Kutafsiri si kuweka maneno kandokando. Hii haina maana. Nakala laini ni kichekesho.
Ujiulize kwanza maana yake ni nini.
Hard copy - a document printed on paper (si ngumu!!! kama ingechongwa kwenye jiwe au kukatwa katika chuma ingekuwa ngumu)
Soft copy: a document available in digital format
Mandharinyuma ya lugha hii ni "hardware - software"
"Hardware" ni sehemu za kompyuta zinazofanywa na plastiki, metali nk. (hapa kuna ugumu kiasi.. kwa hiyo Kiwahili chake si "bidhaa ngumu" - ni maunzi ya kompyuta)
"Software" - neno hili lilitungwa mnamo 1958 kutaja yale ambayo yanaendesha kompyuta, yaani pogramu zake. Programu hizi kiasili ni mfululizo wa namba 0 na 1 kwa mpangilio tofautitofauti.
Siku hizi zinapatikana (bado kimsingi 0 na 1) kama data dijitali ndani ya "hardware". Kiswahili chake si "bidhaa laini" bali "programu"
Kwa hiyo ukitafuta neno la Kiswahili kwa softcopy taja yale jinsi yalivyo: Nakala dijitali.