Soko la Vitenge Nairobi

Soko la Vitenge Nairobi

NDESSA

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2013
Posts
1,946
Reaction score
1,801
Habari wanajanvi,naomba msaada kwa anayejua vizuri kuhusu kutoa vitenge Tz kupeleka Nairobi taarifa zisizo rasmi sana nilizopata ni kwamba vitenge vinanunuliwa sana huko,sasa kabla ya kwenda nimeona ni vizuri nikauliza kwenu wadau mnaopajua na pia kuhusu mpaka wa Namanga kupita na mzigo kuna vikwazo gani,Natanguliza shukrani.
 
Mpaka wa namanga hauna shida sana kwani wewe unachotakiwa kufanya ni kusafiri na mzigo wako kwenye basi kama unaenda tu mkoani.Upande wa kenya huwa hawakagui sana mizigo kwenye mabasi kama ilivyo upande wa tanzania.Jaribu kufanya utafiti wako vizuri kabla ya kwenda ili ujue bei ya soko ikoje,ili uweze kupata picha halisi ya bei utakayoenda kuuza.Usipofanikiwa kupata mtu anayejua nitakushauri uende na sample ya vitenge vichache ukaulizie mahali panaitwa nairobi textiles..hapo kuna maduka mengi ya vitambaa na vitenge.Jaribu kuulizia kama wananunua na ni kwa bei gani.Naamini utapata msaada mkubwa wa jinsi ya kupata soko la biashara yako ukifika hapo.
 
Mpaka wa namanga hauna shida sana kwani wewe unachotakiwa kufanya ni kusafiri na mzigo wako kwenye basi kama unaenda tu mkoani.Upande wa kenya huwa hawakagui sana mizigo kwenye mabasi kama ilivyo upande wa tanzania.Jaribu kufanya utafiti wako vizuri kabla ya kwenda ili ujue bei ya soko ikoje,ili uweze kupata picha halisi ya bei utakayoenda kuuza.Usipofanikiwa kupata mtu anayejua nitakushauri uende na sample ya vitenge vichache ukaulizie mahali panaitwa nairobi textiles..hapo kuna maduka mengi ya vitambaa na vitenge.Jaribu kuulizia kama wananunua na ni kwa bei gani.Naamini utapata msaada mkubwa wa jinsi ya kupata soko la biashara yako ukifika hapo.

Asante sana mkuu.
 
Habari wanajanvi,naomba msaada kwa anayejua vizuri kuhusu kutoa vitenge Tz kupeleka Nairobi taarifa zisizo rasmi sana nilizopata ni kwamba vitenge vinanunuliwa sana huko,sasa kabla ya kwenda nimeona ni vizuri nikauliza kwenu wadau mnaopajua na pia kuhusu mpaka wa Namanga kupita na mzigo kuna vikwazo gani,Natanguliza shukrani.
Hata mimi nimeshasikia hilo,na ni lazima inalipa kwa sababu kuna watu wanafanya,japo nasikia ni vitenge vya Kongo vinavyopendelewa zaidi....tafadhali nifahamishe na progress ya hii kitu.
 
Back
Top Bottom