Somo la uzalendo 🇹🇿 🇺🇸

Ukitembea sehemu mbalimbali Tanzania pia utaona bendera za CCM zinapepea kwenye nyumba nyingi ,magari mengi nimeyaona yakiwa na bendera na nembo za CCM, ofisi nyingi zina picha ya Mh.Rais,huu wote sio uzalendo kwako?

Nazungumzia uzalendo wa taifa; siyo unazi wa chama au vyama.
 
Taaratibu Ni zile zile bendera zinauzwa kwenye maduka ya bohari
 
Huku Tanzania uzalendo unapimwa kwa kupeperusha bendera za CCM kwenye nyumba,ukitembea huko maeneo ya pwani unakuta mtu nyumba ya tembe kaweka bonge la bendera ya kijani,yaani sisi ndiyo uzalendo wetu.
 
Usifananishe USA na vitu vya kijinga kasome emblem act ya mwaka1971 ndio uje upost
 
Uzalendo hauletwi kwa kuvaa Bendera ,wapo walio Vaa hizo Bendera na wengine wamezishonea kwenye Makaunda Suti yao na Dhamana tume wapa lakini ndio wa kwanza kuiuza Nchi kwa kuingia Mikataba isiyo na maslahi na Taifa lao.

Uzalendo unajengwa na mambo mengi ,kama kweli hawa Viongozi wetu wangekuwa Wazalendo tusingekuwa na Hali mbaya hivi Kiuchumi na kisiasa.Uzalendo hauletwi kwa kuhubiriwa kama Matangazo ya Biashara.
 
Chini ya Utawala wa huyu dikteta wa Kihutu jaribu sasa kupeperusha bendera kama hivyo hapa Tanzania kama hutapewa kesi ya kujaribu KUMPINDUA Maguzijuto...cheza na akili matope ya kijani wewe!
 

Naamini kwa Wamarekani wanaamini ktk Uzawa na si Uzalendo.

Uzalendo kwa Tz uko kwa chama twawala, na uzalendo wao ni mbioza mwenge, Sera zetu ni NA HATA HILI LITAPITA TU NA TUTASAHAU, tushasahau la Jana, tunasubiri kesho ifike na ipite

Hata hivyu uzalendo wa bendera ni uvivu tu wa kufikiri.

 
atakubaliana na mimi kuwa Wamarekani wapo kwenye kiwango kingine kabisa katika kuonyesha fahari ya uzalendo kwa nchi yao.
Wakati wa pambano la Mayweather and Mcgregor watu waliacha kupeperusha bendera ya Marekani na kupeperusha ile ya jamhuri ya Ireland, hapo utaona unafiki wa uzalendo wa bendera.

Na siku congress itakapo kubali reparation kwa ADOS (American descendants of slaves) hizo bendera hutaziona kwa hao hillbillies.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…