Sokwe Aagwa na Kuzikwa Kama Binadamu - Uganda

Sokwe Aagwa na Kuzikwa Kama Binadamu - Uganda

BUSAMUDA

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2014
Posts
612
Reaction score
358
Ni Sokwe mwenye jina la ZAKAYO ameagwa na waombolezaji waliokuwa wamekusanyika kwenye Kituo cha Elimu ya Wanyama Pori nchini Uganda.

Mwili wa Sokwe uliwekwe kwenye Jeneza Kisha waombolezaji walipita na kutoa heshima zao za mwisho kabla ya mazishi.
Historia na maisha ya Sokwe huyo ziliweza kusomwa kwa watalii na waombolezaji waliofika.

ZAKAYO ameacha mtoto mmoja - Shaka mwenye umri wa Miaka 17 na wake wawili - Amina na Ruth. Mtoto wake mmoja ambaye ni Yanki alifariki miaka michache iliyopita.

R.I.P - ZAKAYO
Aliandika mwandishi wa gazeti la The New Vision la nchini humo

IMG_2491.JPG
IMG_2492.JPG
IMG_2493.JPG
IMG_2494.JPG
IMG_2495.JPG
 
ameishi miaka 55 akiwa analishwa na kupatiwa uangalizi wa karibu na serikali/mashirika na amemucha mwanae Shaka (17) akiwanawake wawili tena akiwa chini ya uangalizi wa watu makini.
Kwaheri bwana Zakayo
 
Safi sana! Hawa sokwe ni cousin wetu halisi kabisa kihistoria sisi binadamu tulitoka kwao tukawaacha wao wameng'ang'ania usokwe sisi tukafuata na kuzingatia evolution hatimaye tukawa binadamu na wao wakabakia sokwe.

Hivyo sio mbaya kuwaaga ndugu zetu wa zamani.

R.I.P Baba Fifi Zakayo.
 
Lazima warudishe fadhila kwani amawaingizia fedha nyingi za kigeni kutokana na watalii waliokuwa wanakuja kumvutisha sigara na kumywesha pombe.
 
Kala chumvi kuzidi hata... .. . ..............
 
Lazima warudishe fadhila kwani amawaingizia fedha nyingi za kigeni kutokana na watalii waliokuwa wanakuja kumvutisha sigara na kumywesha pombe.


They made his death maana tunaambiwa drinking and smoking are unhealthy habits
 
Back
Top Bottom