masai dada
JF-Expert Member
- Dec 29, 2013
- 16,701
- 16,375
Mawasiliano ya barabara kuu ya Dar es salaam -Lindi yamekatika tena katika eneo la Somanga kuanzia mchana hadi jioni hii leo April 16,2025 kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini ambapo hadi sasa hapapitiki.
Mmoja wa Watumiaji wa barabara ambao wapo eneo la tukio kuwa hadi wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipofika eneo hilo akiwa ameambatana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Stegomena Tax pamoja na Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega palikuwa panapitika lakini muda mfupi baada ya Viongozi hao kuondoka mvua kubwa imenyesha na kupelekea kutopitika.
Soma Pia: Kasheshe Somanga! Alipoenda kukesha Bashungwa na helkopta kumefurika tena, sasa ni zamu ya Ulega kutafuta kura
Kwa sasa kuna boti ndogo ya Serikali inavusha Watu lakini magari hayapiti.
Mmoja wa Watumiaji wa barabara ambao wapo eneo la tukio kuwa hadi wakati Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alipofika eneo hilo akiwa ameambatana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Stegomena Tax pamoja na Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega palikuwa panapitika lakini muda mfupi baada ya Viongozi hao kuondoka mvua kubwa imenyesha na kupelekea kutopitika.
Soma Pia: Kasheshe Somanga! Alipoenda kukesha Bashungwa na helkopta kumefurika tena, sasa ni zamu ya Ulega kutafuta kura
Kwa sasa kuna boti ndogo ya Serikali inavusha Watu lakini magari hayapiti.