ugali dagaa
JF-Expert Member
- Oct 18, 2013
- 1,277
- 1,121
Salaam,
Nikiwa Moshi kama wiki mbili tatu zilizopita walikuja vijana watatu katika hoteli nayolala wamevaa fulana zina maandishi ya bol, wakanisalimu "shkamo blaza" kwani niikuwa nimewazidi umri.
Baada ya salam wakaniambia kuwa wao ni wawakilishi wanatoka kampuni ya mawasiliano ya BOL hii kampuni mi naifahamu kwa Dar ilikuwa na ofisi pale karibu na ubalozi wa ufaransa nakumbuka nilikuwa naenda pale kulipa "internet" lakini badae wakahamia pale makutano ya barabara ya Morogoro na Bibi Titi kuna jengo linamilikiwa na msalaba mwekundu.
Wale vijana wakaendelea kunipa ubora wa huduma yao kwamba laini zao zinatumia satellite kwa hiyo hakuna ardhi nitakayo kayanga chini ya jua nipoteze network nikavutiwa sana kwani shughuli zangu zinahusisha safari za mara kwa mara ndani na nje ya nchi hivyo nikawaza hakutakuwa na haja ya kubadilli line popote nitakapoenda wakanionesha na maandishi kwenye kile kiboksi ya line yameandikwa kwa lugha ya kizungu communication unlimited kweli aise walinishawishi nikajipatia line kwa gharama za shilingi elfu mbili wakanipa angalizo kwamba line ile inatumika kwenye smart phone zenye 3G na modem zinazoingia line zote na kwamba muda wa maongezi (vocha) nitanunua kwenye vibanda vya max malipo.
Baada ya kununua ile laini nikagundua ule mtandao haushiki network mpaka uwe katikati ya jiji la Dar es salaam pekee, namba zao za huduma kwa wateja hazipokelewi mara hazipatikani.
Kama kuna anayejua zaidi labda kuna maelekezo nakosea naombeni msaada manake hata ukifungua ukurasa wa jamiiforum kwenye computer lipo tangazo lao kubwa.
Nimemaliza.
Nikiwa Moshi kama wiki mbili tatu zilizopita walikuja vijana watatu katika hoteli nayolala wamevaa fulana zina maandishi ya bol, wakanisalimu "shkamo blaza" kwani niikuwa nimewazidi umri.
Baada ya salam wakaniambia kuwa wao ni wawakilishi wanatoka kampuni ya mawasiliano ya BOL hii kampuni mi naifahamu kwa Dar ilikuwa na ofisi pale karibu na ubalozi wa ufaransa nakumbuka nilikuwa naenda pale kulipa "internet" lakini badae wakahamia pale makutano ya barabara ya Morogoro na Bibi Titi kuna jengo linamilikiwa na msalaba mwekundu.
Wale vijana wakaendelea kunipa ubora wa huduma yao kwamba laini zao zinatumia satellite kwa hiyo hakuna ardhi nitakayo kayanga chini ya jua nipoteze network nikavutiwa sana kwani shughuli zangu zinahusisha safari za mara kwa mara ndani na nje ya nchi hivyo nikawaza hakutakuwa na haja ya kubadilli line popote nitakapoenda wakanionesha na maandishi kwenye kile kiboksi ya line yameandikwa kwa lugha ya kizungu communication unlimited kweli aise walinishawishi nikajipatia line kwa gharama za shilingi elfu mbili wakanipa angalizo kwamba line ile inatumika kwenye smart phone zenye 3G na modem zinazoingia line zote na kwamba muda wa maongezi (vocha) nitanunua kwenye vibanda vya max malipo.
Baada ya kununua ile laini nikagundua ule mtandao haushiki network mpaka uwe katikati ya jiji la Dar es salaam pekee, namba zao za huduma kwa wateja hazipokelewi mara hazipatikani.
Kama kuna anayejua zaidi labda kuna maelekezo nakosea naombeni msaada manake hata ukifungua ukurasa wa jamiiforum kwenye computer lipo tangazo lao kubwa.
Nimemaliza.