INTROVERT MAN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2019
- 993
- 1,351
Majanga ya moto ni hatari sana hakuna asiyejua. Mali na rasilimali nyingi ikiwemo binadamu hupotea kimasihara tu.
Ajali za moto mashuleni kama iliyotokea jana imeleta simanzi nchi nzima.
Nimekaa na kufikiria kuwa dawa ya hili tatizo ni serikali kuamuru shule zote zenye mabweni ZIFUNGE UMEME WA SOLA badala ya umeme huu wa kawaida kwani ni nadra sana kuona sola imeleta moto.
Naomba Serikali isijali haya mabweni ya shule yako Dar es Salaam eti pana umeme au hapa ni bush Namtumbo yote yatandikwe sola.
Umeme wa TANESCO ni hatari kwani wanafunzi ni wakorofi kwa mfano matumizi ya simu kwa shule za sekondari ni yamekatazwa na hivyo mabweni mengi hayana socket kwa hiyo wanaomiliki hufanya utundu wa kuchubua nyaya ili wachaji simu. Ukiangalia hili ni kweli ndio maana vyuoni ni ngumu kuona majanga ya moto.
Wizara husika nawashauri agizeni shule zote zenye mabweni Tanzania nzima mabweni tu ndiyo yawekewe Umeme wa sola
Ajali za moto mashuleni kama iliyotokea jana imeleta simanzi nchi nzima.
Nimekaa na kufikiria kuwa dawa ya hili tatizo ni serikali kuamuru shule zote zenye mabweni ZIFUNGE UMEME WA SOLA badala ya umeme huu wa kawaida kwani ni nadra sana kuona sola imeleta moto.
Naomba Serikali isijali haya mabweni ya shule yako Dar es Salaam eti pana umeme au hapa ni bush Namtumbo yote yatandikwe sola.
Umeme wa TANESCO ni hatari kwani wanafunzi ni wakorofi kwa mfano matumizi ya simu kwa shule za sekondari ni yamekatazwa na hivyo mabweni mengi hayana socket kwa hiyo wanaomiliki hufanya utundu wa kuchubua nyaya ili wachaji simu. Ukiangalia hili ni kweli ndio maana vyuoni ni ngumu kuona majanga ya moto.
Wizara husika nawashauri agizeni shule zote zenye mabweni Tanzania nzima mabweni tu ndiyo yawekewe Umeme wa sola