Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Teknolojia ya habari na mawasiliano kwa kaisi kikubwa imeleta changamoto za haraka kwenye siasa za Tanzania. Sio siri tena, watendaji wa serikali "wanapelekwa" na upepo wa kwenye mitandao, huu wa JF ukiwa namba moja.
Kinachonishangaza ni pale mawaziri na watendaji wengine wanaposhindwa kutumia faida ya maendeleo ya sekta ya mawasiliano kurahisisha kazi zao.
Mathalani, mawaziri hawa wanne, pamoja na akina Chiza (ambaye hakutafuta suluhu katika mizani ya kuuzia mahindi!), wangeepuka fedheha hii kama wangeanzisha mawasiliano ya MOJA KWA MOJA na wananchi.
Najua kupokea simu za watanzania wote wenye matatizo ni ngumu. Lakini kwa nini kila waziri asitoe, na kuitangaza namba ya simu ambayo kila mwananchi mwenye kero au tatizo la dharura anatuma sms? Namba hiyo ikiunganishwa kwenye iPad ya waziri, na waziri akajipa kautaratibu ka kusoma msg kwa dakika 60 kila siku (tena anaweza kufanya hili hata akiwa safarini), huu uzembe wa kipuuzi puuzi usingetokea.
Kwa mfano operesheni tokomeza ujangili ilitekelezwa kwa zaidi ya siku 25, ni wazi kwamba mawaziri husika wangekuwa wa mwanzo kupata kilio cha wananchi, na kwa haraka sana wangeingilia kati na kuhakikisha yale mapungufu yanarekebishwa.
Sasa mawaziri mnategemea wasaidizi wenu na JF kutapa updates. Sio vibaya lakini mjue kwamba humu JF wengi wetu ni watu wa level ya kati ya maisha na tukaa mijini. Itakuwa ngumu sana kupata zile taarifa za kule ndani kabisa kwa wakati. Mitandao ya simu imeendea hadi vijijini siku hizi. Anzisheni mawasiliano ya moja kwa moja na wananchi sasa kwa kutumia simu za mikononi, mtaweza kudeal kiurahisi zaidi na changamoto zinazozikumba wizara zenu.
MSIWAAMINI, na narudia tena, msiwaamini wasaidi wenu. Wengi wao tuko nao huku mjini, wako bize wanasimamia biashara zao za mabasi, malori, maduka, mahoteli na mabaa... Ripoti nyingi wanazowapa kwenye mikutano ya hapo wizarani ni za uongo.
Ingawa wengine ni wapinzani lakini sio vibaya tukawashauri, maana tumechoka kila siku baraza jipya la mawaziri. Nchi itaendelezwa saa ngapi?...
Kinachonishangaza ni pale mawaziri na watendaji wengine wanaposhindwa kutumia faida ya maendeleo ya sekta ya mawasiliano kurahisisha kazi zao.
Mathalani, mawaziri hawa wanne, pamoja na akina Chiza (ambaye hakutafuta suluhu katika mizani ya kuuzia mahindi!), wangeepuka fedheha hii kama wangeanzisha mawasiliano ya MOJA KWA MOJA na wananchi.
Najua kupokea simu za watanzania wote wenye matatizo ni ngumu. Lakini kwa nini kila waziri asitoe, na kuitangaza namba ya simu ambayo kila mwananchi mwenye kero au tatizo la dharura anatuma sms? Namba hiyo ikiunganishwa kwenye iPad ya waziri, na waziri akajipa kautaratibu ka kusoma msg kwa dakika 60 kila siku (tena anaweza kufanya hili hata akiwa safarini), huu uzembe wa kipuuzi puuzi usingetokea.
Kwa mfano operesheni tokomeza ujangili ilitekelezwa kwa zaidi ya siku 25, ni wazi kwamba mawaziri husika wangekuwa wa mwanzo kupata kilio cha wananchi, na kwa haraka sana wangeingilia kati na kuhakikisha yale mapungufu yanarekebishwa.
Sasa mawaziri mnategemea wasaidizi wenu na JF kutapa updates. Sio vibaya lakini mjue kwamba humu JF wengi wetu ni watu wa level ya kati ya maisha na tukaa mijini. Itakuwa ngumu sana kupata zile taarifa za kule ndani kabisa kwa wakati. Mitandao ya simu imeendea hadi vijijini siku hizi. Anzisheni mawasiliano ya moja kwa moja na wananchi sasa kwa kutumia simu za mikononi, mtaweza kudeal kiurahisi zaidi na changamoto zinazozikumba wizara zenu.
MSIWAAMINI, na narudia tena, msiwaamini wasaidi wenu. Wengi wao tuko nao huku mjini, wako bize wanasimamia biashara zao za mabasi, malori, maduka, mahoteli na mabaa... Ripoti nyingi wanazowapa kwenye mikutano ya hapo wizarani ni za uongo.
Ingawa wengine ni wapinzani lakini sio vibaya tukawashauri, maana tumechoka kila siku baraza jipya la mawaziri. Nchi itaendelezwa saa ngapi?...