Suzi Rafael
Member
- Sep 5, 2026
- 11
- 5
By Suzi Rafael
July 10 mwaka 1956 huko Pretoria, Afrika Kusini alizaliwa Solomon Mahlangu. Baba yake alitoweka mwaka 1962 kwenda kutafuta maisha lakini hakurejea, hivyo Solomon alilelewa na mama yake aliyeitwa Martha Mahlangu.
Akiwa sekondari yalitokea mauaji ya Soweto na akakimbilia Msumbiji katika kambi ya wakimbizi Xai Xai. Akiwa hapo alichukuliwa na viongozi wa ANC na kupelekwa kwenye mafunzo ya kijeshi nchini Angola.
Baadae yeye na kaka yake George Mahlangu na Mondy Motlong walipelekwa nchini Swaziland kwenye kambi ya ANC kwa mafunzo zaidi ya kijeshi.
June 1 mwaka 1977 walivuka Swaziland kwenda Johannersburg wakiwa na silaha kwenye mabegi. Walipofika wakachukua taxi.
Siku chache kabla ya kufika Johannersburg kulitokea mauaji. Watu wenye silaha walivamia duka moja, wakaua walinzi wawili na kupora. Polisi walikua katika harakati za kuwatafuta washukiwa wa tukio hilo.
Walipoliona gari la kina Mahlangu wakalitilia mashaka. Wakasimamisha na kupekua. Kwenye mabegi wakakuta baadhi ya silaha zikiwemo AK47.
Solomon na wenzie wakafanikiwa kukimbia, wakimuacha dereva taxi na mabegi yao. Solomon na Mondy Motloung walikimbilia sehemu moja huku George Mahlangu akikimbilia kivyake.
Baadae Solomon na Mondy walikamatwa na kuhusishwa na tukio hilo la mauaji. Mahakama kuu nchini humo ikawahukumu kunyongwa hadi kufa. Mawakili wao wakaomba kukata rufaa lakini wakakataliwa. Wakapeleka maombi mahakama ya rufaa ili itengue uamuzi wa mahakama kuu wa kuwakatalia kukata rufaa, lakini bado wakakataliwa.
April 06 mwaka 1979 wakanyongwa. Wakati wakipelekwa kwenye eneo la kunyongewa, Solomon alisema "Waambieni watu wangu kuwa nawapenda, na ni lazima waendelee na mapambano. Damu yangu itanyunyizia mti utakaozaa matunda ya uhuru. Aluta continue" Baada ya kusema maneno hayo akanyongwa na kufa.
Katika umri wa miaka 22 tu aliyobahatika kuishi, Solomon aliacha historia kubwa nchini Afrika kusini na barani Afrika kwa ujumla. Nchi nyingi zimekuwa zikimuenzi kwa namna mbalimbali. Nchini Tanzania, chuo kikuu cha Sokoine (SUA) kimeipa campus ya Mazimbu jina la Solomon Mahlangu campus.
VIJANA wa Karne hii, watakumbukwa Kwa kuendeleza anasa, michezo na mambo ambayo hayana mustakabali Kwa Taifa letu.
July 10 mwaka 1956 huko Pretoria, Afrika Kusini alizaliwa Solomon Mahlangu. Baba yake alitoweka mwaka 1962 kwenda kutafuta maisha lakini hakurejea, hivyo Solomon alilelewa na mama yake aliyeitwa Martha Mahlangu.
Akiwa sekondari yalitokea mauaji ya Soweto na akakimbilia Msumbiji katika kambi ya wakimbizi Xai Xai. Akiwa hapo alichukuliwa na viongozi wa ANC na kupelekwa kwenye mafunzo ya kijeshi nchini Angola.
Baadae yeye na kaka yake George Mahlangu na Mondy Motlong walipelekwa nchini Swaziland kwenye kambi ya ANC kwa mafunzo zaidi ya kijeshi.
June 1 mwaka 1977 walivuka Swaziland kwenda Johannersburg wakiwa na silaha kwenye mabegi. Walipofika wakachukua taxi.
Siku chache kabla ya kufika Johannersburg kulitokea mauaji. Watu wenye silaha walivamia duka moja, wakaua walinzi wawili na kupora. Polisi walikua katika harakati za kuwatafuta washukiwa wa tukio hilo.
Walipoliona gari la kina Mahlangu wakalitilia mashaka. Wakasimamisha na kupekua. Kwenye mabegi wakakuta baadhi ya silaha zikiwemo AK47.
Solomon na wenzie wakafanikiwa kukimbia, wakimuacha dereva taxi na mabegi yao. Solomon na Mondy Motloung walikimbilia sehemu moja huku George Mahlangu akikimbilia kivyake.
Baadae Solomon na Mondy walikamatwa na kuhusishwa na tukio hilo la mauaji. Mahakama kuu nchini humo ikawahukumu kunyongwa hadi kufa. Mawakili wao wakaomba kukata rufaa lakini wakakataliwa. Wakapeleka maombi mahakama ya rufaa ili itengue uamuzi wa mahakama kuu wa kuwakatalia kukata rufaa, lakini bado wakakataliwa.
April 06 mwaka 1979 wakanyongwa. Wakati wakipelekwa kwenye eneo la kunyongewa, Solomon alisema "Waambieni watu wangu kuwa nawapenda, na ni lazima waendelee na mapambano. Damu yangu itanyunyizia mti utakaozaa matunda ya uhuru. Aluta continue" Baada ya kusema maneno hayo akanyongwa na kufa.
Katika umri wa miaka 22 tu aliyobahatika kuishi, Solomon aliacha historia kubwa nchini Afrika kusini na barani Afrika kwa ujumla. Nchi nyingi zimekuwa zikimuenzi kwa namna mbalimbali. Nchini Tanzania, chuo kikuu cha Sokoine (SUA) kimeipa campus ya Mazimbu jina la Solomon Mahlangu campus.
VIJANA wa Karne hii, watakumbukwa Kwa kuendeleza anasa, michezo na mambo ambayo hayana mustakabali Kwa Taifa letu.