Ochu
JF-Expert Member
- May 13, 2008
- 975
- 47
MWENYEKITI wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), Sophia Simba ambaye alilipua mabomu yaliyochafua hali ya hewa kwenye kikao cha Kamati ya Mwinyi na wabunge, sasa amehamishia makombora hayo ndani ya jumuiya yake.
Mama Simba sasa hamtaki katibu mkuu wake wa UWT ambaye ndio kwanza ameanza kazi, Mwananchi imebaini.
Taarifa ambazo Mwananchi umezikusanya kwa wiki nzima zinasema kuwa Mama Simba haelewani na katibu wake, Husna Mwilima ambaye aliteuliwa kushika nafasi hiyo katikati ya mwaka huu akitokea Hai mkoani Kilimanjaro ambako alikuwa mkuu wa wilaya.
UWT, ambayo uchaguzi wake ulitanguliwa na mtafaruku mkubwa baina ya Simba na mpinzani wake kwenye nafasi ya mwenyekiti, Janneth Kahama, ilianza mkutano wa baraza kuu la wanawake tangu jana na habari zinasema hali ya kutokuelewana kwa viongozi hao wawili ndiyo iliyotawala maandalizi na kusababisha baadhi ya viongozi wa CCM kuingilie kati.
Hali hiyo ya msuguano ilithibitika jana wakati mpasuko ulipojionyesha na kusababisha wengi wa wajumbe kuonyesha tofauti kubwa na viongozi hao.
Baada ya kuanza kwa kikao hicho cha baraza ambacho kilikwenda sambamba na mafunzo kwa viongozi hao, kulizuka hali ya kutokuelewana baina Simba na Mwilima, ambaye baadaye alipatwa na shinikizo la damu na hivyo kulazwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Alipoulizwa kuhusu ugonjwa wa katibu huyo wa UWT, mganga mkuu wa mkoa, Godfrey Mtey alisema kuwa hayupo mkoani Dodoma na akataka mwandishi awasiliane na kaimu wake, Jacob Chembele.
Hata hivyo, katibu huyo ambaye wauguzi waliiambia Mwananchi kuwa alilazwa wodi 18, aliruhusiwa kutoka hospitalini.
Husna Mwilima aliteuliwa hivi karibuni na vikao vya juu vya CCM kwa ajili ya kushika nafasi hiyo akitokea wilaya ya Hai.
Vyanzo kutoka ndani ya mkutano huo viliidokeza Mwananchi kuwa Simba na Mwilima wamekuwa na mgogoro wa chini chini na hadi sasa wameifanya jumuiya hiyo kumeguka vipande viwili kutokana na baadhi kumuunga mkono Mwilima na wengine wakiwa upande wa Simba.
"Sisi tumekuwa tukiwashangaa sana viongozi wetu, yaani huyu Mwilima kaingia juzi tu katika jumuiya na Simba naye bado ni mgeni katika nafasi aliyonayo, lakini wameanza kutupiana lawama kwa madai kuwa mmoja wao amefuja pesa za jumuiya, jamani hii ni aibu kubwa," alisema mmoja wa wajumbe kutoka moja ya mikoa ya Kaskazini.
Mjumbe huyo alisema kuwa tatizo linaloikabili jumuiya hiyo ni hali ya mitazamo ya viongozi wa juu katika jumuiya hiyo na akasema hivi sasa kumekuwa na matabaka ndani ya uongozi.
Kwa upande wake mmoja wa wabunge wa viti maalumu kutoka mikoa ya Magharibi alilidokeza Mwananchi kuwa si kweli kwamba Mwilima alikuwa amefuja pesa za chama, bali kilichofanyika ni kuwa mwenyekiti amekuwa hampendi tangu mwanzo kutokana na misimamo yake.
"Unajua tufike wakati lazima tuseme ukweli... huyu binti wa watu hana makuu kabisa, lakini tatizo limekuwa ni sisi maana akivaa vizuri, tunasema kuwa anajipenda, akibadili nguo tunasema kuwa anaiba hela... ah, ili mradi kumtwisha maneno mtoto wa watu bila hata sababu za msingi," alisema.
Habari zinasema katibu mkuu wa CCM, Yusufu Makamba na mwanansiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru waliingilia kati ili kunusuru balaa hilo na kufuta aibu ya jumuiya hiyo ambayo ni tegemeo kwa CCM.
Hata hivyo, pamoja na kasoro hizo, UWT ilipitisha katiba yake.
Simba amekuwa akitamba kwenye vyombo vya habari tangu alipotofautiana na Kahama katika kikao cha wanawake cha mkoa wa Dar es salaam.
Lakini, katika siku za karibuni amekuwa akiandikwa zaidi baada ya kutoa maneno makali kwenye kikao cha Kamati ya Mwinyi na wabunge baada ya kuripotiwa akimtetea waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuwa ni mwanamume wa shoka ambaye alijipatia utajiri zamani na kueleza kuwa tuhuma za kashfa ya Richmond dhidi yake ni za uongo.
Pia alimsafisha mwanasheria mkuu wa zamani, Andrew Chenge dhidi ya kashfa ya ununuzi wa rada.
Kama haitoshi, Simba, ambaye anaongoza wizara inayohusika na utawala bora, alimrushia kombora mwenyekiti na waziri mkuu wa zamani, John Malecela kuwa alipewa hela za kifisadi wakati akiwania kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM.
Alimrushia pia kombora Malecela na mkewe, Anne Killango kuwa harusi yao ilifadhiliwa na mtuhumiwa wa ufisadi, Jeetu Patel, huku akiwaelezea wabunge wanaojinadi kuwa wanapambana na ufisadi kuwa wanasumbuliwa na njaa.
Wote hawakujibu tuhuma zake, na badala yake Malecela alisema waziri huyo ni mgonjwa wa akili na akamshauri apitie hospitali ya wagonjwa wa akili ya Mirembe kabla ya kurudi jijini Dar es salaam.
Kama ni kweli, aliyemloga huyu mama ni kichaa
Mama Simba sasa hamtaki katibu mkuu wake wa UWT ambaye ndio kwanza ameanza kazi, Mwananchi imebaini.
Taarifa ambazo Mwananchi umezikusanya kwa wiki nzima zinasema kuwa Mama Simba haelewani na katibu wake, Husna Mwilima ambaye aliteuliwa kushika nafasi hiyo katikati ya mwaka huu akitokea Hai mkoani Kilimanjaro ambako alikuwa mkuu wa wilaya.
UWT, ambayo uchaguzi wake ulitanguliwa na mtafaruku mkubwa baina ya Simba na mpinzani wake kwenye nafasi ya mwenyekiti, Janneth Kahama, ilianza mkutano wa baraza kuu la wanawake tangu jana na habari zinasema hali ya kutokuelewana kwa viongozi hao wawili ndiyo iliyotawala maandalizi na kusababisha baadhi ya viongozi wa CCM kuingilie kati.
Hali hiyo ya msuguano ilithibitika jana wakati mpasuko ulipojionyesha na kusababisha wengi wa wajumbe kuonyesha tofauti kubwa na viongozi hao.
Baada ya kuanza kwa kikao hicho cha baraza ambacho kilikwenda sambamba na mafunzo kwa viongozi hao, kulizuka hali ya kutokuelewana baina Simba na Mwilima, ambaye baadaye alipatwa na shinikizo la damu na hivyo kulazwa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma.
Alipoulizwa kuhusu ugonjwa wa katibu huyo wa UWT, mganga mkuu wa mkoa, Godfrey Mtey alisema kuwa hayupo mkoani Dodoma na akataka mwandishi awasiliane na kaimu wake, Jacob Chembele.
Hata hivyo, katibu huyo ambaye wauguzi waliiambia Mwananchi kuwa alilazwa wodi 18, aliruhusiwa kutoka hospitalini.
Husna Mwilima aliteuliwa hivi karibuni na vikao vya juu vya CCM kwa ajili ya kushika nafasi hiyo akitokea wilaya ya Hai.
Vyanzo kutoka ndani ya mkutano huo viliidokeza Mwananchi kuwa Simba na Mwilima wamekuwa na mgogoro wa chini chini na hadi sasa wameifanya jumuiya hiyo kumeguka vipande viwili kutokana na baadhi kumuunga mkono Mwilima na wengine wakiwa upande wa Simba.
"Sisi tumekuwa tukiwashangaa sana viongozi wetu, yaani huyu Mwilima kaingia juzi tu katika jumuiya na Simba naye bado ni mgeni katika nafasi aliyonayo, lakini wameanza kutupiana lawama kwa madai kuwa mmoja wao amefuja pesa za jumuiya, jamani hii ni aibu kubwa," alisema mmoja wa wajumbe kutoka moja ya mikoa ya Kaskazini.
Mjumbe huyo alisema kuwa tatizo linaloikabili jumuiya hiyo ni hali ya mitazamo ya viongozi wa juu katika jumuiya hiyo na akasema hivi sasa kumekuwa na matabaka ndani ya uongozi.
Kwa upande wake mmoja wa wabunge wa viti maalumu kutoka mikoa ya Magharibi alilidokeza Mwananchi kuwa si kweli kwamba Mwilima alikuwa amefuja pesa za chama, bali kilichofanyika ni kuwa mwenyekiti amekuwa hampendi tangu mwanzo kutokana na misimamo yake.
"Unajua tufike wakati lazima tuseme ukweli... huyu binti wa watu hana makuu kabisa, lakini tatizo limekuwa ni sisi maana akivaa vizuri, tunasema kuwa anajipenda, akibadili nguo tunasema kuwa anaiba hela... ah, ili mradi kumtwisha maneno mtoto wa watu bila hata sababu za msingi," alisema.
Habari zinasema katibu mkuu wa CCM, Yusufu Makamba na mwanansiasa mkongwe nchini, Kingunge Ngombale Mwiru waliingilia kati ili kunusuru balaa hilo na kufuta aibu ya jumuiya hiyo ambayo ni tegemeo kwa CCM.
Hata hivyo, pamoja na kasoro hizo, UWT ilipitisha katiba yake.
Simba amekuwa akitamba kwenye vyombo vya habari tangu alipotofautiana na Kahama katika kikao cha wanawake cha mkoa wa Dar es salaam.
Lakini, katika siku za karibuni amekuwa akiandikwa zaidi baada ya kutoa maneno makali kwenye kikao cha Kamati ya Mwinyi na wabunge baada ya kuripotiwa akimtetea waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuwa ni mwanamume wa shoka ambaye alijipatia utajiri zamani na kueleza kuwa tuhuma za kashfa ya Richmond dhidi yake ni za uongo.
Pia alimsafisha mwanasheria mkuu wa zamani, Andrew Chenge dhidi ya kashfa ya ununuzi wa rada.
Kama haitoshi, Simba, ambaye anaongoza wizara inayohusika na utawala bora, alimrushia kombora mwenyekiti na waziri mkuu wa zamani, John Malecela kuwa alipewa hela za kifisadi wakati akiwania kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM.
Alimrushia pia kombora Malecela na mkewe, Anne Killango kuwa harusi yao ilifadhiliwa na mtuhumiwa wa ufisadi, Jeetu Patel, huku akiwaelezea wabunge wanaojinadi kuwa wanapambana na ufisadi kuwa wanasumbuliwa na njaa.
Wote hawakujibu tuhuma zake, na badala yake Malecela alisema waziri huyo ni mgonjwa wa akili na akamshauri apitie hospitali ya wagonjwa wa akili ya Mirembe kabla ya kurudi jijini Dar es salaam.
Kama ni kweli, aliyemloga huyu mama ni kichaa