Kipenzi Changu
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 58,042
- 134,330
Rudisha kumbukumbu nyuma mpaka kipindi cha Saga la Buzwagi, Zitto akatimuliwa bungeni, nchi ikazizima kwa ajili yake, ''Baba yake'' Dr.Slaa akamtia moyo kijana akamwambia tunaenda kuishitaki CCM kwa watanzania juu ya huu ufisadi. Zitto akashika hatamu, akawa mtu muhimu mbunge wa kitaifa. Akawa mwenyekiti wa kamati nyeti sana, akalipua ufisadi, chama kikamwamini zaidi kikampa uwaziri kivuli Mambo ya Fedha.........................................................................Zitto akashika hatamu mitandaoni, akawa mwana JF, ikiletwa mada ya Zitto humu page si chini ya 20. Hata mimi nikawa CHADEMA aliyevutiwa na Zitto. Na wengi tu humu tuliipenda CHADEMA because of Zitto
Hali ya Sasa
Hali ya sasa inatia simanzi sana, japo hatua zilizochukuliwa na Chama naziunga mkono mia. Lakini namuonea huruma sana. Watu hawamuamini tena, amebaki Zitto wa facebook na twita. Sio yule tena wa kuitisha press conference akiwa na Dr.Slaa pembeni. Hata anapoibua ufisadi facebook/twita hakuna wa kumuunga mkono, watu wanamzodoa tu.Zitto amekuwa mtu wa kuzodolewa wakati alikuwa role model wa vijana katika siasa? Jamiiforums ndio usiseme, shukrani kwa Mods kwa kuficha threads zinazomnanga Zitto.
Kibaya zaidi haheshimiwi tena,wanaPAC hawamuheshimu tena chair wao.Kuna tetesi zinaenea kwny duru kuwa Zito amekula kichapo katika kugombea demu huko Malaysia.habari kamili zitawajia
My Take: Zitto ni case study ya Vijana wanasiasa