi vile Viti Maalumu Rais msione aibu. Watanzania na dunia inajua yote. Mapambano yaendelee ndani na nje ya Bunge.
 
Ni vita Lissu achukue chama kushirikiana na lema!
Lissu, Lema, Mdee,..... wote ni wapambanaji chini ya CHADEMA. Matukio haya yanakiimarisha zaidi CHADEMA dhidi ya wahadhina wachache CCM.
 
Eti Viti maalum ni ofa? Wewe ndiye umetoa darasa la kivita😲😲 dah basi haya madarasa ni utopolo.
 
Eti Viti maalum ni ofa?? Wewe ndiye umetoa darasa la kivita dah basi haya madarasa ni utopolo
Tulia mkuu rudia kusoma, " japo ni haki yao".... mbinu waliyotumia... kujishusha na kuwaingiza king CCM, ofa ni viti vya JPM! kama sehemu kuwapoza CHADEMA.
 
Back
Top Bottom