Slaa awang'ang'ania madiwani 7 Chadema

Slaa awang'ang'ania madiwani 7 Chadema

Umefika wakati Dr Slaa anapaswa awe makini sana na maamuzi yake..kama kila kosa ataangalia tu adhabu kwa mjibu wa taratibu za chama kama kwamba anaongoza malaika basi tutaharibikiwa muda si mrefu..si kila kosa ni kufukuza mtu au kumsimamisha uanachama..ambo mengine ya malizwe kidiplomasia...Kumpoteza mtu kama E.Nanyaro ndani ya chama hasa katika kipindi hiki ambacho CCM wanaonekana kuzinduka usingizini siyo afya kwa CHADEMA hata kidogo.Nimeliona hili Mkoani Geita, ambapo Katibu wa Bavicha, Bwana Paulo Vicenti,Mwenyekiti wake Otto na Mratibu wa Uenezi Bwn Filbeti, walifanya makosa ambayo kwangu niliona yanaweza kumalizika kwa njia ya kidiplomasia..lakini Dr aliwasimamisha uanachama...siyo siri kuondoka kwao kumesababisha cdm ifubae Geita...kama kuna mwana Geita hapa jamvini aliye genuine aje akanushe.Hawa vijana wameanza na chama wilayani hapa from zero, lakini kwa kosa moja tu wametupwa nje,nadiriki kusema wazi kuwa vijana hawa kama wangekuwepo tungeweza hata kushinda kata ya Lwenzera ambapo Dr.Slaa mwenyewe alifika kwenye kampeni lakini tukaambulia patupu. Nakumbuka vizuri maneno ya Mwenyekiti mteule wa CCM bwana MSUKUMA alivyokuwa akitamba hadharani kuwa cdm imefifia tangu wawaengue vijana hao na kwamba atatwaa kata ya Lwenzera bila msaada toka makao makuu ya ccm. Slaa tafakari
 
Tuwe wakweli huyu sasa ni unafiki wa hali ya juu!!
CDM haikumtambua rais Kikwete kwamba hakuchaguliwa kihalali 2010 na wakatoka nje ya bunge, lakini baada ya muda kwa maslahi ya taifa wakamtambua na viongozi mbalimbali wa CDM wamemwalika kikwete katika hafla zao na kumpongeza kwa mafanikio flani, alianza Dr Slaa alipomwalika JK kwenye hafla ya uchangiaji wa CCBRT, Kikwete alipokuwa Kilimanjaro wabunge wale walishiriki kwenye ziara zake na wakampongeza kwa mafanikio yake, mbona hawakukemewa na yeyote hawa? kwa kuwa ni viongozi wakubwa?
Madiwani hawa wadogo wameshiriki kwenye suala la jiji wanaambiwa Meya hakuchaguliwa kihalali, hivi kwa nini isifike wakati CDM ikubali kwamba tugange yajayo kwa manufaa ya wananchi? leo maamuzi na hoja za madiwani wa CDM hazifanyiwi kazi ila wanaoathirika ni wananchi, je, CDM inakosa huruma na hawa wananchi?
kuna ishu ya posho, madiwani wanalaumiwa kwa kuchukua posho, lakini bungeni CDM msimamo wake rasmi ni kutochukua posho hizo, wabunge kadhaa kama Shibuda, Selasini na Msigwa walisema wao hawataziacha na wabunge wengine kisirisiri hawaziachi isipokuwa Zitto, mbona hatumsikii Slaa akiwakoromea hawa kwamba wameenda kinyume na msimamo wa chama? je adhabu hizi si kwamba ni kwa wadogo tu?

muhimu, chama kfanye maamuzi ambayo hayawaathiri wananchi, wanachama wapewe adhabu ndani ya chama lakini maamuzi hayo yasiwaumize wananchi, vinginevyo wanachi wanaweza kujuta kwanini waliichagua CDM na next election wakaamua otherwise
 
Ni heri kukosa Madiwani kabisa au hata wabunge kuliko kuwa na viongozi wasioendana na kasi, mtazamo, msimamo na mkakati wa Chama. CCM ni nyumba ya majizi, mabakaji, mataahira, majuha, mafisadi;
 
Shida ya Watanzania tunapenda mabadiliko lakini bado hatujakuwa tayari kwa hayo mabadiliko?!

Mabadiliko si lele mama au si maongezi ya kwenye kahawa? Jiulizeni maswali Watanzania wenzangu! Je tunataka mabadiliko ktk hii nchi yetu?

Mkipata majibu ndo mchangie kwa kina kuhusu misimamo ya CHADEMA NA UTEKELEZWAJI WAKE! Ambao Dr Slaa anausimamia.

Tukienda kwa mwelekeo huu tunaotaka Watanzania wenzangu? Kila siku tutabaki na kusema oo Kinana kampuni yake ndo imesafirisha makontena ya Pembe za Ndovu?
Au ni kwanini mwizi wa kuku anafungwa? Wakati mwizi wa pesa za EPA anaambiwa akirudisha anasameewa?!

Tafakarini vizuri Watanzania wenzangu! Nchi inaliwa na hata asiye na meno? Iko siku mtajaulizwa maswali na wajukuu zetu na mkakosa majibu.
 
Hii sio CCM, kama sio makini nje!
Baada ya matokeo ya uchaguzi mwaka 2010 Slaa alisema hatambui matokeo na automatically ushindi wa urais kwa JK, hata ikapelekea JK akasema hata mkikataa mie ndio Rais wenu unakumbuka? Je hakuna viongozi wa CDM wanaoshirikiana na JK ambae hawakumtambua before? Na kama wapo wamepewa adhabu? Aache kuwaonea madiwani vidagaa hivyo. Mfano mzuri CDM walipoeenda Ikulu kuongea na JK ambae walishamkana. Acheni uonevu kama haki itendeke kote sio kupiga rungu kwa wadogo tu.
 
Nishaanza kupata picha! Kumbe Dr Slaa anataka madiwani wote wawe mapadri kama yeye! maana hao ndio hawafanyi makosa.
Mtoto akikunyoa kiganjani unaosha sio kukikata kiganja!
 
Back
Top Bottom